Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya zinazopatikana: Betsimisaraka (Northern), Betsimisaraka (Southern), Konkomba, Matses, Mi'kmaq
  • Leo

Jumatatu, Novemba 3

[Yehova] akisema jambo, je, hatalitenda?—Hes. 23:19.

Njia moja tunayoweza kuimarisha imani yetu ni kwa kutafakari kuhusu fidia. Fidia inatuhakikishia kwamba ahadi za Mungu zitatimia. Tunapotafakari kwa makini kwa nini fidia ilitolewa na mambo yaliyohusika, tunaimarisha imani yetu kwamba ahadi ya Mungu kuhusu kuishi milele katika ulimwengu bora itatimizwa kwa uhakika. Kwa nini tunaweza kusema hivyo? Fidia ilihusisha nini? Yehova alimtuma Mwana wake mpendwa mzaliwa wa kwanza, mwandamani wake wa karibu zaidi, atoke mbinguni na kuzaliwa akiwa mwanadamu mkamilifu. Alipokuwa duniani, Yesu alivumilia hali ngumu mbalimbali. Kisha akateswa na kufa kifo chenye maumivu. Yehova alilipa bei kubwa sana! Mungu wetu mwenye upendo hangeruhusu kamwe Mwana wake ateseke na kufa ili tu kutuandalia maisha bora lakini ya muda mfupi. (Yoh. 3:16; 1 Pet. 1:​18, 19) Kwa kuwa alilipa bei kubwa sana, Yehova atahakikisha kwamba tutaishi milele katika ulimwengu mpya. w23.04 27 ¶8-9

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Novemba 4

Ewe Kifo, yako wapi maumivu yako makali?—Hos. 13:14.

Je, Yehova anatamani kuwafufua wafu? Bila shaka, anatamani kuwafufua. Aliwaongoza baadhi ya waandikaji wa Biblia kuandika kuhusu ahadi ya ufufuo wa wakati ujao. (Isa. 26:19; Ufu. 20:​11-13) Na Yehova anapotoa ahadi sikuzote yeye huitimiza. (Yos. 23:14) Kwa kweli, Yehova anatamani kuwafufua waliokufa. Fikiria maneno ambayo Ayubu alisema. Alikuwa na uhakika kwamba hata akifa, Yehova angekuwa na hamu kubwa ya kumwona akiishi tena. (Ayu. 14:​14, 15, maelezo ya chini) Bado Yehova anahisi hivyo kuelekea waabudu wake wote waliokufa. Anatamani kuwafufua, wakiwa na afya nzuri na furaha. Namna gani mabilioni ya watu ambao walikufa bila kupata nafasi ya kujifunza ukweli kumhusu Yehova? Mungu wetu mwenye upendo anataka kuwafufua pia. (Mdo. 24:15) Anataka wawe na nafasi ya kuwa rafiki zake na kuishi milele duniani.—Yoh. 3:16. w23.04 9 ¶5-6

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatano, Novemba 5

Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu.—Zab. 108:13.

Unawezaje kuimarisha tumaini lako? Kwa mfano, ikiwa una tumaini la kuishi milele duniani, soma ufafanuzi wa Biblia kuhusu Paradiso na utafakari kuhusu mambo hayo. (Isa. 25:8; 32:​16-18) Fikiria jinsi maisha yatavyokuwa katika ulimwengu mpya. Jiwazie ukiwa huko. Ikiwa tutaendelea kufikiria kuhusu tumaini la ulimwengu mpya, matatizo yetu yatakuwa ya ‘muda mfupi na mepesi.’ (2 Kor. 4:17) Tumaini ambalo Yehova amekupatia linaweza kukutia nguvu. Tayari amekuandalia mambo unayohitaji ili upate nguvu kutoka kwake. Basi, unapohitaji msaada ili kutimiza mgawo fulani, kuvumilia jaribu, au kudumisha shangwe yako, sali kwa Yehova kwa bidii na utafute mwongozo wake kupitia funzo la kibinafsi. Waruhusu ndugu na dada zako Wakristo wakutie moyo. Dumisha tumaini lako likiwa jangavu na wazi akilini. Kisha utaimarishwa “kwa nguvu zote kwa uwezo [wa Mungu] wenye utukufu ili uvumilie kikamili kwa subira na shangwe.”—Kol. 1:11. w23.10 17 ¶19-20

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki