Ufunuo
Ufunuo kwa Yohana
1 Ufunuo+ kupitia Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa,+ kuwaonyesha watumwa+ wake mambo ambayo lazima yatendeke upesi.+ Naye alimtuma malaika+ wake na kupitia yeye akautoa kwa njia ya ishara+ kwa mtumwa wake Yohana,+ 2 aliyetoa ushahidi kuhusu neno ambalo Mungu alitoa+ na kuhusu ushahidi ambao Yesu Kristo alitoa,+ naam, kuhusu mambo yote aliyoyaona. 3 Mwenye furaha+ ni yeye anayesoma kwa sauti+ na wale wanaosikia maneno ya unabii huu,+ na wanaoshika mambo yaliyoandikwa humo;+ kwa maana wakati uliowekwa uko karibu.+
4 Yohana kwa makutaniko saba+ yaliyo katika wilaya ya Asia:
Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja,”+ na kutoka kwa zile roho saba+ zilizo mbele ya kiti chake cha ufalme, 5 na kutoka kwa Yesu Kristo, “Shahidi Mwaminifu,”+ “Mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,”+ na “Mtawala wa wafalme wa dunia.”+
Kwake yeye anayetupenda+ na aliyetufungua kutoka katika dhambi zetu kupitia damu yake mwenyewe+— 6 naye alitufanya tuwe ufalme,+ makuhani+ kwa Mungu na Baba yake—ndiyo, kwake yeye na kuwe utukufu na nguvu milele.+ Amina.
7 Tazama! Anakuja na mawingu,+ na kila jicho litamwona,+ na wale waliomchoma;+ na makabila yote ya dunia yatajipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake.+ Ndiyo, Amina.
8 “Mimi ndiye Alfa na Omega,”+ asema Yehova Mungu, “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja,+ Mweza-Yote.”+
9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mshiriki pamoja nanyi katika dhiki+ na ufalme+ na uvumilivu+ kwa kushirikiana na Yesu,+ nilikuja kuwa katika kisiwa kinachoitwa Patmo kwa sababu ya kusema juu ya Mungu na kutoa ushahidi kumhusu Yesu.+ 10 Kwa uongozi wa roho+ nilikuja kuwa+ katika siku ya Bwana,+ nami nikasikia nyuma yangu sauti yenye nguvu+ kama ile ya tarumbeta, 11 ikisema: “Yale unayoona yaandike+ katika kitabu cha kukunjwa kisha uyatume kwa yale makutaniko saba,+ katika Efeso+ na katika Smirna+ na katika Pergamamu+ na katika Thiatira+ na katika Sardi+ na katika Filadelfia+ na katika Laodikia.”+
12 Nami nikageuka ili nione sauti iliyokuwa ikisema nami, na, nilipokuwa nimegeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,+ 13 na katikati ya vinara hivyo vya taa palikuwa na mtu kama mwana wa binadamu,+ aliyevikwa vazi lililofika chini miguuni, na aliyefungwa kifuani mshipi wa dhahabu. 14 Zaidi ya hayo, kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe,+ kama theluji, na macho yake kama mwali wa moto;+ 15 na miguu yake ilikuwa kama shaba safi+ inapowaka katika tanuru; na sauti+ yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi. 16 Na katika mkono wake wa kuume kulikuwa na nyota saba,+ na kutoka katika kinywa chake upanga mkali, mrefu na wenye makali kuwili+ ulikuwa umechomoka, na sura yake ilikuwa kama jua linapoangaza katika nguvu zake.+ 17 Nami nilipomwona, nikaanguka kana kwamba nimekufa miguuni pake.
Naye akaweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope.+ Mimi ndiye wa Kwanza+ na wa Mwisho,+ 18 na aliye hai;+ nami nilikufa,+ lakini, tazama! ninaishi milele na milele,+ nami nina funguo za kifo+ na za Kaburi.*+ 19 Kwa hiyo andika mambo uliyoyaona, na mambo yaliyopo na mambo yatakayotendeka baada ya haya.+ 20 Kwa habari ya siri takatifu ya zile nyota saba+ ulizoona juu ya mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu:+ Zile nyota saba zinamaanisha wale malaika wa yale makutaniko saba, na vile vinara saba vya taa vinamaanisha makutaniko saba.+