1 Samweli
16 Mwishowe Yehova akamwambia Samweli: “Ni mpaka wakati gani utamwombolezea Sauli,+ huku mimi, kwa upande mwingine, nimemkataa asitawale akiwa mfalme juu ya Israeli?+ Jaza pembe yako mafuta,+ nawe uende. Nitakutuma kwa Yese+ Mbethlehemu, kwa maana nimejipatia mfalme kati ya wanawe.”+ 2 Lakini Samweli akasema: “Nawezaje kwenda? Mara Sauli atakaposikia habari hizo, ataniua hakika.”+ Na Yehova akaendelea kusema: “Chukua ng’ombe mchanga wa mifugo pamoja nawe, nawe useme, ‘Nimekuja kumtolea Yehova dhabihu.’+ 3 Na umwite Yese aje kwenye dhabihu; nami, kwa upande wangu, nitakujulisha unalopaswa kufanya,+ nawe unitilie mafuta+ yule nitakayekuonyesha.”
4 Na Samweli akafanya yale ambayo Yehova alisema. Alipokuja Bethlehemu,+ wanaume wazee wa jiji wakaanza kutetemeka+ walipokutana naye, nao wakasema: “Je, kuja kwako kunamaanisha amani?”+ 5 Naye akasema: “Kunamaanisha amani. Nimekuja kumtolea Yehova dhabihu. Jitakaseni,+ nanyi mje pamoja nami kwenye dhabihu.” Ndipo akamtakasa Yese na wanawe, kisha akawaita waje kwenye dhabihu. 6 Na ikawa kwamba walipokuwa wakiingia naye akamwona Eliabu,+ mara moja akasema: “Hakika mtiwa-mafuta wake yuko mbele za Yehova.” 7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usiangalie sura yake wala urefu+ wa umbo lake, kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona,+ kwa maana mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho,+ lakini Yehova huona jinsi moyo+ ulivyo.” 8 Ndipo Yese akamwita Abinadabu,+ akampitisha mbele ya Samweli, lakini akasema: “Yehova hakumchagua huyu pia.” 9 Kisha Yese akampitisha Shamma,+ lakini akasema: “Yehova hakumchagua huyu pia.” 10 Basi Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli; na bado Samweli akamwambia Yese: “Yehova hakuwachagua hawa.”
11 Mwishowe Samweli akamwambia Yese: “Je, hawa ndio wavulana wote?” Naye akasema: “Aliye mdogo zaidi ameachwa mpaka sasa,+ na tazama! analisha kondoo.”+ Kwa hiyo Samweli akamwambia Yese: “Tuma watu, wamlete, kwa sababu hatutaketi kula chakula mpaka atakapokuja hapa.” 12 Basi akatuma watu, naye akaletwa. Naye alikuwa mwekundu,+ kijana mwenye macho yenye kupendeza na mwenye sura nzuri. Ndipo Yehova akasema: “Simama, mtie mafuta, kwa maana huyu ndiye!”+ 13 Basi Samweli akachukua ile pembe ya mafuta,+ akamtia mafuta katikati ya ndugu zake. Na roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu ya Daudi kuanzia siku hiyo na kuendelea.+ Baadaye Samweli akasimama, akaenda zake mpaka Rama.+
14 Na roho ya Yehova ikaondoka+ juu ya Sauli, nayo roho mbaya+ kutoka kwa Yehova ikamtia hofu. 15 Na watumishi wa Sauli wakaanza kumwambia: “Tazama, roho mbaya ya Mungu inakutia hofu. 16 Tafadhali basi, bwana wetu na aamuru watumishi wako walio mbele yako kwamba watafute mtu mwenye ustadi,+ anayepiga kinubi.+ Na itatukia kwamba wakati roho mbaya ya Mungu inapokuja juu yako, yeye atakipiga kwa mkono wake, na mambo yatakuendea vema.” 17 Basi Sauli akawaambia watumishi wake: “Tafadhali, nipeni mtu anayejua kukipiga vema, kisha mkamlete kwangu.”+
18 Na mmoja wa watumishi akajibu na kusema: “Tazama! Nimeona jinsi mwana fulani wa Yese Mbethlehemu alivyo mwenye ustadi wa kukipiga,+ naye ni shujaa,+ mwanamume mwenye nguvu,+ na mwanamume wa vita na msemaji mwenye akili+ na mwanamume mwenye umbo zuri,+ na Yehova yupo pamoja naye.”+ 19 Kwa hiyo Sauli akatuma wajumbe kwa Yese na kusema: “Mtume kwangu Daudi mwana wako, aliye pamoja na kundi.”+ 20 Basi Yese akachukua punda, mkate na kiriba cha ngozi+ cha divai na mwana-mbuzi, na kuvituma kwa Sauli kwa mkono wa Daudi mwana wake.+ 21 Kwa hiyo Daudi akamjia Sauli na kumtumikia;+ naye akampenda sana, kisha akawa mchukua-silaha wake.+ 22 Basi Sauli akatuma watu kwa Yese, akisema: “Tafadhali, acha Daudi aendelee kunitumikia, kwa kuwa amepata kibali machoni pangu.” 23 Na ikatukia kwamba wakati roho ya Mungu ilipokuja juu ya Sauli, Daudi alichukua kinubi na kukipiga kwa mkono wake; ndipo Sauli akapata faraja na mambo yakamwendea vema, na ile roho mbaya ikaondoka juu yake.+