Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki, wimbo.
68 Mungu na asimame,+ adui zake na watawanyike,+
Na wale wanaomchukia vikali na wakimbie kwa sababu yake.+
2 Kama vile moshi unavyofukuziwa mbali, na uwafukuzie mbali vivyo hivyo;+
Kama vile nta inavyoyeyuka kwa sababu ya moto,+
Waovu na waangamie vivyo hivyo kutoka mbele za Mungu.+
4 Mwimbieni Mungu, lipigieni jina lake muziki;+
Mwimbieni wimbo Yeye anayepanda akipitia nchi tambarare za jangwani+
Akiwa Yah, ambalo ndilo jina lake;+ na kushangilia mbele zake;
6 Mungu anawafanya wapweke wakae katika nyumba;+
Anawafanikisha kabisa wafungwa.+
Hata hivyo, walio wakaidi, lazima wakae katika nchi iliyokauka.+
7 Ee Mungu, ulipoenda mbele ya watu wako,+
Ulipopiga mwendo jangwani+—Sela—
Nayo mbingu pia ikadondoka maji kwa sababu ya Mungu;+
Mlima huu Sinai ukatikisika kwa sababu ya Mungu,+ Mungu wa Israeli.+
9 Ulisababisha mvua kubwa ianze kunyesha, Ee Mungu;+
Urithi wako, hata wakati ulipokuwa umechoka—wewe mwenyewe uliupatia nguvu tena.+
10 Kambi yako ya mahema+—wamekaa ndani yake;+
Kwa wema wako uliitayarisha kwa ajili ya mwenye kuteseka, Ee Mungu.+
12 Hata wafalme wa majeshi wanakimbia, naam, wanakimbia.+
Lakini mwanamke anayekaa nyumbani, hugawa nyara.+
13 Ijapokuwa ninyi mliendelea kulala katikati ya marundo ya majivu ya kambi,
Kutakuwako mabawa ya njiwa yaliyofunikwa kwa fedha
Na manyoya yake yakiwa yamefunikwa kwa dhahabu ya kijani-manjano.+
14 Wakati Mweza-Yote alipowatawanya kotekote wafalme walio ndani yake,+
Theluji ilianza kuanguka Salmoni.+
15 Eneo lenye milima la Bashani+ ni mlima wa Mungu;+
Eneo lenye milima la Bashani ni mlima wenye vilele.+
16 Kwa nini ninyi, enyi milima yenye vilele, mnaendelea kutazama kwa wivu
Mlima ambao Mungu ametamani kukaa ndani yake?+
Naam, Yehova atakaa humo milele.+
17 Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu zaidi na zaidi.+
Yehova mwenyewe amekuja kutoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+
Umechukua mateka;+
Umechukua zawadi katika namna ya wanadamu,+
Naam, hata walio wakaidi,+ ili kukaa kati yao,+ Ee Yah Mungu.
19 Na abarikiwe Yehova, ambaye hutubebea mzigo wetu kila siku,+
Mungu wa kweli wa wokovu wetu.+ Sela.
20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu wa matendo ya kuokoa;+
Nazo njia za kutoka katika kifo+ ni za Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+
21 Kwa kweli Mungu mwenyewe atavunja vipande-vipande kichwa cha adui zake,+
Utosi wenye nywele wa mtu yeyote anayetembea katika hatia yake.+
23 Ili upate kuosha mguu wako katika damu,+
Ili ulimi wa mbwa zako upate fungu lake kutoka katika adui.”+
24 Wameona maandamano yako, Ee Mungu,+
Maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, kuingia mahali patakatifu.+
25 Waimbaji walitangulia mbele, wapiga-vinanda wakawafuata;+
Katikati yao palikuwa na wanawali wakipiga matari.+
26 Katika makundi yaliyokutanika mbarikini Mungu,+
Yehova, enyi mnaotoka katika Chemchemi ya Israeli.+
27 Tazama Benyamini mdogo akiwatiisha,+
Wakuu wa Yuda pamoja na umati wao unaopaaza sauti,
Wakuu wa Zabuloni, wakuu wa Naftali.+
28 Mungu wako ameweka amri juu ya nguvu zako.+
Uonyeshe nguvu, Ee Mungu, wewe ambaye umechukua hatua kwa ajili yetu.+
30 Umkemee mnyama-mwitu wa matete,+ kusanyiko la ng’ombe-dume,+
Na ndama za vikundi vya watu, kila mmoja akikanyaga-kanyaga vipande vya fedha.+
Ametawanya vikundi vya watu vinavyopenda mapigano.+