Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 34:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na Yehova akapita karibu mbele ya uso wake na kutangaza: “Yehova, Yehova, Mungu mwenye rehema+ na neema,+ si mwepesi wa hasira+ naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo+ na kweli,+

  • Kumbukumbu la Torati 32:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Yeye Mwamba, kazi zake ni kamilifu,+

      Kwa maana njia zake zote ni haki.+

      Mungu wa uaminifu,+ ambaye hana ukosefu wowote wa haki;+

      Yeye ni mwadilifu na mnyoofu.+

  • Nehemia 9:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Nawe ukaona moyo wake kuwa ni mwaminifu mbele zako;+ basi ukafanya lile agano+ pamoja na yeye ili umpe nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori na Waperizi na Wayebusi na Wagirgashi, kuupa uzao wake;+ nawe ukatimiza maneno yako, kwa maana wewe ni mwadilifu.+

  • Zaburi 103:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema,+

      Si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.+

  • Zaburi 119:137
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 137 Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+

      Nayo maamuzi yako ya hukumu ni manyoofu.+

  • Zaburi 145:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Yehova ni mwadilifu katika njia zake zote+

      Na mshikamanifu katika kazi zake zote.+

  • Waroma 3:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Mungu alimweka kuwa toleo la kupatanisha+ kupitia imani katika damu+ yake. Ilikuwa hivyo ili kuonyesha wazi uadilifu wake mwenyewe, kwa sababu alikuwa akizisamehe dhambi+ zilizotokea wakati uliopita wakati Mungu alipokuwa akivumilia kwa subira;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki