Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya zinazopatikana: Betsimisaraka (Northern), Betsimisaraka (Southern), Konkomba, Matses, Mi'kmaq
  • Leo

Jumamosi, Novemba 1

Kutoka katika vinywa vya watoto wadogo na wanaonyonya, umetoa sifa.—Mt. 21:16.

Ikiwa wewe ni mzazi, wasaidie watoto wako watayarishe maelezo yanayolingana na umri wao. Nyakati nyingine, mambo mazito kama vile matatizo ya ndoa au masuala ya kiadili, huzungumziwa wakati wa funzo, lakini huenda kuna fungu moja au mawili ambayo mtoto anaweza kutoa maelezo. Pia, wasaidie watoto wako waelewe kwa nini huenda hawatachaguliwa kila mara wanapoinua mkono. Kufafanua jambo hilo kunaweza kuwasaidia wasivunjike moyo watu wengine wanapochaguliwa. (1 Tim. 6:18) Sisi sote tunaweza kutayarisha maelezo yenye kujenga ambayo yatamletea Yehova heshima na kuwatia moyo Wakristo wenzetu. (Met. 25:11) Ingawa wakati mwingine tunaweza kutoa maelezo mafupi ya mambo tuliyojionea, tunapaswa kuepuka kuzungumza sana kujihusu. (Met. 27:2; 2 Kor. 10:18) Badala yake, tunajitahidi kumkazia fikira Yehova, Neno lake, na watu wake kwa ujumla.—Ufu. 4:11. w23.04 24-25 ¶17-18

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Novemba 2

Tusiendelee kulala usingizi kama wengine wanavyofanya, bali tukae macho na kutunza akili zetu.—1 The. 5:6.

Tunahitaji upendo ili tukae macho na kuendelea kutunza akili zetu. (Mt. 22:​37-39) Kumpenda Mungu kunatusaidia kuendelea kuhubiri licha ya changamoto zozote ambazo huenda tukakabili. (2 Tim. 1:​7, 8) Kwa kuwa tunawaonyesha upendo hata watu ambao hawamtumikii Yehova, tunaendelea kuhubiri, hata kutoa ushahidi kupitia simu na barua. Tunaendelea kutumaini kwamba siku moja jirani zetu watafanya mabadiliko na kuanza kutenda mambo yanayofaa. (Eze. 18:​27, 28) Pia, tunawapenda ndugu na dada zetu. Tunaonyesha upendo huo kwa “kutiana moyo na kujengana.” (1 The. 5:11) Kama wanajeshi wanaotumikia vitani bega kwa bega, sisi pia tunatiana moyo. Hatuwezi kamwe kuwaumiza kimakusudi ndugu na dada zetu au kulipa ubaya kwa ubaya. (1 The. 5:​13, 15) Pia, tunaonyesha upendo kwa kuwaheshimu ndugu wanaoongoza kutanikoni.—1 The. 5:12. w23.06 10 ¶6; 11 ¶10-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Novemba 3

[Yehova] akisema jambo, je, hatalitenda?—Hes. 23:19.

Njia moja tunayoweza kuimarisha imani yetu ni kwa kutafakari kuhusu fidia. Fidia inatuhakikishia kwamba ahadi za Mungu zitatimia. Tunapotafakari kwa makini kwa nini fidia ilitolewa na mambo yaliyohusika, tunaimarisha imani yetu kwamba ahadi ya Mungu kuhusu kuishi milele katika ulimwengu bora itatimizwa kwa uhakika. Kwa nini tunaweza kusema hivyo? Fidia ilihusisha nini? Yehova alimtuma Mwana wake mpendwa mzaliwa wa kwanza, mwandamani wake wa karibu zaidi, atoke mbinguni na kuzaliwa akiwa mwanadamu mkamilifu. Alipokuwa duniani, Yesu alivumilia hali ngumu mbalimbali. Kisha akateswa na kufa kifo chenye maumivu. Yehova alilipa bei kubwa sana! Mungu wetu mwenye upendo hangeruhusu kamwe Mwana wake ateseke na kufa ili tu kutuandalia maisha bora lakini ya muda mfupi. (Yoh. 3:16; 1 Pet. 1:​18, 19) Kwa kuwa alilipa bei kubwa sana, Yehova atahakikisha kwamba tutaishi milele katika ulimwengu mpya. w23.04 27 ¶8-9

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki