10 “Na hesabu ya wana wa Israeli itakuwa kama chembe za mchanga wa bahari ambao hauwezi kupimwa wala kuhesabiwa.+ Na itakuwa kwamba mahali ambapo walikuwa wakiambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’+ wataambiwa, ‘Wana wa Mungu aliye hai.’+
23 Nami hakika nitampanda yeye duniani kama mbegu kwa ajili yangu,+ nami nitamwonyesha rehema yeye ambaye hakuonyeshwa rehema,+ nami nitawaambia wale ambao si watu wangu: “Ninyi ni watu wangu”;+ wao nao watasema: “Wewe ni Mungu wangu.” ’ ”+
11 Kwa hiyo nauliza, Je, walijikwaa hivi kwamba wakaanguka+ kabisa? Hilo lisitendeke kamwe! Lakini kwa kujikwaa+ kwao kuna wokovu kwa watu wa mataifa,+ kuwachochea wao kuwa na wivu.+
10 Kwa kuwa wakati mmoja ninyi mlikuwa si watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu;+ mlikuwa wale ambao hawakuwa wameonyeshwa rehema, lakini sasa ninyi ni wale ambao wameonyeshwa rehema.+