7 Na ikawa kwamba mara tu mfalme wa Israeli aliposoma ile barua, mara moja akayararua+ mavazi yake na kusema: “Je, mimi ni Mungu,+ ili kuua au kuhifadhi hai?+ Kwa maana mtu huyu anatuma mtu kwangu ili nimponye ukoma wake; kwa maana angalieni, tafadhali, mwone jinsi anavyotafuta ugomvi nami.”+