11 Na ikiwa baba yake hana ndugu, mtampa urithi wake mtu wa familia yake aliye wa karibu zaidi na mwenye uhusiano wa damu,+ naye atauchukua. Nayo itatumika kama sheria kulingana na uamuzi wa hukumu kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.’”