Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumapili, Julai 20

Mawazo yangu si mawazo yenu.—Isa. 55:8.

Ikiwa sala yetu haijibiwi, huenda tukahitaji kujiuliza, ‘Je, ninasali kuhusu jambo linalofaa?’ Mara nyingi, huenda tukafikiri kwamba tunajua jambo ambalo linatufaa zaidi. Lakini inawezekana mambo tunayoomba hata yasitunufaishe. Ikiwa tunasali kuhusu tatizo fulani, huenda kukawa na suluhisho bora zaidi kuliko lile tunaloomba. Na labda baadhi ya mambo tunayoomba hayapatani na mapenzi ya Yehova. (1 Yoh. 5:14) Kwa mfano, fikiria mfano wa wazazi ambao walimwomba Yehova amsaidie mtoto wao abaki katika kweli. Hilo linaonekana kuwa ombi linalofaa. Hata hivyo, Yehova hamlazimishi yeyote kati yetu amtumikie. Anataka kila mmoja wetu, kutia ndani watoto wetu, wachague kumwabudu yeye. (Kum. 10:​12, 13; 30:​19, 20) Hivyo, wazazi wanaweza kumwomba Yehova awasaidie kugusa moyo wa mtoto wao ili aweze kuchochewa kumpenda Yehova na kuwa rafiki Yake.—Met. 22:6; Efe. 6:4. w23.11 21 ¶5; 23 ¶12

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Julai 21

Endeleeni kufarijiana.—1 The. 4:18.

Kwa nini kuwafariji wengine ni njia muhimu ya kuwaonyesha kwamba tunawapenda? Kulingana na rejeo fulani la Biblia, neno “kufarijiana” ambalo Paulo alitumia linamaanisha “kusimama kando ya mtu na kumtia moyo anapopata majaribu makali.” Hivyo, tunapotoa faraja tunamsaidia mwabudu mwenzetu anayekabili hali ngumu, asimame na kuendelea kutembea katika barabara ya uzima. Kila mara tunapomfariji ndugu au dada yetu, tunamwonyesha upendo mwabudu mwenzetu. (2 Kor. 7:​6, 7, 13) Kuonyesha huruma na kufariji ni sifa zinazohusiana kwa ukaribu. Kwa njia gani? Mtu mwenye huruma huchochewa kuwafariji wengine na kujitahidi kuwapunguzia mateso yao. Hivyo, kwanza tunaonyesha huruma; kisha tunawafariji wengine. Ona jinsi Paulo anavyohusianisha huruma ya Yehova na faraja anayotoa. Paulo anamfafanua Yehova kuwa “Baba wa rehema nyororo na Mungu wa faraja yote.”—2 Kor. 1:3. w23.11 9-10 ¶8-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumanne, Julai 22

Tushangilie tukiwa katika dhiki.—Rom. 5:3.

Wafuasi wote wa Kristo wanaweza kutazamia kupata dhiki. Fikiria mfano wa mtume Paulo. Aliwaambia hivi Wathesalonike: “Tulipokuwa pamoja nanyi, tulikuwa tukiwaambia mapema kwamba tutapatwa na dhiki, na imekuwa hivyo.” (1 The. 3:4) Na aliwaandikia hivi Wakorintho: “Hatutaki mkose kujua, akina ndugu, kuhusu dhiki tuliyopata . . . Hatukuwa na uhakika hata kuhusu uhai wetu. (2 Kor. 1:8; 11:​23-27) Leo pia, Wakristo wanaweza kutazamia kupatwa na dhiki ya aina fulani. (2 Tim. 3:12) Kwa sababu ya kumwamini Yesu na kumfuata, huenda marafiki na watu wa ukoo wakakutendea kwa ukatili. Je, unapata matatizo kazini kwa sababu ya azimio lako la kuendelea kuwa mnyoofu katika mambo yote? (Ebr. 13:18) Je, umekabili upinzani kutoka kwa serikali kwa sababu ya kuwaambia wengine tumaini lako? Hata tukabili dhiki ya aina gani, Paulo anasema tunapaswa kushangilia. w23.12 10-11 ¶9-10

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki