Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 90
  • Nitaepukaje Maoni Yasiyofaa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nitaepukaje Maoni Yasiyofaa?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Unajionaje?
  • Kwa nini ni muhimu?
  • Unachoweza kufanya
  • Jifunze mengi zaidi
  • Hisiamoyo Zisizofaa— Zinaweza Kushindwaje?
    Amkeni!—1992
  • Mtazamo Unaweza Kuboresha Maisha Yako!
    Amkeni!—2016
  • Nifanye Nini Ikiwa Inaonekana Wengine Hawanipendi?
    Vijana Huuliza
  • Nifanye Nini Ikiwa Sitamani Kuendelea Kuishi?
    Vijana Huuliza
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 90
Mwanamke akiwa na maoni yasiyofaa wingu zito linapotanda na kumnyeshea

VIJANA HUULIZA

Nitaepukaje Maoni Yasiyofaa?

  • Unajionaje?

  • Kwa nini ni muhimu?

  • Unachoweza kufanya

  • Jifunze mengi zaidi

  • Vijana wenzako wanasema nini

Unajionaje?

  • Nina kawaida ya kutazamia mema

    “Ninajitahidi kuwa mwenye shangwe na kuishi na watu vizuri kadiri niwezavyo. Kwa nini nisiwe na tabasamu kila siku?”—Valerie.

  • Nina kawaida ya kutazamia mabaya

    “Ninapoona jambo zuri limefanyika, huwa ninatafuta kasoro—haiwezekani mambo yawe mazuri hivyo, labda hali itabadilika na kuwa mbaya.”—Rebecca.

  • Nina kawaida ya kuona mambo kihalisi

    “Mtu mwenye kutazamia mema hukatishwa tamaa, na mwenye kutazamia mambo mabaya wakati wote hukosa shangwe kila wakati. Kuona mambo kihalisi kunanisaidia kuona mambo kama yalivyo maishani.”—Anna.

Kwa nini ni muhimu?

Biblia inasema kwamba “mtu aliye na moyo mchangamfu huwa na karamu daima.” (Methali 15:15) Ni wazi kwamba watu wanaoepuka maoni yasiyofaa na kuishi wakiwa na mtazamo mzuri wanakuwa wenye furaha zaidi. Mara nyingi wanakuwa na marafiki wengi. Kwa kweli, ni nani ambaye angependa kushirikiana na watu ambao wana huzuni wakati wote?

Lakini bado kuna mambo ambayo lazima hata mtu mwenye mtazamo unaofaa zaidi atakabiliana nayo. Kwa mfano:

  • Kila mara vyombo vya habari vinatoa taarifa kuhusu vita, ugaidi na wizi.

  • Huenda ukakabiliana na matatizo ya kifamilia.

  • Bila shaka kuna wakati unapopambana na udhaifu wako mwenyewe na makosa yako.

  • Rafiki yako anaweza kuwa ameumiza hisia zako.

Badala ya kupuuza hali halisi zilizopo—au kuzikazia fikira kupita kiasi hivi kwamba unapoteza shangwe—jaribu kuwa na usawaziko. Kuona mambo kihalisi kutakusaidia kuepuka maoni yasiyofaa na kushughulika na changamoto za maisha bila kulemewa nayo.

Mwanamke anaanza kuwa na maoni yanayofaa mvua inapoacha kunyesha

Unapolemewa na mawingu mazito maishani, uwe na uhakika jua litatokea tena

Unachoweza kufanya

  • Kubali makosa yako.

    Biblia inasema hivi: “Hakuna mtu mwadilifu duniani atendaye mema daima bila kutenda dhambi.” (Mhubiri 7:20, Biblia Habari Njema) Kwa kuwa una udhaifu na unakosea inaonyesha kwamba wewe ni mwanadamu, haionyeshi kwamba hufai.

    Jinsi ya kuona mambo kihalisi: Jaribu kushinda udhaifu wako, lakini usitazamie kutenda kwa ukamilifu. Kijana fulani anayeitwa Caleb anasema hivi: “Ninaepuka kufikiria makosa yangu kila wakati, badala yake, ninajaribu kujifunza kutokana nayo na kuona jinsi yanavyoweza kunisaidia kuboresha mwenendo wangu.”

  • Epuka kujilinganisha.

    Biblia inasema hivi: “Tusiwe tukijisifu, tusichochee mashindano kati yetu, wala tusioneane wivu.” (Wagalatia 5:26) Unapotazama picha mtandaoni za sherehe zote ambazo hukualikwa unaweza kukasirika na kuvunjika moyo. Unaweza kuanza kuwaona rafiki zako wa karibu zaidi kuwa maadui wakubwa.

    Jinsi ya kuona mambo kihalisi: Kubaliana na ukweli wa mambo, hutaalikwa kwenye sherehe zote. Pia, habari zinazorushwa mtandaoni hazifafanui mambo kikamili. Kijana anayeitwa Alexis anasema kwamba “mambo yanayowekwa mtandaoni ni yale yanayoonekana kuwa yenye kusisimua zaidi maishani, watu hawarushi mambo ya kawaida mtandaoni.”

  • Uwe mwenye kufanya amani—hasa katika familia yako.

    Biblia inasema hivi: ‘Ikiwezekana, kwa kadiri inavyokutegemea wewe, fanya amani na watu wote.’ (Waroma 12:18) Huwezi kuongoza matendo ya watu wengine, lakini unaweza kudhibiti njia yako ya kutenda. Unaweza kuchagua kuwa mwenye kufanya amani.

    Jinsi ya kuona mambo kihalisi: Unaweza kuamua kuwa mwenye kufanya amani badala ya kuongezea familia yako mikazo, kama inavyopaswa kuwa katika urafiki wowote. Kijana anayeitwa Melinda anasema hivi: “Hakuna mtu mkamilifu, na kila mara tunakosana, kwa hiyo, inabidi tupange mapema jinsi tutakavyotenda—iwe ni kwa amani au la.”

  • Jifunze kuonyesha shukrani.

    Biblia inasema hivi: “Mjionyeshe kuwa wenye shukrani.” (Wakolosai 3:15) Kuwa na roho ya shukrani kutakusaidia kukazia fikira mambo ambayo yanaenda vizuri maishani mwako, badala ya mambo yote ambayo yanaenda mrama.

    Jinsi ya kuona mambo kihalisi: Kubali kwamba kuna matatizo maishani, lakini usipuuze mambo mazuri yanayotokea. Kijana fulani anayeitwa Rebecca anasema hivi: “Kila siku ninaandika jambo moja zuri katika kitabu changu cha kumbukumbu. Ninataka kujikumbusha kwamba nina mambo mengi mazuri ya kuendelea kutafakari.”

  • Chunguza watu unaoshirikiana nao.

    Biblia inasema hivi: “Kushirikiana na watu wabaya huharibu tabia nzuri.” (1 Wakorintho 15:33) Unaposhirikiana na watu wanaochambua-chambua mambo, wenye dhihaka, au wanaofungia kinyongo, mtazamo wao mbaya utakuathiri.

    Jinsi ya kuona mambo kihalisi: Rafiki zetu watapitia hali ngumu pindi fulani, na kwa muda huo, huenda wakashuka moyo na kuona mambo yakiwa mabaya tu maishani mwao. Wasaidie, lakini usiruhusu matatizo yao yakuathiri. Kijana fulani anayeitwa Michelle anasema hivi: “Usishirikiane na watu wenye mtazamo mbaya muda wote. Katika somo la hesabu, unapojumlisha namba mbili ambazo ni hasi, unakuwa na namba moja kubwa zaidi ambayo ni hasi.”

Jifunze mengi zaidi

Tunaishi katika kipindi ambacho Biblia inakiita “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1) Je, unaona ikiwa vigumu kudumisha mtazamo mzuri katika ulimwengu wenye maoni yasiyofaa? Soma “Kwa Nini Kuna Mateso Mengi Ulimwenguni?”

Vijana wenzako wanasema nini

Emma

“Nyakati fulani ninapojikuta nikifikiria kwa njia isiyofaa, mimi huandika orodha ya faida na hasara za jambo linalonisumbua. Hilo hunipa nafasi ya kutua na kuona mambo kihalisi, si kwa kutegemea hisia zangu. Mara nyingi, hata hali zinapoonekana kuwa mbaya sana, kunakuwa na mambo fulani mazuri.”—Emma.

Jesse

“Ninapokuwa na mtazamo usiofaa, ninatafuta fursa ya kumsaidia mtu au ninatafuta kitu ambacho ninaweza kufanya ili niwasaidie wengine. Yesu alisema kwamba kuna furaha katika kutoa, na kwa kawaida ninapotoa ninakuwa na usawaziko kwa kuwa ninaacha kukazia fikira hali mbaya ninazokabiliana nazo.”—Jesse.

Muhtasari: Nitaepukaje Maoni Yasiyofaa?

Kubali makosa yako. Jaribu kushinda udhaifu wako, lakini usitazamie ukamilifu.

Epuka kujilinganisha. Usihisi vibaya usipoalikwa kwenye sherehe.

Uwe mwenye kufanya amani—hasa katika familia yako. Usiongezee familia yako mikazo zaidi, fanya sehemu yako ili kuwe na amani.

Jifunze kuonyesha shukrani. Kubali kwamba kuna matatizo, lakini usipuuze mambo mazuri yanayotokea maishani mwako.

Chunguza watu unaoshirikiana nao. Tafuta rafiki ambao hawalemewi na matatizo yao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki