-
4 “Sheoli,” “Hadesi” Kaburi la Wanadamu WoteBiblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Matumizi Kumi ya Neno Hadesi, Yaani, Kaburi
Neno “Hadesi” ambalo huenda linamaanisha “mahali pasipoonekana” linapatikana mara kumi katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, nalo limetafsiriwa “Kaburi” katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki, yaani, katika Mt 11:23; 16:18; Lu 10:15; 16:23; Mdo 2:27, 31; Ufu 1:18; 6:8; 20:13, 14.
Katika Mdo 2:27, Petro anaponukuu Zb 16:10 inaonyesha kwamba Hadesi ni sawa na Sheoli na neno hilo linatumiwa kuonyesha kaburi la wanadamu wote (tofauti na neno la Kigiriki taʹphos, kaburi la mtu mmoja). Neno la Kilatini linalolingana na Hadesi ni in·ferʹnus (nyakati nyingine inʹfe·rus). Linamaanisha “kile kilicho chini; eneo la chini,” nalo linafaa kuhusu kaburi. Kwa hiyo linakaribiana vizuri na yale maneno ya Kigiriki na Kiebrania.
Katika Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu maneno “Sheoli” na “Hadesi” yanahusianishwa na kifo na wafu, wala si uhai na walio hai. (Ufu 20:13) Kulingana na maneno hayo yalivyo, hayana kamwe wazo au dokezo juu ya raha wala maumivu.
-
-
4 “Sheoli,” “Hadesi” Kaburi la Wanadamu WoteBiblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
“Hadesi” Kaburi la Wanadamu Wote
Kiebrania, שאול (sheʼohlʹ); Kigiriki, ᾅδης (haiʹdes);
-