Kumbukumbu la Torati
2 Mafundisho yangu yatatiririka kama mvua,+
Maneno yangu yatadondoka kama umande,+
Kama mvua ya rasharasha juu ya majani+
Na kama manyunyu mengi juu ya mimea+
4 Yeye Mwamba, kazi zake ni kamilifu,+
Kwa maana njia zake zote ni haki.+
Mungu wa uaminifu,+ ambaye hana ukosefu wowote wa haki;+
Yeye ni mwadilifu na mnyoofu.+
6 Je, Yehova ndiye mnayeendelea kumfanyia hivi,+
Enyi watu wajinga na ambao hawana hekima?+
Je, yeye si Baba yenu aliyewazaa,+
Yeye aliyewafanyiza ninyi na kuwaimarisha?+
Fikirieni miaka iliyopita kutoka kizazi mpaka kizazi;
Muulize baba yako, naye anaweza kukuambia;+
Wanaume wenu wazee, nao wanaweza kukuambia.+
8 Wakati Aliye Juu Zaidi alipoyapa mataifa urithi,+
Alipowatenganisha wana wa Adamu,+
Ndipo alipoweka mpaka wa vikundi vya watu+
Kuhusiana na hesabu ya wana wa Israeli.+
10 Alimpata katika nchi ya nyika,+
Na katika jangwa tupu, lenye kulia.+
Alianza kumzunguka,+ kumtunza,+
Kumlinda kama mboni ya jicho lake.+
11 Kama vile tai anavyokitikisa kiota chake,
Anavyoelea angani juu ya watoto wake,+
Anavyotandaza mabawa yake, na kuwachukua,
Anavyowachukua kwenye manyoya yake,+
12 Ndivyo Yehova peke yake alivyoendelea kumwongoza,+
Na hapakuwa na mungu yeyote wa kigeni pamoja naye.+
13 Aliendelea kumfanya apande juu ya mahali pa juu pa dunia,+
Hivi kwamba akala mazao ya shamba.+
Naye akaendelea kumfanya anyonye asali kutoka katika mwamba,+
Na mafuta kutoka katika jiwe gumu;+
14 Siagi ya mifugo na maziwa ya kundi+
Pamoja na mafuta ya kondoo-dume,
Na kondoo-dume, uzao wa Bashani, na mbuzi-dume+
Pamoja na mafuta ya figo ya ngano;+
Nawe uliendelea kunywa kama divai damu ya zabibu.+
15 Yeshuruni+ alipoanza kunenepa, ndipo akapiga teke.+
Umepata mafuta, umekuwa mnene, umeshiba mno.+
Basi akamwacha Mungu, aliyemfanya,+
Na kumdharau Mwamba+ wa wokovu wake.
16 Walianza kumchochea awe na wivu+ kwa miungu migeni;+
Kwa mambo yenye kuchukiza waliendelea kumtia uchungu.+
17 Waliwatolea dhabihu roho waovu, wala si Mungu,+
Miungu ambayo hawakuijua,+
Mipya iliyokuja hivi karibuni,+
Ambayo mababu zenu hawakuifahamu.
18 Mwamba aliyekuzaa wewe, ulimsahau,+
Nawe ukaanza kumwondoa Mungu katika kumbukumbu, yule anayekutokeza kwa uchungu wa kuzaa.+
19 Yehova alipoona hilo, ndipo akawadharau wao,+
Kwa sababu ya usumbufu uliosababishwa na wanawe na binti zake.
20 Kwa hiyo akasema, ‘Acha niufiche uso wangu kutoka kwao,+
Acha nione mwisho wao utakuwaje baadaye.
Kwa maana wao ni kizazi chenye upotovu,+
Wana ambao ndani yao hamna uaminifu.+
21 Wao wamenichochea niwe na wivu kwa kile ambacho si mungu;+
Wameniudhi kwa sanamu zao za ubatili;+
Na mimi, nitawachochea wawe na wivu kwa kile ambacho si kikundi cha watu;+
Kwa taifa jinga nitawatia uchungu.+
22 Kwa maana moto umewashwa katika hasira yangu+
Nao utateketeza mpaka katika Kaburi,* mahali pa chini zaidi,+
Nao utateketeza dunia na mazao yake+
Nao utawasha misingi ya milima.+
24 Watachoka kutokana na njaa+ na kuliwa na homa kali+
Na maangamizi machungu.+
Na meno ya wanyama nitatuma juu yao,+
Kwa sumu ya watambaazi wa mavumbini.+
25 Nje upanga utawasababishia vifo,+
Na ndani woga,+
Wa kijana na bikira,+
Anayenyonya pamoja na mwanamume mwenye mvi.+
26 Ningalikuwa nimesema: “Nitawatawanya,+
Nitalifanya jina lao likome kutoka katikati ya watu wanaoweza kufa,”+
27 Isingalikuwa kwa sababu niliogopa usumbufu kutoka kwa adui,+
Kwamba wapinzani wao wangaliweza kuelewa vibaya,+
Ili waseme: “Mkono wetu umeshinda,+
Na si Yehova aliyefanya mambo haya yote.”+
29 Laiti wangalikuwa wenye hekima!+ Ndipo wangalifikiria hili kwa uzito.+
Wangaliufikiria mwisho wao baadaye.+
Haingewezekana isipokuwa Mwamba wao awe amewauza+
Na Yehova awe amewatoa.
Zabibu zao ni zabibu za sumu,
Vishada vyao ni vichungu.+
35 Kisasi ni changu, na malipo.+
Katika wakati uliowekwa mguu wao utasogea kwa kuyumba-yumba,+
Kwa maana siku ya maafa yao iko karibu,+
Na matukio yanafanya haraka kujitayarisha kwa ajili yao.’+
36 Kwa maana Yehova atawahukumu watu wake+
Naye atajuta juu ya watumishi wake,+
Kwa sababu ataona kwamba tegemeo limetoweka
Na aliyeko tu ni mtu asiye na uwezo na asiye na thamani.
38 Iliyokuwa ikila mafuta ya dhabihu zao,+
Ili kunywa divai ya matoleo yao ya kinywaji?+
Na isimame na kuwasaidia ninyi.+
Na iwe mahali pa maficho kwa ajili yenu.+
39 Oneni sasa kwamba mimi—mimi ndiye+
Na hakuna miungu pamoja nami.+
Mimi huua, nami hufanya hai.+
Nimejeruhi vikali,+ na mimi—mimi nitaponya,+
Na hakuna anayenyakua kutoka mkononi mwangu.+
40 Kwa maana mimi nainua mkono wangu kuelekea mbinguni kwa kiapo,+
Nami ninasema: “Kama nilivyo hai mpaka wakati usio na
kipimo,”+
41 Kwa kweli nikiunoa upanga wangu unaometameta,+
Na mkono wangu ushike hukumu,+
Nitawalipa kisasi wapinzani wangu+
Na kutoa malipo kwa wale wanaonichukia vikali.+
42 Nitailewesha mishale yangu kwa damu,+
Nao upanga wangu utakula nyama,+
Kwa damu ya waliouawa na mateka,
Kwa vichwa vya viongozi wa adui.’+
43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,+
Kwa maana atalipiza kisasi damu ya watumishi wake,+
Naye atawalipa kisasi adui zake+
Naye kwa kweli atafanya upatanisho kwa ajili ya nchi ya watu wake.”
44 Basi Musa akaja na kusema maneno yote ya wimbo huu masikioni mwa watu,+ yeye na Hoshea mwana wa Nuni.+ 45 Baada ya Musa kumaliza kuwaambia Israeli wote maneno yote hayo, 46 ndipo akawaambia: “Tieni mioyo yenu katika maneno yote ninayosema kwa kuwaonya ninyi leo,+ ili muwaamuru wana wenu wawe waangalifu kufanya maneno yote ya sheria hii.+ 47 Kwa maana hilo si neno lisilo na thamani kwenu,+ bali linamaanisha uhai wenu,+ na kwa neno hili mnaweza kurefusha siku zenu juu ya udongo ambao mnavuka Yordani ili kuumiliki.”+
48 Na Yehova akasema na Musa siku hiyohiyo, na kumwambia: 49 “Panda juu ya mlima huu wa Abarimu,+ Mlima Nebo,+ ulio katika nchi ya Moabu, mbele ya Yeriko, nawe uione nchi ya Kanaani, ninayowapa wana wa Israeli waimiliki.+ 50 Kisha ufe katika mlima utakaopanda, na kukusanywa kwa watu wako,+ kama vile Haruni ndugu yako alivyokufa katika Mlima Hori+ na kukusanywa kwa watu wake; 51 Kwa sababu ninyi mlitenda isivyofaa kunielekea mimi+ katikati ya wana wa Israeli kwenye maji ya Meriba+ ya Kadeshi katika nyika ya Zini; kwa sababu ninyi hamkunitakasa mimi katikati ya wana wa Israeli.+ 52 Kwa maana kutoka mbali utaiona nchi, lakini hutaingia katika nchi ninayowapa wana wa Israeli.”+