18 Kwa habari ya wana wa Rubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase; kati ya wale waliokuwa watu mashujaa,+ wanaume wanaochukua ngao na upanga na kupinda upinde na kuzoezwa katika vita, kulikuwa na 44,760 wanaoingia jeshini.+
20 Nao wakaja kusaidiwa kupigana nao, hivi kwamba Wahagri na wale wote waliokuwa pamoja nao wakatiwa mkononi mwao, kwa maana walikuwa wameomba msaada+ kutoka kwa Mungu katika vita, naye akakubali kusihiwa awape kibali kwa sababu walimtegemea.+