Methali
27 Usijisifu kwa sababu ya siku inayofuata,+ kwa maana hujui siku itazaa nini.+
2 Mwingine na akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mgeni na afanye hivyo, wala si midomo yako mwenyewe.+
3 Uzito wa jiwe na mzigo wa mchanga+—lakini usumbufu wa mpumbavu ni mzito kuliko vyote viwili.+
4 Kuna ukatili wa ghadhabu, pia furiko la hasira,+ lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?+
5 Karipio lililofunuliwa+ ni afadhali kuliko upendo uliofichwa.
6 Vidonda vinavyosababishwa na mpenzi ni vya uaminifu,+ lakini busu za mtu mwenye chuki zinapatikana kwa maombi ya kusihi.+
7 Nafsi ambayo imeshiba itakanyagia chini asali ya sega, lakini kwa nafsi yenye njaa kila kitu kichungu ni kitamu.+
8 Kama ndege anayekimbia kiota chake,+ ndivyo alivyo mtu anayekimbia mahali pake.+
9 Mafuta na uvumba+ ndivyo huufanya moyo ushangilie, ndivyo pia utamu wa rafiki ya mtu kwa sababu ya shauri la nafsi.+
10 Usimwache rafiki yako au rafiki ya baba yako, wala usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku ya msiba wako. Jirani aliye karibu ni afadhali kuliko ndugu aliye mbali.+
11 Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie,+ ili nipate kumjibu anayenidhihaki.+
12 Mtu mwerevu ambaye ameuona msiba amejificha;+ wasio na uzoefu ambao wamepita wamepatwa na mabaya.+
13 Ikiwa mtu amemwekea mgeni dhamana, lichukue vazi lake;+ na ikiwa amejihusisha na mwanamke mgeni, chukua rehani kutoka kwake.+
14 Anayembariki mwenzake kwa sauti kubwa asubuhi na mapema, itahesabiwa kwake kuwa ni laana.+
15 Paa inayovuja maji ambayo humfukuza mtu katika siku ya mvua inayonyesha mfululizo ni sawa na mke mgomvi.+ 16 Mtu yeyote anayemzuia, ameuzuia upepo, na mkono wake wa kuume hukutana na mafuta.
17 Chuma hunolewa kwa chuma. Ndivyo mtu anavyounoa uso wa mwingine.+
18 Anayeulinda mtini atakula matunda yake,+ naye anayemlinda bwana wake ataheshimiwa.+
19 Kama uso unavyolingana na uso kwenye maji, kadhalika moyo wa mwanadamu hulingana na moyo wa mwanadamu mwenzake.
20 Kaburi* na mahali pa uharibifu+ hazitosheki;+ wala macho ya mwanadamu hayatosheki.+
21 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha,+ na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu;+ na mtu hulingana na sifa yake.+
22 Hata ukimtwanga mpumbavu awe laini kwa mtwangio katika kinu, pamoja na nafaka iliyovunjika, upumbavu wake hautamtoka.+
23 Unapaswa kujua vizuri hali ya kundi lako. Elekeza moyo wako kwenye makundi yako;+ 24 kwa maana hazina haitadumu mpaka wakati usio na kipimo,+ wala taji kwa vizazi vyote.
25 Majani mabichi yameondoka, na majani mapya yametokea, na majani ya milimani yamekusanywa.+ 26 Wana-kondoo dume hufaa kwa mavazi yako,+ nao mbuzi-dume ni bei ya shamba. 27 Pia kuna maziwa ya kutosha ya mbuzi kuwa chakula chako, na cha watu wa nyumbani mwako, na riziki+ ya wasichana wako.