Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 16:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usiangalie sura yake wala urefu+ wa umbo lake, kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona,+ kwa maana mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho,+ lakini Yehova huona jinsi moyo+ ulivyo.”

  • 1 Wafalme 8:39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 basi na usikie ukiwa mbinguni,+ makao yako yaliyofanywa imara,+ nawe usamehe+ na kutenda+ na kumpa kila mmoja kulingana na njia zake zote,+ kwa sababu unaujua moyo wake+ (kwa maana ni wewe peke yako unayejua vema moyo wa wanadamu wote);+

  • 1 Mambo ya Nyakati 28:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 “Nawe, Sulemani mwanangu, mjue+ Mungu wa baba yako, umtumikie+ kwa moyo kamili+ na kwa nafsi yenye shangwe;+ kwa maana Yehova anaichunguza mioyo yote,+ naye anatambua kila mwelekeo wa fikira.+ Ukimtafuta, ataacha umpate;+ lakini ukimwacha,+ atakutupa mbali milele.+

  • Zaburi 17:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Umeuchunguza moyo wangu, umefanya ukaguzi wakati wa usiku,+

      Umenisafisha; utagundua kwamba sijapanga hila.+

      Kinywa changu hakitafanya kosa.+

  • Zaburi 44:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Je, Mungu mwenyewe hatachunguza hilo?+

      Kwa maana yeye anajua siri za moyo.+

  • Zaburi 139:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+

      Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha,+

  • Yeremia 12:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nawe, Ee Yehova, unanijua mimi vema;+ unaniona, nawe umeuchunguza moyo wangu katika muungano na wewe.+ Waweke peke yao kama kondoo wa kuchinjwa,+ na kuwatenga kwa ajili ya siku ya kuuawa.

  • Yeremia 20:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Lakini wewe, Ee Yehova wa majeshi, unamchunguza mwadilifu;+ unaziona figo na moyo.+ Na nione kisasi chako juu yao,+ kwa maana nimekufunulia wewe kesi yangu.+

  • Waebrania 4:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Na hakuna kiumbe kisichokuwa wazi machoni pake,+ bali vitu vyote viko uchi navyo vimefunuliwa wazi machoni pake yeye ambaye tunatoa hesabu kwake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki