Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 uku. 1959
  • 4 “Sheoli,” “Hadesi” Kaburi la Wanadamu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 4 “Sheoli,” “Hadesi” Kaburi la Wanadamu Wote
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
4 “Sheoli,” “Hadesi” Kaburi la Wanadamu Wote

4 “Sheoli,” “Hadesi” Kaburi la Wanadamu Wote

Kiebrania, שאול (sheʼohlʹ); Kigiriki, ᾅδης (haiʹdes); Kilatini, in·ferʹnus; Kisiria, shiul

Tumetafsiri neno Sheoli na Hadesi kuwa “Kaburi.” Neno hili Kaburi tumetumia herufi kubwa ya “K” ili kulitofautisha na neno la kawaida la Kiswahili “kaburi.”

Matumizi 66 ya Neno Sheoli, Yaani, Kaburi

Neno la Kiebrania “Sheoli” linapatikana mara 66 katika Maandiko ya Kiebrania. Katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kiebrania, neno “Sheoli” linatumiwa mara 66 kama “Kaburi,” yaani, katika Mwa 37:35; 42:38; 44:29, 31; Hes 16:30, 33; Kum 32:22; 1Sa 2:6; 2Sa 22:6; 1Fa 2:6, 9; Ayu 7:9; 11:8; 14:13; 17:13, 16; 21:13; 24:19; 26:6; Zb 6:5; 9:17; 16:10; 18:5; 30:3; 31:17; 49:14, 14, 15; 55:15; 86:13; 88:3; 89:48; 116:3; 139:8; 141:7; Met 1:12; 5:5; 7:27; 9:18; 15:11, 24; 23:14; 27:20; 30:16; Mhu 9:10; Wim 8:6; Isa 5:14; [7:11]; 14:9, 11, 15; 28:15, 18; 38:10, 18; 57:9; Eze 31:15, 16, 17; 32:21, 27; Ho 13:14, 14; Amo 9:2; Yon 2:2; Hab 2:5.

Katika Maandiko ya Kiebrania matumizi ya “Sheoli” kama “Kaburi,” yanatia ndani zile mara 65 ambapo linatumiwa katika maandishi ya Kiebrania ya Masora, pia mara moja katika Isa 7:11, ambapo maandishi yana neno sheʼaʹlah, “omba,” lakini kwa kubadili kidogo ishara ya irabu na kwa kupatana na tafsiri ­mbalimbali za kale, neno hilo linasomeka sheʼoʹlah, “kuelekea Sheoli,” au, “kwenda Sheoli.” Mara zote ­Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inatumia “Kaburi” badala ya “Sheoli” ambalo ni neno la Kiebrania. Kwa ­ujumla ­Septuajinti ya Kigiriki ina­tafsiri ­sheʼohlʹ kuwa haiʹdes, yaani, Hadesi.

Ijapokuwa asili mbalimbali za neno la Kiebrania sheʼohlʹ zimeonyeshwa, inaonekana linatokana na kitenzi cha Kiebrania שׁאל (sha·ʼalʹ), kinachomaanisha “kudai” au “kutaka.” Jambo hilo linaelekea kuonyesha kwamba Sheoli (Kaburi) ni mahali (wala si hali) ambapo hutaka au kudai kuwapata wote bila kubagua, wakati wa kupokea ndani yake wanadamu wafu. Imo duniani na sikuzote inahusianishwa na wafu, na ni wazi Sheoli inamaanisha kaburi la wanadamu wote, au eneo la nchi (si la bahari) la wafu. Tofauti na hilo, neno la Kiebrania qeʹver linamaanisha kaburi moja au mahali pa kumzikia mtu mmoja.—Mwa 23:4, 6, 9, 20.

Matumizi Kumi ya Neno Hadesi, Yaani, Kaburi

Neno “Hadesi” ambalo huenda linamaanisha “mahali pasipoonekana” linapatikana mara kumi katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, nalo limetafsiriwa “Kaburi” katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki, yaani, katika Mt 11:23; 16:18; Lu 10:15; 16:23; Mdo 2:27, 31; Ufu 1:18; 6:8; 20:13, 14.

Katika Mdo 2:27, Petro anaponukuu Zb 16:10 inaonyesha kwamba Hadesi ni sawa na Sheoli na neno hilo linatumiwa kuonyesha kaburi la wanadamu wote (tofauti na neno la Kigiriki taʹphos, kaburi la mtu mmoja). Neno la Kilatini linalolingana na Hadesi ni in·ferʹnus (nyakati nyingine inʹfe·rus). Linamaanisha “kile kilicho chini; eneo la chini,” nalo linafaa kuhusu kaburi. Kwa hiyo linakaribiana vizuri na yale maneno ya Kigiriki na Kiebrania.

Katika Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu maneno “Sheoli” na “Hadesi” yanahusianishwa na kifo na wafu, wala si uhai na walio hai. (Ufu 20:13) Kulingana na maneno hayo yalivyo, hayana kamwe wazo au dokezo juu ya raha wala maumivu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki