116 Ninajawa na upendo, kwa sababu Yehova husikia+
Sauti yangu, kusihi kwangu.+
2 Kwa maana yeye amenitegea sikio lake,+
Nami nitaita siku zangu zote.+
3 Kamba za kifo zilinizunguka+
Na hali zenye kutaabisha za Kaburi zikanipata.+
Nikaendelea kupata taabu na huzuni.+
4 Lakini nikaliitia jina la Yehova:+
“Ah, Yehova, uiokoe nafsi yangu!”+
5 Yehova ni mwenye neema na ni mwadilifu;+
Naye Mungu wetu, Yeye ni mwenye kuonyesha rehema.+
6 Yehova anawalinda wasio na uzoefu.+
Nilikuwa maskini, naye akaniokoa.+
7 Rudi mahali pako pa kupumzika, Ee nafsi yangu,+
Kwa maana Yehova mwenyewe amekutendea inavyofaa.+
8 Kwa maana umeiokoa nafsi yangu kutokana na kifo,+
Jicho langu kutokana na machozi, mguu wangu kutokana na kujikwaa.+
9 Nitatembea+ mbele za Yehova katika nchi za walio hai.+
10 Nilikuwa na imani,+ kwa maana nilisema.+
Mimi mwenyewe nilikuwa nimeteseka sana.
11 Mimi mwenyewe nilisema, wakati nilipokuwa na wasiwasi mkubwa:+
“Kila mwanadamu ni mwongo.”+
12 Nitamlipa Yehova nini+
Kwa ajili ya faida zake zote kwangu?+
13 Nitakichukua kikombe cha wokovu mkuu,+
Nami nitaliitia jina la Yehova.+
14 Nadhiri zangu nitamtimizia Yehova,+
Naam, mbele ya watu wake wote.
15 Ni chenye thamani machoni pa Yehova
Kifo cha washikamanifu wake.+
16 Ah, sasa, Ee Yehova,+
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+
Mimi ni mtumishi wako, mwana wa kijakazi wako.+
Umezifungua pingu zangu.+
17 Nitakutolea wewe dhabihu ya kutoa shukrani,+
Nami nitaliitia jina la Yehova.+
18 Nadhiri zangu nitamtimizia Yehova,+
Naam, mbele ya watu wake wote,+
19 Katika nyua za nyumba ya Yehova,+
Katikati yako, Ee Yerusalemu.+
Msifuni Yah!+