Kumbukumbu la Torati
34 Kisha Musa akatoka katika nchi tambarare za jangwa la Moabu na kuingia katika Mlima Nebo,+ mpaka juu ya Pisga,+ mbele ya Yeriko.+ Naye Yehova akamwonyesha nchi yote, Gileadi mpaka Dani,+ 2 na Naftali yote na nchi ya Efraimu na Manase na nchi yote ya Yuda mpaka bahari ya magharibi,+ 3 na Negebu+ na Wilaya,+ nchi tambarare ya bonde la Yeriko, jiji la mitende,+ mpaka Soari.+
4 Na Yehova akamwambia: “Hii ndiyo nchi ambayo nilimwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, na kusema, ‘Nitaupa uzao wako.’+ Nimekufanya uione kwa macho yako mwenyewe, kwa maana wewe hutavuka kuingia huko.”+
5 Baada ya hilo Musa mtumishi wa Yehova+ akafa huko katika nchi ya Moabu kulingana na agizo la Yehova.+ 6 Naye akamzika katika bonde katika nchi ya Moabu mbele ya Beth-peori,+ na hakuna mtu ambaye amepata kujua kaburi lake mpaka leo hii.+ 7 Naye Musa alikuwa na umri wa miaka 120 wakati wa kifo chake.+ Jicho lake halikuwa limeingia giza,+ na nguvu zake hazikuwa zimepotea.+ 8 Na wana wa Israeli wakamlilia Musa kwenye nchi tambarare za jangwa la Moabu kwa siku 30.+ Mwishowe siku za kulia za kipindi cha kumwombolezea Musa zikamalizika.
9 Na Yoshua mwana wa Nuni alikuwa amejaa roho ya hekima,+ kwa kuwa Musa alikuwa ameweka mkono wake juu yake;+ na wana wa Israeli wakaanza kumsikiliza nao wakafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.+ 10 Lakini hajainuka kamwe nabii katika Israeli aliye kama Musa,+ ambaye Yehova alimjua uso kwa uso,+ 11 kuhusiana na ishara zote na miujiza yote ambayo Yehova alimtuma afanye katika nchi ya Misri kwa Farao na watumishi wake wote na nchi yake yote,+ 12 na kuhusiana na mkono wote wenye nguvu na hofu kuu yote ambayo Musa alifanya ionekane mbele ya macho ya Israeli wote.+