Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hujui Ni Wapi Itafanikiwa!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
    • Wavu wa Kukokota

      15, 16. (a) Eleza kwa ufupi mfano wa wavu wa kukokota. (b) Wavu wa kukokota unawakilisha nini, na mfano huo unaonyesha jambo gani kuhusu ukuzi wa Ufalme?

      15 Jambo la maana zaidi si hesabu ya wale wanaodai kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo bali ni ubora wa wanafunzi hao. Yesu anazungumzia jambo hilo kuhusu ukuzi wa Ufalme anapotoa mfano mwingine kuhusu wavu wa kukokota. Alisema hivi: “Tena ufalme wa mbinguni ni kama wavu wa kukokota ulioshushwa ndani ya bahari na kukusanya samaki wa kila aina.”—Mt. 13:47.

      16 Wavu wa kukokota, ambao unawakilisha kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme, unakusanya samaki wa kila aina. Yesu anaendelea kusema hivi: “[Wavu wa kukokota] ulipojaa waliuvuta pwani na, baada ya kuketi, wakakusanya walio wazuri ndani ya vyombo, lakini wasiofaa wakawatupilia mbali. Hivyo ndivyo itakavyokuwa katika umalizio wa mfumo wa mambo: malaika watatoka kwenda na kuwatenga waovu kutoka katikati ya waadilifu nao watawatupa ndani ya tanuru ya moto. Humo ndimo watalia na kusaga meno yao.”—Mt. 13:48-50.

      17. Kazi ya kutenganisha inayotajwa katika mfano wa wavu wa kukokota inatukia katika kipindi gani cha wakati?

      17 Je, kazi hiyo ya kutenganisha inahusiana na hukumu ya mwisho ya kondoo na mbuzi ambayo Yesu alisema ingetukia wakati ambapo angekuja katika utukufu wake? (Mt. 25:31-33) Hapana. Hukumu hiyo ya mwisho itatukia Yesu atakapokuja wakati wa dhiki kuu. Kinyume chake, kazi ya kutenganisha inayotajwa katika mfano wa wavu wa kukokota inatukia wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo.”b Tunaishi katika kipindi hicho cha wakati—siku zinazotangulia dhiki kuu. Basi, kazi ya kutenganisha inafanywa jinsi gani leo?

      18, 19. (a) Kazi ya kutenganisha inafanywa jinsi gani leo? (b) Ni lazima watu wenye mioyo minyoofu wachukue hatua gani? (Ona pia maelezo ya chini yaliyo kwenye ukurasa wa 21.)

      18 Leo, kwa njia halisi, mamilioni ya samaki wa mfano kutoka katika bahari ya wanadamu wamevutwa kuingia katika kutaniko la Yehova. Wengine wao wanahudhuria Ukumbusho, wengine wanahudhuria mikutano yetu, na kuna wengine wanaokubali kujifunza Biblia. Lakini je, watu hao wote wanathibitika kuwa Wakristo wa kweli? Huenda ‘wanavutwa pwani,’ lakini Yesu anatuambia kwamba ni “walio wazuri” tu ndio wanaokusanywa ndani ya vyombo. Vyombo hivyo vinawakilisha makutaniko ya Kikristo. Samaki wasiofaa wanatupiliwa mbali, na mwishowe watatupwa katika tanuru ya moto ya mfano, inayofananisha uharibifu wa wakati ujao.

      19 Kama samaki wasiofaa, watu wengi ambao walikuwa wakijifunza Biblia na watu wa Yehova wameacha kujifunza. Wengine ambao walizaliwa na wazazi Wakristo hawataki kamwe kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu. Hawana nia ya kufanya uamuzi wa kumtumikia Yehova au wamemtumikia kwa muda kisha wakaacha.c (Eze. 33:32, 33) Hata hivyo, ni lazima watu wote wenye mioyo minyoofu wakusanywe ndani ya makutaniko ambayo ni kama vyombo kabla ya siku ya mwisho ya hukumu na waendelee kukaa mahali penye usalama.

  • Hujui Ni Wapi Itafanikiwa!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
    • b Ingawa andiko la Mathayo 13:39-43 linazungumzia jambo tofauti kuhusu kazi ya kuhubiri juu ya Ufalme, linatimizwa wakati mmoja na mfano wa wavu wa kukokota, yaani, wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo.” Kutenganishwa kwa samaki wa mfano ni kazi inayoendelea, kama vile kazi ya kupanda na kuvuna inavyoendelea katika kipindi hicho chote cha wakati.—Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 2000, ukurasa wa 25-26; Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, ukurasa wa 178-181, fungu la 8-11.

      c Je, hilo linamaanisha kwamba malaika wamemtupilia mbali kila mtu ambaye ameacha kujifunza au kushirikiana na watu wa Yehova kana kwamba hafai? Hapana! Njia imefunguliwa kwa mtu yeyote anayetamani kwa moyo wote kumrudia Yehova.—Mal. 3:7.

  • Hujui Ni Wapi Itafanikiwa!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
    • Tatu, si watu wote waliokubali ujumbe huo ambao wanathibitika kuwa wanafaa. Wengine wamekuwa kama samaki wasiofaa katika mfano wa Yesu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki