Zaburi
Wimbo, muziki wa wana wa Kora. Kwa kiongozi juu ya Mahalathi kwa ajili ya maitikio. Maskili ya Hemani+ Mwezra.
4 Nimehesabiwa katikati ya wale wanaoshuka kuingia shimoni;+
Nimekuwa kama mwanamume ambaye hana nguvu,+
5 Aliyewekwa huru katikati ya wafu,+
Kama waliouawa ambao wanalala kaburini,+
Ambao huwakumbuki tena
Na ambao wametenganishwa na mkono wako wenye kusaidia.+
6 Umeniweka katika shimo lililo katika vina vya chini kabisa,
Katika mahali penye giza, katika abiso kubwa.+
8 Umewaweka rafiki zangu mbali nami;+
Umeniweka kuwa kama kitu chenye kuchukiza sana kwao.+
Niko chini ya kizuizi wala siwezi kwenda.+
9 Jicho langu mwenyewe limedhoofika kwa sababu ya mateso yangu.+
Nimekuitia wewe, Ee Yehova, mchana kutwa;+
Nimekunyooshea mikono yangu.+
10 Je, utawafanyia wale waliokufa jambo la ajabu?+
Au je, wale wasiojiweza katika kifo watasimama,+
Je, watakusifu wewe?+ Sela.
11 Je, fadhili zako zenye upendo zitatangazwa katika kaburi,
Na uaminifu wako katika mahali pa maangamizi?+
15 Ninateseka nami niko karibu kukata pumzi tangu uvulana;+
Nimevumilia sana vitu vyenye kuogopesha kutoka kwako.+