-
MatangazoHuduma ya Ufalme—2007 | Mei
-
-
Matangazo
◼ Toleo la Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutajitahidi kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha, tukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Juni: Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Pia kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa. Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutolewa: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je, Uamini Utatu?, Jina la,Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?
◼ Hundi zinazotolewa kama michango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote katika makusanyiko ya wilaya na zile zinazotumwa kwenye ofisi ya tawi ziandikwe jina la shirika linalotambuliwa kisheria katika nchi yenu.
◼ Mabaraza ya wazee yanapaswa kupitia barua ya Julai 6, 2006 kuhusu kujitayarisha kwa ajili ya msiba na wahakikishe kwamba wana habari za karibuni za kila mhubiri. Katika maeneo ambayo hukumbwa na misiba mara kwa mara, wazee wanapaswa kuwa na habari za ziada za jinsi wanavyoweza kuwasiliana na wahubiri wakati wa dharura. Mbali na wakati wa dharura, ingefaa wahubiri wamjulishe mwangalizi wa Funzo lao la Kitabu la Kutaniko au mzee mwingine ikiwa hawatakuwapo kwa muda mrefu kama vile ikiwa watasafiri kwenda likizo au safari za kikazi, ikiwa watalazwa hospitalini, au hali nyingine kama hizo.
-
-
Sanduku La SwaliHuduma ya Ufalme—2007 | Mei
-
-
Sanduku La Swali
◼ Wimbo wa kufungua Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, Mkutano wa Utumishi, Mkutano wa Watu Wote. na Funzo la Mnara wa Mlinzi unapaswa kutangazwa lini, na ni nani anayepaswa kufanya hivyo?
Nyimbo za kufungua mkutano wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi huorodheshwa katika Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inayopatikana katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba. Nyimbo za kufungua na kumalizia Mkutano wa Utumishi wa kila juma huonyeshwa kwenye ukurasa wa 2 wa Huduma Yetu ya Ufalme. Pia, namba za nyimbo za Funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma zinapatikana kwenye ukurasa wa 2 wa kila gazeti la Mnara wa Mlinzi. Kwa kuwa nyimbo zilizoteuliwa ni sehemu ya mkutano fulani hususa, zinapaswa kutangazwa na ndugu anayeongoza mkutano huo bali si na mwenyekiti wa mkutano uliotangulia.
Kwa mfano, mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi atakaribisha wasikilizaji, atatangaza wimbo wa kufungua, ataongoza shule, kisha atamkaribisha jukwaani msemaji wa kwanza wa Mkutano wa Utumishi. Ndugu aliye na sehemu hiyo ya Mkutano wa Utumishi ndiye anayepaswa kutangaza wimbo unaofungua Mkutano wa Utumishi.
Vivyo hivyo, Mkutano wa Watu Wote utaanzishwa na mwenyekiti. Atawakaribisha kwa uchangamfu wote waliohudhuria na kuwaalika washiriki kuimba wimbo wa kufungua ambao umeteuliwa na msemaji. Mwenyekiti (au labda ndugu mwingine anayestahili aliyepewa mgawo mapema) atafungua mkutano huo kwa sala. Kisha mwenyekiti atamtaja msemaji na kichwa cha hotuba yake. Baada ya hotuba, mwenyekiti atatoa shukrani kwa ufupi kwa ajili ya mafundisho hayo bila kurudia kwa muhtasari mambo ambayo msemaji amekwisha kuyasema. Mwenyekiti atatangaza kichwa cha hotuba ya watu wote itakayotolewa juma linalofuata, kisha atawaomba wote waliohudhuria wabaki kwa ajili ya Funzo la Mnara wa Mlinzi. Hakuna haja ya mwenyekiti kuomba wasikilizaji watume salamu kwenye kutaniko la msemaji anayezuru. Kisha, mwenyekiti atamkaribisha jukwaani kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi.
Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi atatangaza wimbo wa kwanza wa funzo hilo. Ataongoza funzo hilo kupatana na maagizo yaliyochapishwa kisha atatangaza wimbo wa kumalizia. Kwa kawaida, kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi atamkaribisha ndugu aliyetoa hotuba ya watu wote atoe sala ya kumalizia.
Miongozo hii ikifuatwa, mikutano yetu ya kutaniko itaendeshwa kwa umoja.
-