36 Toka Aroeri,+ jiji lililo kando ya ukingo wa bonde la mto la Arnoni, na lile jiji lililo katika bonde la mto, mpaka Gileadi, hakukuwa na mji wowote uliokuwa juu sana kwetu.+ Yehova Mungu wetu aliitia yote mkononi mwetu.
22 “Na Yehova Mungu wako atayasukumia mbali mataifa haya toka mbele yako kidogo kidogo.+ Hutaruhusiwa kuwamaliza kabisa upesi, wanyama wa mwituni wasije wakaongezeka dhidi yako.
13 Nendeni, basi, mkajifunze maana ya jambo hili, ‘Ninataka rehema, wala si dhabihu.’+ Kwa maana nilikuja kuwaita, si watu waadilifu, bali watenda-dhambi.”
13 ijapokuwa hapo zamani nilikuwa mkufuru na mtesaji+ na mtu mwenye dharau.+ Hata hivyo, nilionyeshwa rehema,+ kwa sababu nilikosa ujuzi+ nami nilitenda kwa ukosefu wa imani.