Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 23:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana yeye anajua vema ile njia ninayoenda.+

      Baada ya yeye kunijaribu, nitatoka nikiwa kama dhahabu.+

  • Zaburi 26:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Unichunguze, Ee Yehova, na kunijaribu;+

      Usafishe figo zangu na moyo wangu.+

  • Zaburi 66:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana umetuchunguza, Ee Mungu;+

      Umetusafisha kama kusafisha fedha.+

  • Yeremia 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, ninawayeyusha, nami lazima niwachunguze,+ kwa sababu nitatendaje vinginevyo kwa ajili ya binti ya watu wangu?+

  • Zekaria 13:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Nami nitaleta sehemu hiyo ya tatu kupitia moto;+ nami nitawasafisha kama vile fedha inavyosafishwa,+ na kuwajaribu kama vile dhahabu inavyojaribiwa.+ Nayo italiitia jina langu, nami nitaijibu.+ Nitasema, ‘Ni watu wangu,’+ nayo itasema, ‘Yehova ni Mungu wangu.’ ”+

  • Malaki 3:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Naye ataketi kama msafishaji na mtakasaji wa fedha+ naye atawatakasa wana wa Lawi;+ naye atawasafisha kama dhahabu+ na kama fedha, nao watakuwa kwa Yehova watu wanaotoa toleo la zawadi+ katika uadilifu.

  • 1 Petro 1:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 ili sifa iliyojaribiwa ya imani+ yenu, iliyo na thamani kubwa zaidi kuliko dhahabu ambayo huharibika ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto,+ ipatikane kuwa sababu ya sifa na utukufu na heshima wakati wa ufunuo+ wa Yesu Kristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki