Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Alhamisi, Julai 31

Endeleeni kuhakikisha jambo linalokubalika kwa Bwana.—Efe. 5:10.

Tunapotaka kufanya maamuzi muhimu, tunahitaji “kuyafahamu mapenzi ya Yehova” na kisha tutende kupatana nayo. (Efe. 5:17) Tunapotafuta kanuni za Biblia zinazohusu hali yetu, kwa kweli tutakuwa tukitafuta mawazo ya Mungu kuhusu jambo hilo. Kisha, kadiri tunavyotumia kanuni za Mungu, ndivyo tutakavyoweza kufanya maamuzi mazuri. “Yule mwovu,” adui yetu Shetani, angependa tutumie muda mwingi kufuatilia mambo ya ulimwengu huu, hivi kwamba tukose wakati wa kufanya utumishi wetu kwa Mungu. (1 Yoh. 5:19) Inaweza kuwa rahisi sana kwa Mkristo kutanguliza mali, elimu, au kazi yake badala ya kutafuta fursa za kumtumikia Yehova. Ikiwa jambo hilo litatokea, itaonyesha kwamba Mkristo huyo ameathiriwa na njia ya kufikiri ya ulimwengu. Kwa kweli, mali, elimu, au kazi si mambo mabaya, lakini hayapaswi kamwe kutangulizwa maishani mwetu. w24.03 24 ¶16-17

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Agosti 1

Mwadilifu ana matatizo mengi, lakini Yehova humwokoa kutoka katika matatizo hayo yote.—Zab. 34:19.

Ona mambo mawili muhimu katika Zaburi hiyo: (1) Watu waadilifu hukabili matatizo. (2) Yehova hutukomboa kutoka katika majaribu yetu. Yehova hutukomboa jinsi gani? Njia moja ni kwa kutusaidia kuona mambo kihalisi kwenye mfumo huu wa mambo. Ingawa Yehova anatuahidi kwamba tutapata shangwe tunapomtumikia, hajatuhakikishia kwamba hatutapatwa na matatizo sasa. (Isa. 66:14) Anatuhimiza tukazie fikira wakati ujao—wakati ambapo tutaishi maisha anayotaka tufurahie milele. (2 Kor. 4:​16-18) Kwa sasa, anatusaidia kuendelea kumtumikia kila siku. (Omb. 3:​22-24) Tunaweza kujifunza nini kutokana na mifano ya waabudu waaminifu wa Yehova wanaotajwa katika Biblia na wa nyakati zetu? Huenda tukakabili matatizo tusiyotarajia. Lakini tunapomtegemea Yehova, atatutegemeza sikuzote.—Zab. 55:22. w23.04 14-15 ¶3-4

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Agosti 2

[Jitiishe] kwa mamlaka zilizo kubwa.—Rom. 13:1.

Tunaweza kujifunza kutokana na mfano wa Yosefu na Maria, ambao walikuwa tayari kutii mamlaka zilizo kubwa hata ilipokuwa vigumu kufanya hivyo. (Luka 2:​1-6) Maria alipokuwa mjamzito kwa kipindi cha miezi tisa hivi, yeye na Yosefu walikabili jaribu la kutii. Augusto, ambaye alitawala Milki ya Roma, aliamuru watu wote waandikishwe. Yosefu na Maria walilazimika kusafiri kwenda Bethlehemu, safari ya kilomita 150 hivi wakipitia katika eneo lenye milima-milima. Safari hiyo haikuwa rahisi, hasa kwa Maria. Huenda wenzi hao walihofia usalama wao na wa mtoto wao ambaye bado hakuwa amezaliwa. Namna gani ikiwa Maria angepatwa na uchungu wa kuzaa wakiwa njiani? Tumboni mwake alikuwa amembeba Masihi wa wakati ujao. Je, wangetumia hali hiyo kuwa kisingizio cha kutotii serikali? Yosefu na Maria hawakuruhusu mahangaiko hayo yaamue ikiwa watatii sheria. Yehova aliwabariki kwa kutii. Maria aliwasili salama Bethlehemu, akajifungua mtoto mwenye afya, na hata akasaidia kutimiza unabii wa Biblia!—Mika 5:2. w23.10 8 ¶9; 9 ¶11-12

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki