Kumbukumbu la Torati
33 Sasa hii ndiyo baraka+ ambayo Musa mtu wa Mungu wa kweli+ aliwabariki nayo wana wa Israeli kabla ya kifo chake. 2 Naye akasema:
“Yehova—alikuja kutoka Sinai,+
Naye akamulika juu yao kutoka Seiri.+
Aliangaza kutoka katika eneo lenye milima la Parani,+
Naye alikuwa pamoja na makumi ya maelfu ya watakatifu,+
Mashujaa wao kwenye mkono wake wa kuume.+
3 Pia alikuwa akiwatunza kwa upendo watu wake;+
Watakatifu wao wote wako mkononi mwako.+
Na wao—wao waliegama miguuni pako;+
Walianza kupokea baadhi ya maneno yako.+
5 Naye akawa mfalme katika Yeshuruni,+
Wakati ambapo walio vichwa vya watu walikusanyika pamoja,+
Hesabu kamili ya makabila ya Israeli.+
7 Nayo hii ndiyo iliyokuwa baraka ya Yuda,+ alipoendelea kusema:
“Usikie, Ee Yehova, sauti ya Yuda,+
Nawe umlete kwa watu wake.
Mikono yake imeshindania kilicho chake;
Nawe uwe msaidizi juu ya wapinzani wake.”+
“Thumimu yako na Urimu+ yako ni vyake mtu aliye mshikamanifu kwako,+
Uliyemjaribu huko Masa.+
Ulianza kushindana naye kando ya maji ya Meriba,+
9 Mtu aliyemwambia baba yake na mama yake, ‘Mimi sijamwona.’
Hata ndugu zake hakuwatambua,+
Na wanawe hakuwajua.
Kwa maana walilishika neno lako,+
Na agano lako waliendelea kulishika.+
10 Na wamfundishe Yakobo hukumu zako+
Na Israeli sheria yako.+
Na watoe uvumba mbele za mianzi ya pua yako+
Na toleo zima kwenye madhabahu yako.+
11 Bariki, Ee Yehova, nguvu zake,+
Na ufurahie utendaji wa mikono yake.+
Waumize vikali viunoni mwao wale wanaoinuka juu yake,+
Na wale wanaomchukia vikali, ili wasiinuke.”+
“Mpendwa+ wa Yehova na akae katika usalama kando yake,+
Anapomkinga siku nzima,+
Naye lazima akae katikati ya mabega yake.”+
“Nchi yake na ibarikiwe daima na Yehova+
Kwa vitu bora vya mbinguni, kwa umande,+
Na kwa kilindi cha maji kilicho chini,+
14 Na kwa vitu bora, mazao ya jua,+
Na kwa vitu bora, mazao ya mwezi.+
15 Na kwa vilivyo bora kabisa kutoka katika milima ya mashariki,+
Na kwa vitu bora vya vilima vyenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo,
16 Na kwa vitu bora vya dunia na vitu vinavyoijaza,+
Na kwa kibali cha Yule anayekaa katika kichaka cha miiba.+
Na vije juu ya kichwa cha Yosefu+
Na juu ya utosi wa kichwa cha yule aliyechaguliwa kutoka kati ya ndugu zake.+
17 Kama mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe-dume ndivyo fahari yake ilivyo,+
Na pembe zake ni pembe za ng’ombe-dume wa mwituni.+
Atasukuma vikundi vya watu kwa pembe hizo+
Wote pamoja mpaka miisho ya dunia,
Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,+
Nao ni maelfu ya Manase.”
19 Wataita vikundi vya watu mlimani.
Huko watatoa dhabihu za uadilifu.+
Kwa maana watanyonya mali nyingi ya bahari+
Na akiba zilizofichika za mchanga.”
“Amebarikiwa yule anayepanua mipaka ya Gadi.+
Yeye atakaa kama simba,+
Naye atararua mkono, naam, utosi wa kichwa.+
21 Naye atajichagulia sehemu ya kwanza,+
Kwa maana huko fungu la mpaji-sheria linahifadhiwa.+
Na walio vichwa vya watu watajikusanya pamoja.
Hakika atautimiza uadilifu wa Yehova
Na maamuzi yake ya hukumu pamoja na Israeli.”
“Aliyebarikiwa na wana ni Asheri.+
Na awe aliyekubaliwa na ndugu zake,+
Na yule anayechovya mguu wake katika mafuta.+
25 Chuma na shaba ni makufuli ya lango lako,+
Na kulingana na siku zako ndivyo yalivyo matembezi yako ya starehe.
26 Hakuna aliye kama Mungu wa kweli+ wa Yeshuruni,+
Anayepanda juu ya mbingu ili kukusaidia+
Na juu ya anga zenye kutanda mawingu katika adhama yake.+
27 Mungu wa nyakati za kale ni mahali pa kujificha,+
Na chini kuna mikono yenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo.+
Naye atawafukuzia mbali adui zako toka mbele yako,+
Naye atasema, ‘Waangamize!’+