Ayubu
22 Naye Elifazi Mtemani akajibu, akasema:
2 “Je, mwanamume anaweza kuwa na faida kwa Mungu mwenyewe,+
Kwamba mtu mwenye ufahamu awe na faida kwake?
3 Je, Mweza-Yote anapendezwa kwa vyovyote kwa kuwa wewe ni mwadilifu,+
Au, kupata faida yoyote kwa kuwa wewe unafanya njia yako isiwe na lawama?+
6 Kwa maana wewe unanyakua rehani kutoka kwa ndugu zako bila sababu,+
Nawe unavua hata mavazi ya watu walio uchi.
10 Ndiyo sababu mitego ya ndege imekuzunguka pande zote,+
Na hofu ya ghafula inakutia wasiwasi;
11 Au giza, hivi kwamba huwezi kuona,
Na mkusanyo wa maji yanayosukasuka unakufunika.
13 Na bado umesema: ‘Kweli Mungu anajua nini?
Je, anaweza kuhukumu kupitia giza zito?
14 Mawingu ni mahali pake pa kujificha hivi kwamba haoni,
Naye hutembea huku na huku juu ya ngome ya mbingu.’
15 Je, utaendelea kuifuata njia ya zamani za kale
Ambayo watu wenye kudhuru wametembea,
16 Watu ambao wamenyakuliwa kabla ya wakati wao,+
Ambao msingi+ wao unamwagwa kama mto,
17 Ambao wanamwambia Mungu wa kweli: ‘Tuondokee!+
Na Mweza-Yote anaweza kutimiza nini juu yetu?’
20 ‘Kwa kweli wapinzani wetu wamefutiliwa mbali;
Na mabaki yao hakika moto utayateketeza.’
21 Tafadhali, fahamiana naye, na udumishe amani;
Hivyo mambo mema yatakujia.
23 Ukirudi kwa Mweza-Yote,+ utajengwa;
Ukiweka ukosefu wa uadilifu mbali na hema lako,
24 Na mawe ya madini yenye thamani yakiwekwa katika mavumbi
Na dhahabu ya Ofiri+ katika mwamba wa mabonde ya mito,
25 Pia Mweza-Yote kwelikweli atakuwa madini yako yenye thamani,
Na fedha, iliyo bora kabisa, kwako.+
26 Kwa maana ndipo utakapopata furaha tele katika Mweza-Yote,+
Nawe utamwinulia Mungu mwenyewe uso wako.+
28 Nawe utafanya uamuzi kuhusu jambo fulani, nalo litasimama kwako;
Na hakika nuru itaziangaza njia zako.+