Zaburi
Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi.
2 Unisikilize kwa makini na kunijibu.+
Mahangaiko yangu yananisukuma huku na huku bila kuwa na utulivu,+
Sina jambo lingine la kufanya ila kuonyesha wasiwasi.
3 Kwa sababu ya sauti ya adui, kwa sababu ya mkazo wa yule mwovu.+
Kwa maana wanaendelea kuniangushia mambo yenye kuumiza,+
Na kwa hasira wanadumisha uadui juu yangu.+
8 Ningefanya haraka kwenda mahali pangu pa kuponyokea
Kutokana na upepo wenye kuvuma, kutokana na tufani.”+
10 Mchana na usiku wanalizunguka pande zote juu ya kuta zake;+
Na mambo yenye kuumiza na taabu ziko ndani yake.+
11 Shida ziko ndani yake;
Na katika viwanja vyake vya watu wote ukandamizaji na udanganyifu haujaondoka.+
12 Kwa maana sikushutumiwa na adui;+
Kama ndivyo ningaliweza kuvumilia hilo.
Si mtu anayenichukia vikali aliyejivuna sana dhidi yangu;+
Kama ndivyo ningaliweza kujificha kutoka kwake.+
13 Lakini ilikuwa ni wewe, mwanadamu anayeweza kufa tunayelingana,+
Mtu tunayejuana na ambaye ni rafiki yangu,+
14 Kwa sababu tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki ulio mtamu;+
Tulikuwa tukitembea kuingia katika nyumba ya Mungu pamoja na watu wengi.+
Na washuke katika Kaburi* wakiwa hai;+
Kwa maana wakati wao wa kukaa ugenini mambo mabaya yamekuwa ndani yao.+
17 Jioni na asubuhi na katikati ya mchana sikosi kuhangaika nami naomboleza,+
Naye huisikia sauti yangu.+
18 Hakika ataikomboa na kuiweka nafsi yangu katika amani mbali na vita vinavyofanywa juu yangu,+
Kwa maana wakiwa umati wamekuja kuwa dhidi yangu.+
19 Mungu atasikia na kuwajibu,+
Naam, Yeye anayeketi juu ya kiti cha ufalme kama zamani+—Sela—
Wale ambao hawafanyi mabadiliko+
Na ambao hawajamwogopa Mungu.+