17 Na Elisha akaanza kusali+ na kusema: “Ee Yehova, tafadhali fungua macho yake,+ ili aone.” Mara moja Yehova akafungua macho ya yule mtumishi, hivi kwamba akaona; na, tazama! lile eneo lenye milima lilikuwa limejaa farasi na magari ya vita+ ya moto kumzunguka Elisha pande zote.+
10 Kulikuwa na mto wa moto unaotiririka kutoka mbele zake.+ Kulikuwa na maelfu elfu walioendelea kumtumikia,+ na elfu kumi mara elfu kumi walioendelea kusimama mbele zake.+ Ile Mahakama+ ikaketi, na vitabu vikafunguliwa.
11 Nami nikaona, nami nikasikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kile kiti cha ufalme na wale viumbe hai na wale wazee, na hesabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu+ na maelfu ya maelfu,+