Kwa kiongozi wa vinanda. Maskili. Ya Daudi. Wakati Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Je, Daudi hajifichi pamoja nasi?”+
54 Ee Mungu, uniokoe kwa jina lako,+
Nawe unitetee katika kesi yangu kwa uwezo wako.+
2 Ee Mungu, uisikie sala yangu;+
Utege sikio usikie maneno ya kinywa changu.+
3 Kwa maana kuna wageni ambao wameinuka dhidi yangu,
Na waonevu wanaoitafuta nafsi yangu.+
Hawajamweka Mungu mbele yao.+ Sela.
4 Tazama! Mungu ni msaidizi wangu;+
Yehova yuko kati ya wale wanaoitegemeza nafsi yangu.
5 Atawalipa adui zangu ubaya;+
Katika ukweli wako uwanyamazishe.+
6 Nitakutolea dhabihu kwa kupenda.+
Nitalisifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni jema.+
7 Kwa maana alinikomboa kutoka katika kila taabu,+
Nalo jicho langu limewatazama adui zangu.+