Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.+
2 Wewe mwenyewe umepata kujua kuketi kwangu na kusimama kwangu.+
Umeichunguza fikira yangu tokea mbali.+
4 Kwa maana hamna neno hata moja katika ulimi wangu,+
Lakini, tazama! Ee Yehova, tayari unajua yote.+
5 Nyuma na mbele umenizingira;
Nawe unauweka mkono wako juu yangu.
7 Ni wapi ninapoweza kwenda mbali na roho yako,+
Na ni wapi ninapoweza kukimbilia mbali na uso wako?+
8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa huko;+
Na kama ningetandika kitanda changu katika Kaburi,* tazama! ungekuwa huko.+
12 Hata giza lenyewe halingekuwa jeusi mno kwako,+
Lakini usiku wenyewe ungeng’aa kama mchana;+
Giza lingekuwa sawa tu na nuru.+
13 Kwa maana wewe mwenyewe uliumba figo zangu;+
Wewe uliniweka nikiwa nimekingwa katika tumbo la mama yangu.+
14 Nitakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.+
Kazi zako ni za ajabu,+
Kama vile nafsi yangu inavyojua vema.+
15 Mifupa yangu haikufichwa kwako+
Nilipofanyizwa katika siri,+
Nilipoungwa katika sehemu za chini kabisa+ za dunia.
16 Macho yako yalikiona kiini-tete changu,+
Na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa,
Kuhusiana na siku ambazo zilifanyizwa+
Na hakukuwako hata moja kati ya hizo.
17 Kwa hiyo, jinsi mawazo yako yalivyo yenye thamani kwangu!+
Ee Mungu, jinsi jumla yake yote ilivyo kuu!+
18 Kama ningejaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko hata chembe za mchanga.+
Nimeamka, na bado niko pamoja nawe.+
19 Laiti wewe, Ee Mungu, ungemuua mwovu!+
Ndipo hata watu wenye hatia ya damu+ hakika wangeniondokea,