Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 136
  • Je, Maria Ni Mama ya Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Maria Ni Mama ya Mungu?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Abudu Muumba, Si Kilichoumbwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • “Tazama! Kijakazi wa Yehova!”
    Igeni Imani Yao
  • Je, Umepata Kujiuliza?
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 136
Maria akiwa na Yesu mchanga

Je, Maria Ni Mama ya Mungu?

Jibu la Biblia

La, Biblia haifundishi kwamba Maria ni mama ya Mungu, wala hakuna mahali inapodokeza kwamba Wakristo wanapaswa kumwabudu Maria au kumpa heshima kupita kiasi.a Fikiria hili:

  • Maria hakudai wakati wowote kwamba alikuwa mama ya Mungu. Biblia inaeleza kwamba alimzaa “Mwana wa Mungu,” si Mungu.​—Marko 1:1; Luka 1:32.

  • Yesu Kristo hakusema kamwe kwamba Maria alikuwa mama ya Mungu au kwamba alipaswa kupewa heshima ya pekee. Yesu hata alimkosoa mwanamke ambaye alimpa Maria heshima ya pekee ya kuwa mama yake, akisema: “Hapana, badala yake, wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”​—Luka 11:27, 28.

  • Maneno “Mama ya Mungu” na “Theotokos” (mzaa-Mungu) hayapatikani popote katika Biblia.

  • Maneno “Malkia wa Mbinguni” yaliyo katika Biblia, hayarejelei Maria, bali yanarejelea mungu wa kike wa uwongo aliyeabudiwa na Waisraeli walioasi imani. (Yeremia 44:15-19) Huenda “Malkia wa Mbinguni” alikuwa Ishtari (Astarte), mungu wa kike wa Babiloni.

  • Wakristo wa mapema hawakumwabudu Maria, wala hawakumtukuza kwa njia yoyote ya pekee. Mwanahistoria mmoja anasema kwamba Wakristo wa mapema “walipinga madhehebu na huenda waliogopa kwamba kumpa Maria uangalifu usiohitajika kungetokeza wazo la kwamba wanaabudu mungu wa kike.”​—In Quest of the Jewish Mary.

  • Biblia inasema kwamba Mungu amekuwepo sikuzote. (Zaburi 90:1, 2; Isaya 40:28) Kwa kuwa hakuwa na mwanzo, hawezi kuwa na mama. Isitoshe, Maria hangeweza kumbeba Mungu katika tumbo lake la uzazi; Biblia inaonyesha wazi kwamba mbingu haziwezi kumtosha Mungu.​—1 Wafalme 8:​27.

Maria Alikuwa Mama ya Yesu Si “Mama ya Mungu”

Maria alizaliwa katika taifa la Wayahudi, na alikuwa mzao wa ukoo wa Mfalme Daudi. (Luka 3:23-31) Alipendwa sana na Mungu kwa sababu ya imani na ujitoaji wake. (Luka 1:28) Mungu alimchagua awe mama ya Yesu. (Luka 1:31, 35) Maria alizaa watoto wengine ambao walikuwa wa Yosefu, mume wake.​—Marko 6:3.

Ingawa Biblia inaonyesha kwamba Maria alikuja kuwa mwanafunzi wa Yesu, hakuna habari nyingi za ziada zinazotolewa kumhusu.​—Matendo 1:14.

Kwa nini watu fulani humwona Maria kuwa mama ya Mungu?

Uthibitisho wa mapema zaidi wa watu kumheshimu Maria kwa njia ya pekee ni wa karne ya nne W.K. Wakati huo, Kanisa Katoliki lilikuwa dini rasmi ya Milki ya Roma. Kwa sababu hiyo, watu wengi ambao walitoka katika dini za kipagani walijiunga na dini zinazodai kuwa za Kikristo. Kanisa lilikuwa pia limeanza kufundisha fundisho la uwongo la Utatu.

Fundisho la Utatu liliwafanya wengi katika Kanisa Katoliki waanze kuamini kwamba ikiwa Yesu alikuwa Mungu, basi lazima Maria awe mama ya Mungu. Katika mwaka wa 431 W.K., baraza la kanisa kule Efeso lilimtangaza rasmi Maria kuwa “Mama ya Mungu.” Kutukuzwa kwa Maria kulienea sana baada ya Baraza hilo la Efeso. Na wale waliotoka katika dini za kipagani walipojiunga na kanisa, picha na sanamu za Bikira Maria zilichukua mahali pa miungu yao ya kike ya uzazi, kama vile Artemi (ambaye Waroma walimwita Diana) na Isisi.

Katika mwaka wa 432 W.K., Papa Sixtus wa Tatu aliagiza kwamba kanisa lijengwe jijini Roma ili kumtukuza “Mama ya Mungu.” Lilijengwa karibu na eneo ambalo zamani kulikuwa na hekalu lililojengwa ili kumtukuza Lucina, mungu wa kike wa uzazi wa Waroma. Mwandishi mmoja alifafanua kanisa hilo kuwa “ishara ya kudumu ya kupatanishwa kwa Mama Mkuu wa madhehebu ya kipagani na madhehebu ya Maria iliyotokea baada ya Roma kufanywa kuwa ya Kikristo.”​—Mary​—The Complete Resource.

a Dini kadhaa zinafundisha kwamba Maria ndiye mama ya Mungu. Huenda wakamwita “Malkia wa Mbinguni” au Theotokos, neno la Kigiriki linalomaanisha “mzaa-Mungu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki