-
Thamini Zawadi ya UhaiFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Tunawezaje kumwonyesha Yehova kwamba tunathamini zawadi ya uhai?
Tangu ulipokuwa tumboni kabla hujazaliwa, Yehova alikutunza. Katika Biblia, Daudi mtumishi wa Yehova alisali hivi: “Macho yako hata yaliniona nikiwa kiinitete.” (Zaburi 139:16) Uhai wako ni wenye thamani kubwa machoni pa Yehova. (Soma Mathayo 10:29-31.) Yehova huhuzunika sana mtu anaposababisha kimakusudi kifo cha mtu mwingine, au hata kifo chake mwenyewe.a (Kutoka 20:13) Yehova huhuzunika pia tunapohatarisha uhai wetu isivyo lazima au tunapokosa kuchukua tahadhari ili kulinda uhai wa wengine. Tunapolinda uhai wetu na kuheshimu uhai wa watu wengine, tunaonyesha kwamba tunathamini zawadi bora ya uhai.
-
-
Thamini Zawadi ya UhaiFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
5. Heshimu uhai wa mtoto ambaye hajazaliwa
Daudi alifafanua jinsi Yehova anavyopendezwa na ukuzi wa mtoto katika tumbo la mama yake. Soma Zaburi 139:13-17, kisha mzungumzie swali hili:
Kulingana na maoni ya Yehova, je, uhai wa mtu huanza mimba inapotungwa au mtoto anapozaliwa?
Sheria ambazo Yehova aliwapa Waisraeli wa kale ziliwalinda akina mama na watoto wao ambao hawajazaliwa. Soma Kutoka 21:22, 23, kisha mzungumzie maswali haya:
Yehova alimwonaje mtu aliyesababisha bila kukusudia kifo cha mtoto ambaye hajazaliwa?
Yehova atahisije ikiwa mtu atafanya hivyo kimakusudi?b
Unaonaje maoni ya Mungu kuhusu jambo hilo?
Hata mwanamke anayethamini uhai huenda akahisi kwamba hali zinamlazimu kutoa mimba. Soma Isaya 41:10, kisha mzungumzie maswali haya:
Ikiwa mwanamke anakabili mkazo wa kutoa mimba anapaswa kutafuta msaada kwa nani? Kwa nini?
-
-
Thamini Zawadi ya UhaiFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
b Wale ambao wamewahi kutoa mimba hawapaswi kulemewa na hisia za hatia, Yehova anaweza kuwasamehe. Ili kupata habari zaidi, soma makala “Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa Mimba?” iliyo kwenye sehemu ya Chunguza Zaidi katika somo hili.
-