Ayubu
23 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Hata leo hangaiko+ langu ni uasi;
Mkono wangu wenyewe ni mzito kwa sababu ya kuugua kwangu.
4 Ningeleta mbele zake kesi ya hukumu,
Nami ningekijaza kinywa changu na hoja za kujibu;
5 Ningeyajua maneno anayonijibu,
Nami ningefikiria yale anayoniambia.+
7 Hapo mtu mnyoofu mwenyewe atanyoosha mambo pamoja na yeye,
Nami ningeenda nikiwa salama milele kutoka kwa mwamuzi wangu.
9 Kuelekea upande wa kushoto ambako anafanya kazi, lakini siwezi kumwona;
Anageuka kando upande wa kuume, lakini simwoni.
10 Kwa maana yeye anajua vema ile njia ninayoenda.+
Baada ya yeye kunijaribu, nitatoka nikiwa kama dhahabu.+
12 Siondoki katika amri ya midomo yake.+
Nimeyachukua kuwa hazina maneno ya kinywa chake+ kuliko yale niliyoamriwa.
13 Naye ana akili moja, na ni nani anayeweza kumpinga?+
Na nafsi yake mwenyewe ina tamaa, naye ataifanya.+
17 Kwa maana sikunyamazishwa kimya kwa sababu ya giza,
Wala kwa sababu weusi umeufunika uso wangu.