Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya zinazopatikana: Betsimisaraka (Northern), Betsimisaraka (Southern), Konkomba, Matses, Mi'kmaq
  • Leo

Jumanne, Novemba 4

Ewe Kifo, yako wapi maumivu yako makali?—Hos. 13:14.

Je, Yehova anatamani kuwafufua wafu? Bila shaka, anatamani kuwafufua. Aliwaongoza baadhi ya waandikaji wa Biblia kuandika kuhusu ahadi ya ufufuo wa wakati ujao. (Isa. 26:19; Ufu. 20:​11-13) Na Yehova anapotoa ahadi sikuzote yeye huitimiza. (Yos. 23:14) Kwa kweli, Yehova anatamani kuwafufua waliokufa. Fikiria maneno ambayo Ayubu alisema. Alikuwa na uhakika kwamba hata akifa, Yehova angekuwa na hamu kubwa ya kumwona akiishi tena. (Ayu. 14:​14, 15, maelezo ya chini) Bado Yehova anahisi hivyo kuelekea waabudu wake wote waliokufa. Anatamani kuwafufua, wakiwa na afya nzuri na furaha. Namna gani mabilioni ya watu ambao walikufa bila kupata nafasi ya kujifunza ukweli kumhusu Yehova? Mungu wetu mwenye upendo anataka kuwafufua pia. (Mdo. 24:15) Anataka wawe na nafasi ya kuwa rafiki zake na kuishi milele duniani.—Yoh. 3:16. w23.04 9 ¶5-6

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Novemba 5

Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu.—Zab. 108:13.

Unawezaje kuimarisha tumaini lako? Kwa mfano, ikiwa una tumaini la kuishi milele duniani, soma ufafanuzi wa Biblia kuhusu Paradiso na utafakari kuhusu mambo hayo. (Isa. 25:8; 32:​16-18) Fikiria jinsi maisha yatavyokuwa katika ulimwengu mpya. Jiwazie ukiwa huko. Ikiwa tutaendelea kufikiria kuhusu tumaini la ulimwengu mpya, matatizo yetu yatakuwa ya ‘muda mfupi na mepesi.’ (2 Kor. 4:17) Tumaini ambalo Yehova amekupatia linaweza kukutia nguvu. Tayari amekuandalia mambo unayohitaji ili upate nguvu kutoka kwake. Basi, unapohitaji msaada ili kutimiza mgawo fulani, kuvumilia jaribu, au kudumisha shangwe yako, sali kwa Yehova kwa bidii na utafute mwongozo wake kupitia funzo la kibinafsi. Waruhusu ndugu na dada zako Wakristo wakutie moyo. Dumisha tumaini lako likiwa jangavu na wazi akilini. Kisha utaimarishwa “kwa nguvu zote kwa uwezo [wa Mungu] wenye utukufu ili uvumilie kikamili kwa subira na shangwe.”—Kol. 1:11. w23.10 17 ¶19-20

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Alhamisi, Novemba 6

Toeni shukrani kuhusu kila jambo.—1 The. 5:18.

Tuna sababu nyingi za kumshukuru Yehova katika sala. Tunaweza kumshukuru kwa ajili ya kitu chochote kizuri tulicho nacho; kwa sababu kila zawadi njema hutoka kwake. (Yak. 1:17) Kwa mfano, tunaweza kumshukuru kwa dunia yetu maridadi na vitu vyenye kustaajabisha alivyoumba. Pia, tunaweza kumshukuru kwa uhai wetu, familia yetu, rafiki zetu, na tumaini letu. Na tungependa kumshukuru Yehova kwa kuturuhusu tufurahie urafiki wenye thamani pamoja naye. Huenda tukahitaji kufanya jitihada za pekee ili kufikiria sababu ambazo zinatufanya sisi binafsi tumshukuru Yehova. Tunaishi katika ulimwengu usio na shukrani. Mara nyingi watu hukazia fikira vitu wanavyotaka, badala ya kukazia fikira mambo wanayoweza kufanya ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya vitu walivyo navyo. Ikiwa tutaathiriwa na mtazamo huo, sala zetu zinaweza kuwa orodha ya mambo tunayotaka. Ili jambo hilo lisitokee, tunapaswa kuendelea kusitawisha na kuonyesha shukrani kwa ajili ya mambo yote ambayo Yehova anatufanyia.—Luka 6:45. w23.05 4 ¶8-9

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki