Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Vuka Uingie Makedonia”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • SURA YA 16

      “Vuka Uingie Makedonia”

      Baraka zinazotokana na kukubali mgawo na kuvumilia mateso kwa shangwe

      Matendo 16:6-40

      1-3. (a) Roho takatifu iliwaongozaje Paulo na wenzake? (b) Tutachunguza mambo gani?

      KIKUNDI cha wanawake kinaondoka jijini Filipi, huko Makedonia. Baada ya muda mfupi wanawake hao wanafika kwenye mto mdogo unaoitwa Gangites. Kama ilivyo desturi yao, wanaketi kwenye ukingo wa mto huo ili kusali kwa Mungu wa Israeli. Yehova anaona wanalofanya.​—2 Nya. 16:9; Zab. 65:2.

      2 Wakati huohuo, zaidi ya kilomita 800 upande wa mashariki wa Filipi, kikundi cha wanaume kinaondoka katika jiji la Listra, lililo upande wa kusini mwa Galatia. Siku kadhaa baadaye, wanaume hao wanafika kwenye barabara kuu ya Roma inayoelekea upande wa magharibi katika eneo la wilaya ya Asia lenye idadi kubwa zaidi ya watu. Wanaume hao—Paulo, Sila, na Timotheo—wana hamu ya kutembelea Efeso na miji mingine ambayo maelfu ya watu wanahitaji kusikia kumhusu Kristo. Lakini, kabla ya kuondoka, roho takatifu inawazuia kwa njia fulani. Wanazuiwa kuhubiri Asia. Kwa nini? Kwa sababu Yesu anatumia roho ya Mungu kukiongoza kikundi hicho cha Paulo kupitia Asia Ndogo na kuvuka Bahari ya Aegea ili kwenda kwenye kingo za mto huo mdogo unaoitwa Gangites.

      3 Tunaweza kujifunza mambo muhimu kutokana na jinsi Yesu alivyowaongoza Paulo na wenzake katika safari hiyo ya pekee ya kwenda Makedonia. Kwa hiyo, tuchunguze mambo fulani yaliyotukia katika safari hii ya pili ya Paulo ya umishonari, iliyoanza mwaka wa 49 hivi W.K.

      “Mungu Alikuwa Ametuita” (Mdo. 16:6-15)

      4, 5. (a) Ni nini kilichotokea Paulo na wenzake walipokaribia Bithinia? (b) Wanafunzi hao waliamua kufanya nini, na matokeo yalikuwa nini?

      4 Walipozuiwa kuhubiri Asia, Paulo na wenzake walienda upande wa kaskazini ili kuhubiri katika majiji ya Bithinia. Huenda walitembea kwa siku kadhaa kwenye vijia katika maeneo yasiyo na watu wengi ya Frigia na Galatia ili wafike huko. Hata hivyo, walipokaribia Bithinia, Yesu alitumia tena roho takatifu kuwazuia. (Mdo. 16:6, 7) Kufikia wakati huo, huenda wanaume hao hawakuelewa wafanye nini. Walikuwa na ujumbe wa kuhubiri, walijua jinsi ya kuhubiri, lakini hawakujua mahali pa kuhubiri. Ni kana kwamba walikuwa wamepiga hodi kwenye mlango wa kuingia Asia, lakini hawakuruhusiwa kuingia. Walipiga hodi kwenye mlango wa kuingia Bithinia, na hapo pia, hawakuruhusiwa kuingia. Paulo alikuwa ameazimia kuendelea kupiga hodi mpaka apate mlango utakaofunguka. Kisha, wanaume hao wakafanya uamuzi ambao huenda ukaonekana kuwa usiopatana na akili. Waliamua kwenda upande wa magharibi na kutembea kilomita 550, wakipita majiji mengi mpaka wakafika bandari ya Troa, ambako wangeweza kusafiri baharini kwenda Makedonia. (Mdo. 16:8) Naam, kwa mara ya tatu, Paulo alipiga hodi na mlango ukafunguka wazi kabisa.

      5 Luka, mwandishi wa Injili, aliyejiunga na Paulo na wenzake huko Troa, aliandika kilichotokea: “Paulo akaona maono usiku—mwanamume Mmakedonia alikuwa amesimama hapo akimsihi: “Vuka uingie Makedonia utusaidie.” Mara tu alipoona maono hayo, tukajaribu kuingia Makedonia, tukikata kauli kwamba Mungu alikuwa ametuita tuwatangazie habari njema.”a (Mdo. 16:9, 10) Sasa, Paulo alijua mahali pa kuhubiri. Bila shaka alifurahi sana kwa sababu hakukata tamaa alipokuwa njiani! Mara moja, wanaume hao wanne wakasafiri kwa mashua kwenda Makedonia.

      Mtume Paulo na Timotheo wakiwa wamesimama kwenye meli. Timotheo akionyesha kitu fulani kilicho mbali huku wafanyakazi wa meli wakiendelea na kazi.

      “Basi tukatoka Troa na kusafiri . . . baharini.”—Matendo 16:11

      6, 7. (a) Tunaweza kujifunza nini kutokana na mambo yaliyotokea katika safari ya Paulo? (b) Tunaweza kuwa na uhakika gani kutokana na mambo yaliyompata Paulo?

      6 Tunaweza kujifunza nini kutokana na masimulizi hayo? Kumbuka jambo hili: Roho ya Mungu iliingilia kati baada ya Paulo kufunga safari kwenda Asia. Yesu aliingilia kati baada ya Paulo kukaribia Bithinia. Na Yesu alimwelekeza Paulo aende Makedonia, baada ya Paulo kufika Troa. Yesu akiwa Kichwa cha kutaniko anaweza kutuongoza kwa njia kama hiyo pia. (Kol. 1:18) Kwa mfano, huenda tumefikiria kuwa mapainia au kuhamia eneo lenye uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme. Hata hivyo, Yesu anaweza kutumia roho ya Mungu kutuongoza baada ya sisi kuchukua hatua zinazohitajika ili kutimiza malengo yetu. Kwa nini? Fikiria mfano huu: Dereva anaweza kuongoza gari kuelekea upande wa kushoto au kulia likiwa mwendoni, lakini hawezi kufanya hivyo ikiwa gari hilo limesimama. Vivyo hivyo, Yesu hutusaidia kupanua utumishi wetu, ikiwa tuko mwendoni, yaani, tunajitahidi kabisa kufikia malengo yetu.

      7 Tufanye nini ikiwa mwanzoni hatupati matokeo yoyote? Je, tukate tamaa tukifikiri kwamba hatuna roho ya Mungu? Hapana. Kumbuka kwamba haikuwa rahisi pia kwa Paulo kufikia malengo yake. Lakini aliendelea kutafuta mpaka alipopata mlango uliofunguka. Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atabariki jitihada zetu tukivumilia na kuendelea kutafuta “mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji.”​—1 Kor. 16:9.

      8. (a) Filipi lilikuwa jiji la aina gani? (b) Ni jambo gani lenye kufurahisha lililotokea baada ya Paulo kuhubiri “mahali pa sala”?

      8 Baada ya kufika wilaya ya Makedonia, Paulo na wenzake walielekea Filipi, jiji lenye wakaaji waliojivunia kuwa raia wa Roma. Askari-jeshi Waroma waliostaafu waliishi huko na waliona jiji hilo kuwa Italia ndogo, Roma ndogo ya Makedonia. Wakiwa nje ya lango la jiji, kando ya mto mwembamba, wamishonari hao walifika katika eneo ambalo walifikiri ni “mahali pa sala.”b Walipoenda huko siku ya Sabato, waliwakuta wanawake kadhaa waliokuwa wamekusanyika hapo ili kumwabudu Mungu. Wanafunzi hao wakaketi chini na kuzungumza nao. Mwanamke aliyeitwa Lidia “alikuwa akisikiliza, na Yehova akaufungua moyo wake.” Lidia alichochewa sana na mambo aliyojifunza kutoka kwa wamishonari hao hivi kwamba yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Kisha, Lidia akamsihi Paulo na wenzake wakae nyumbani kwake.c—Mdo. 16:13-15.

      9. Wengi leo wanafuata mfano wa Paulo jinsi gani, na wamepata baraka gani?

      9 Wazia shangwe iliyotokea Lidia alipobatizwa! Bila shaka Paulo alifurahi sana kwamba alikubali mwaliko wa ‘kuvuka na kuingia Makedonia’ na Yehova aliona inafaa kumtumia yeye na wenzake kujibu sala za wanawake hao wanaomwogopa Mungu! Leo, ndugu na dada wengi, vijana kwa wazee, waliofunga ndoa kwa waseja, uhamia maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi wa wahubiri wa Ufalme. Ni kweli kwamba kuna hali nyingi ngumu, hata hivyo, haziwezi kulinganishwa na uradhi unaotokana na kuwapata watu kama Lidia, ambao hukubali kweli za Biblia. Je, unaweza kufanya marekebisho ili ‘uvuke na kuingia’ katika eneo lenye uhitaji? Utapata baraka nyingi. Kwa mfano, mfikirie Aaron, ndugu mwenye umri wa miaka 20 hivi, ambaye alihamia nchi moja ya Amerika ya Kati. Maoni yake yanafanana na ya wengi, anaposema: “Kutumikia nchi ya kigeni kumenisaidia kukua kiroho na kumkaribia Yehova zaidi. Na utumishi wa shambani unafurahisha—ninaongoza mafunzo nane ya Biblia!”

      Dada wawili wakimhubiria mwanamke mtaani. Kijana anajaribu kuangalia ili aone wanachozungumzia.

      Tunawezaje ‘kuvuka na kuingia Makedonia?’

      “Umati Ukasimama . . . Dhidi Yao” (Mdo. 16:16-24)

      10. Roho waovu walijaribu kuzuia kazi ya Paulo na wenzake jinsi gani?

      10 Shetani alikasirika sana kuona watu wakijifunza habari njema na kubatizwa katika eneo ambalo yeye na roho wake waovu hawakuwa na upinzani. Si ajabu kwamba roho waovu walihusika kusababisha kipingamizi katika kazi ya kuhubiri ya Paulo na wenzake! Walipokuwa wakienda mahali pale pa kusali, kijakazi fulani mwenye roho mwovu, aliyewapatia mabwana zake faida nyingi kwa kubashiri, alikuwa akimfuata Paulo na wenzake na kusema kwa sauti kubwa: “Watu hawa ni watumwa wa Mungu Aliye Juu Zaidi nao wanawatangazia ninyi njia ya wokovu.” Huenda roho huyo mwovu alimfanya msichana huyo aseme maneno hayo ili ionekane kana kwamba mabashiri yake na mafundisho ya Paulo yanatoka katika chanzo kimoja. Kwa kufanya hivyo, watazamaji wangekengeushwa wasiwasikilize wafuasi wa kweli wa Kristo. Lakini Paulo alimnyamazisha msichana huyo kwa kumfukuza roho huyo mwovu.​—Mdo. 16:16-18.

      11. Baada ya roho mwovu kufukuzwa, ni nini kilichowapata Paulo na Sila?

      11 Mabwana wa kijakazi huyo walipoona kwamba njia yao ya kupata faida imetoweka, wakakasirika sana. Wakawakamata Paulo na Sila na kuwapeleka sokoni, mahali ambapo mahakimu—maofisa wanaowakilisha Roma—walikuwa wakihukumu. Kwa kuwa mabwana hao walijua kwamba mahakimu waliwachukia Wayahudi na walijivunia kuwa Waroma, walitoa madai yanayoonyesha kuwa Paulo na Sila wanasumbua. Ni kana kwamba walisema: ‘Wayahudi hawa wanasumbua kwa kufundisha mapokeo ambayo sisi Waroma hatuwezi kuyakubali.’ Matokeo ya maneno yao yalionekana mara moja. “Umati [uliokuwa sokoni] ukasimama pamoja dhidi yao [Paulo na Sila],” nao mahakimu wakatoa amri “wapigwe kwa fimbo.” Kisha, Paulo na Sila wakapelekwa gerezani. Mlinzi akawatupa ndani ya gereza la ndani zaidi na kuifunga miguu yao katika mikatale. (Mdo. 16:19-24) Mlinzi huyo alipoufunga mlango wa gereza, kulikuwa giza zito hivi kwamba Paulo na Sila hawangeweza kuonana. Hata hivyo, Yehova alikuwa akitazama.​—Zab. 139:12.

      12. (a) Wanafunzi wa Kristo waliyaonaje mateso na kwa nini? (b) Shetani na wale walio chini ya uvutano wake wanawapingaje wafuasi wa Kristo leo?

      12 Miaka kadhaa iliyotangulia, Yesu aliwaambia wafuasi wake: “Watawatesa ninyi.” (Yoh. 15:20) Hivyo, Paulo na wenzake walipovuka ili kuingia Makedonia, walitarajia kukabili upinzani. Walipoanza kuteswa walijua kwamba ni kwa sababu ya hasira ya Shetani na haimaanishi walipoteza kibali cha Yehova. Leo, watu walio chini ya uvutano wa Shetani wanatenda kama watu waliompinga Paulo katika jiji la Filipi. Tukiwa shuleni au kazini, wapinzani hao wasio wanyoofu husema mambo yalipotoka kutuhusu ili kuwachochea wengine watupinge. Katika nchi fulani, wapinzani wa kidini wanatushtaki mahakamani, ni kana kwamba wanasema: ‘Mashahidi hawa wanasumbua kwa kufundisha mapokeo ambayo sisi “waumini wa zamani” hatuwezi kuyakubali.’ Katika maeneo mengine, waabudu wenzetu hupigwa na kutupwa gerezani. Hata hivyo, Yehova anatazama.​—1 Pet. 3:12.

      “Wakabatizwa Bila Kukawia” (Mdo. 16:25-34)

      13. Kwa nini mlinzi aliuliza: “Nifanye nini ili niokolewe?”

      13 Paulo na Sila walihitaji wakati wa kutafakari mambo yaliyowapata. Hata hivyo, kufikia usiku wa manane, walijihisi nafuu kutokana na maumivu hivi kwamba “walikuwa wakisali na kumsifu Mungu kwa wimbo.” Kisha, ghafla, tetemeko la ardhi likatikisa gereza! Mlinzi akaamka, na alipoona milango ya gereza imefunguka, akafikiri wafungwa wametoroka. Akijua kwamba ataadhibiwa kwa kuwaacha wafungwa watoroke, “akauchomoa upanga wake naye karibu ajiue.” Lakini Paulo akamwambia kwa sauti kubwa: “Usijiumize, kwa maana sisi sote tupo hapa!” Mlinzi huyo mwenye wasiwasi akauliza: “Mabwana zangu, nifanye nini ili niokolewe?” Paulo na Sila hawangeweza kumwokoa lakini Yesu pekee angeweza. Kwa hiyo, wakamjibu: “Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa.”​—Mdo. 16:25-31.

      14. (a) Paulo na Sila walimsaidiaje mlinzi wa jela? (b) Paulo na Sila walipata baraka gani kwa kuvumilia mateso kwa shangwe?

      14 Je, mlinzi huyo aliuliza swali hilo kwa unyoofu? Paulo hakutilia shaka unyoofu wake. Mlinzi huyo alikuwa Mtu wa Mataifa, asiyejua Maandiko. Kabla ya kuwa Mkristo, alihitaji kujifunza na kukubali kweli za msingi za Maandiko. Hivyo, Paulo na Sila walitumia wakati ‘kumhubiria neno la Yehova.’ Kwa kuwa walikazia fikira kumfundisha mtu huyo Maandiko huenda walisahau maumivu waliyokuwa nayo. Hata hivyo, mlinzi huyo aliona vidonda migongoni mwao, naye akaviosha. Kisha yeye na familia yake “wakabatizwa bila kukawia.” Paulo na Sila walipata baraka kubwa sana kwa kuvumilia mateso kwa shangwe!—Mdo. 16:32-34.

      15. (a) Mashahidi wengi leo wanafuata mfano wa Paulo na Sila jinsi gani? (b) Kwa nini tuwatembelee tena na tena watu wanaoishi katika eneo letu?

      15 Kama Paulo na Sila, leo, Mashahidi wengi waliofungwa kwa sababu ya imani yao wamepata matokeo mazuri kwa kuhubiri habari njema wakiwa gerezani. Kwa mfano, wakati mmoja kulikuwa na asilimia 40 ya Mashahidi waliojifunza ukweli kumhusu Yehova wakiwa gerezani katika nchi moja ambayo utendaji wetu ulipigwa marufuku. (Isa. 54:17) Pia, kumbuka kwamba mlinzi huyo aliomba msaada baada ya tetemeko la ardhi. Vivyo hivyo, watu fulani leo ambao hawajawahi kukubali ujumbe wa Ufalme huenda wakaukubali baada tu ya ulimwengu wao kutikiswa na jambo fulani lenye kuhuzunisha. Kuwarudia tena na tena watu wanaoishi katika eneo letu, huonyesha kwamba tuko tayari kutoa msaada wakati wowote unapohitajika.

      “Je, Sasa Wanatufukuza kwa Siri?” (Mdo. 16:35-40)

      16. Ni nini kilichotokea siku moja baada ya Paulo na Sila kupigwa viboko?

      16 Siku iliyofuata mahakimu waliamuru Paulo na Sila wafunguliwe. Lakini Paulo akasema: “Walitupiga viboko hadharani bila kutuhukumu, ingawa sisi ni Waroma, na wakatutupa gerezani. Je, sasa wanatufukuza kwa siri? Hapana, haiwezekani! Acha waje watutoe nje wao wenyewe.” Baada ya kutambua kwamba wanaume hao wawili ni raia wa Roma, mahakimu hao “wakaogopa,” kwa sababu walikuwa wamekiuka haki zao.d Mambo yakageuka. Wanafunzi hao walipigwa viboko hadharani; sasa mahakimu walilazimika kuwaomba msamaha hadharani. Wakawasihi Paulo na Sila waondoke Filipi. Walikubali, lakini kwanza wakakitia moyo kikundi kipya cha wanafunzi kilichokuwa kikikua. Kisha wakaondoka.

      17. Uvumilivu wa Paulo na Sila ungeweza kuwafundisha nini wanafunzi wapya?

      17 Ikiwa Paulo na Sila wangesema mwanzoni kwamba wao ni raia wa Roma, huenda hawangepigwa viboko. (Mdo. 22:25, 26) Hata hivyo, huenda wanafunzi wa Filipi wangefikiri kwamba Paulo na Sila walitumia uraia wao kuepuka kuteseka kwa ajili ya Kristo. Kufanya hivyo kungeathirije imani ya wanafunzi ambao hawakuwa raia wa Roma? Sheria haingewazuia wao wasipigwe viboko. Hivyo, kwa kuvumilia adhabu ya viboko Paulo na mwenzake waliwawekea waabudu hao wapya kielelezo kwamba wafuasi wa Kristo wanaweza kusimama imara licha ya mateso. Isitoshe, kwa kusisitiza uraia wao utambuliwe, Paulo na Sila walitaka ijulikane hadharani kwamba mahakimu hao wametenda kinyume cha sheria. Kufanya hivyo kungeweza kuwazuia wasiwatendee vibaya waamini wengine na badala yake kuwapa ulinzi wa kisheria mashambulizi kama hayo yatakapotokea wakati ujao.

      18. (a) Waangalizi Wakristo leo hufuata kielelezo cha Paulo jinsi gani? (b) Tunawezaje “kuitetea na kuithibitisha kisheria habari njema?”

      18 Leo, waangalizi katika kutaniko la Kikristo huliwekea kutaniko kielelezo cha kufuata. Chochote wanachotazamia waabudu wenzao wafanye, Wachungaji hao Wakristo wako tayari kufanya. Kama Paulo, sisi pia huchunguza mambo kwa uangalifu kabla ya kutumia haki zetu za kisheria. Ikihitajika, sisi hukata rufaa katika mahakama za kitaifa na hata za kimataifa ili kutetea uhuru wetu wa ibada. Tunapofanya hivyo, lengo letu si kuleta mapinduzi ya kijamii, bali “kuitetea na kuithibitisha kisheria habari njema” kama Paulo alivyoliandikia kutaniko la Filipi miaka kumi hivi baada ya kufungwa huko. (Flp. 1:7) Hata mahakama itoe uamuzi gani, tumeazimia kuendelea ‘kutangaza habari njema’ popote ambapo roho ya Mungu itatuongoza kama Paulo na wenzake walivyofanya.​—Mdo. 16:10.

      LUKA—MWANDISHI WA KITABU CHA MATENDO

      Kuanzia sura ya 1 hadi sura ya 16 mstari wa 9 wa kitabu cha Matendo, mwandishi wa kitabu cha matendo anazungumzia mambo ambayo wengine wanasema na kufanya. Hata hivyo, kuanzia Matendo 16:10, 11, mtindo wa uandikaji unabadilika. Kwa mfano, katika mstari wa 11, mwandishi anasema: “Tukatoka Troa na kusafiri moja kwa moja baharini hadi Samothrake.” Hapa ndipo mwandishi Luka, alianza kujihusisha katika matukio yanayosimuliwa. Hata hivyo, kwa kuwa jina la Luka halipatikani mahali popote katika kitabu cha Matendo ya Mitume, tunajuaje kwamba yeye ndiye mwandishi wa kitabu hicho?

      Luka amekaa akiandika kwenye kitabu cha kukunjwa kilicho mezani.

      Tunaweza kupata jibu kwa kuchunguza utangulizi wa kitabu cha Matendo na Injili ya Luka. Utangulizi wa vitabu vyote viwili unataja mtu anayeitwa “Theofilo.” (Luka 1:1, 3; Mdo. 1:1) Utangulizi wa kitabu cha Matendo unasema: “Lile simulizi la kwanza, ewe Theofilo, niliandika kuhusu mambo yote ambayo Yesu alianza kufanya na kufundisha.” Kwa kuwa wasomi wenye kutegemeka wamekubali kwa muda mrefu kwamba “lile simulizi la kwanza,” yaani, Injili, liliandikwa na Luka, basi lazima pia aliandika kitabu cha Matendo.

      Hatujui mengi kumhusu Luka. Jina lake linapatikana mara tatu tu katika Biblia. Mtume Paulo anamwita Luka “daktari mpendwa” na ‘mfanyakazi mwenzake.’ (Kol. 4:14; Flm. 24) Sehemu za kitabu cha Matendo ambazo Luka anajihusisha katika masimulizi zinaonyesha kwamba Luka alisafiri pamoja na mtume Paulo kutoka Troa mpaka Filipi mwaka wa 50 W.K. hivi, lakini Paulo alipoondoka Filipi, Luka hakusafiri pamoja naye. Wanaume hao wawili walikutana tena Filipi mwaka wa 56 W.K. hivi na kusafiri pamoja na ndugu wengine saba kutoka Filipi kwenda Yerusalemu, ambapo Paulo alikamatwa. Miaka miwili baadaye, Luka alisafiri pamoja na Paulo, akiwa mfungwa, kutoka Kaisaria kwenda Roma. (Mdo. 16:10-17, 40; 20:5–21:17; 24:27; 27:1–28:16) Paulo alifungwa Roma kwa mara ya pili, na hata alipotambua kwamba anakaribia kuuawa, ni “Luka tu” ndiye aliyekuwa pamoja naye. (2 Tim. 4:6, 11) Ni wazi kwamba Luka alisafiri maeneo ya mbali na alikuwa tayari kuteseka kwa ajili ya habari njema.

      Luka hakudai kwamba alijionea mambo aliyoandika kumhusu Yesu. Badala yake, anasema kwamba alijitahidi ‘kukusanya habari kuhusu mambo aliyosadiki kabisa’ yaliyosimuliwa na “mashahidi wa kujionea.” Anaendelea kusema, “nimefuatilia mambo yote kwa usahihi tangu mwanzo, nami nimeamua kukuandikia mambo hayo kwa utaratibu mzuri.” (Luka 1:1-3) Kitabu cha Luka kinaonyesha wazi kwamba alifanya utafiti kwa makini. Huenda alimhoji Elisabeti, Maria, mama ya Yesu, na wengine ili kukusanya habari za kuandika. Mambo mengi aliyoandika hayapatikani katika vitabu vingine vya Injili.​—Luka 1:5-80.

      Mtume Paulo alisema kwamba Luka alikuwa daktari, na masimulizi yake ya Injili yanaonyesha wazi alihangaishwa na afya ya watu walioteseka. Kwa mfano: Luka aliandika kwamba Yesu alipomponya mtu aliyesumbuliwa na roho mwovu, “yule roho mwovu akamtoka bila kumuumiza.” Pia, aliandika kwamba mama mkwe wa mtume Petro alikuwa na “homa kali,” na kwamba mwanamke ambaye Yesu alimsaidia alisumbuliwa na “roho ya udhaifu kwa miaka 18, mwili wake ulikuwa umepindika na hangeweza kusimama wima.”​—Luka 4:35, 38; 13:11.

      Luka alitanguliza “kazi ya Bwana” maishani mwake. (1 Kor. 15:58) Lengo lake lilikuwa kuwasaidia wengine wamjue na kumtumikia Yehova bali si kutafuta utajiri au umashuhuri.

      LIDIA—MUUZAJI WA BIDHAA ZA RANGI YA ZAMBARAU

      Lidia aliishi Filipi, jiji mashuhuri katika wilaya ya Makedonia. Alitoka Thiatira, jiji lililokuwa magharibi mwa Asia Ndogo katika eneo linaloitwa Lidia. Ili kuendeleza biashara yake, Lidia alihamia eneo la ng’ambo ya Bahari ya Aegea. Inawezekana aliuza bidhaa mbalimbali za rangi ya zambarau, kama vile mazulia, mapambo, vitambaa, na hata rangi yenyewe. Maandishi yaliyopatikana Filipi yanathibitisha kwamba kulikuwa na kikundi cha wauzaji wa bidhaa za zambarau katika jiji hilo.

      Lidia akionyesha kitambaa.

      Kwa kuwa Lidia anatajwa kuwa “mwabudu wa Mungu,” huenda aligeuzwa imani na kuwa mfuasi wa dini ya Kiyahudi. (Mdo. 16:14) Inawezekana alikuwa amepata habari fulani kuhusu ibada ya Yehova katika jiji la nyumbani kwao. Tofauti na Filipi, jiji la kwao lilikuwa na sinagogi la Wayahudi. Watu fulani wanaamini kwamba Lidia lilikuwa jina la utani—linalomaanisha “Mwanamke kutoka Lidia”​—ambalo alipewa alipokuwa Filipi. Hata hivyo, kuna uthibitisho unaoonyesha kwamba kulikuwa na wanawake wengine walioitwa Lidia.

      Tangu siku za Homer, katika karne ya tisa au nane K.W.K., watu wa Lidia na majirani zao walijulikana kwa ustadi wao wa kutia rangi ya zambarau kwenye vitambaa. Maji ya Thiatira yalijulikana kwa kutokeza “rangi nyangavu na zinazodumu sana.”

      Bidhaa za zambarau zilikuwa ghali sana na zingeweza kununuliwa na matajiri tu. Ingawa rangi ya zambarau ingeweza kupatikana kutoka katika vitu mbalimbali, rangi bora na iliyokuwa ghali zaidi—iliyowekwa kwenye vitambaa laini—ilitokana na samaki-gamba wa Mediterania. Kila samaki angeweza kutokeza tone moja tu la rangi hiyo, na ili kupata gramu moja ya rangi hiyo ya pekee, samaki 8,000 hivi walihitajika. Ndiyo sababu nguo za rangi hiyo zilikuwa ghali sana.

      Inawezekana Lidia alikuwa mfanyabiashara tajiri kwa sababu biashara yake ilihitaji awe na pesa nyingi na pia alikuwa na nyumba kubwa ambapo Paulo, Sila, Timotheo, na Luka wangeweza kukaa. Biblia inataja “watu wa nyumbani mwake,” huenda alikuwa anaishi na watu wake wa ukoo, au alikuwa na vijakazi na watumishi. (Mdo. 16:15) Na kwa kuwa kabla ya kuondoka katika jiji hilo, Paulo na Sila walikutana na ndugu kadhaa katika nyumba ya mwanamke huyo mkarimu, inawezekana kwamba baadaye nyumba hiyo ilikuwa mahali ambapo Wakristo wa kwanza katika jiji la Filipi walikutana kwa ajili ya ibada.​—Mdo. 16:40.

      Miaka kumi baadaye, Paulo alipoliandikia barua kutaniko la Filipi, hakumtaja Lidia. Kwa hiyo habari pekee tulizo nazo kumhusu ni zile zinazopatikana katika sura ya 16 ya kitabu cha Matendo.

      a Ona sanduku lenye kichwa “Luka—Mwandishi wa Kitabu cha Matendo.”

      b Huenda Wayahudi hawakuruhusiwa kuwa na sinagogi katika jiji la Filipi kwa sababu lilikuwa jiji la kijeshi. Au labda jiji hilo halikuwa na angalau wanaume kumi Wayahudi—idadi ya chini zaidi iliyohitajiwa ili kuwa na sinagogi.

      c Ona sanduku lenye kichwa “Lidia—Muuzaji wa Bidhaa za Rangi ya Zambarau.”

      d Kulingana na sheria ya Roma, raia alikuwa na haki ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa naye hakupaswa kamwe kuadhibiwa hadharani kabla ya kuthibitishwa kuwa mwenye hatia.

  • “Akajadiliana Nao Akitumia Maandiko”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • SURA YA 17

      “Akajadiliana Nao Akitumia Maandiko”

      Msingi mzuri wa kufundisha; mfano mzuri uliowekwa na Waberoya

      Matendo 17:1-15

      1, 2. Ni nani wanaosafiri kutoka Filipi kwenda Thesalonike, na huenda wanafikiria nini?

      BARABARA nzuri sana iliyojengwa na wahandisi stadi kutoka Roma. Barabara hiyo iliyojipinda inapitia milimani. Kuna kelele nyingi—milio ya punda, kelele za magurudumu ya magari ya kukokotwa, na kelele za wasafiri. Huenda wasafiri walitia ndani wanajeshi, wafanyabiashara, na mafundi. Paulo, Sila na Timotheo wanatumia barabara hiyo kusafiri kutoka Filipi kwenda Thesalonike, umbali wa zaidi ya kilomita 130. Safari hiyo si rahisi, hasa kwa Paulo na Sila kwa kuwa bado walikuwa na majeraha waliyopata Filipi, ambako walipigwa kwa fimbo.​—Mdo. 16:22, 23.

      2 Ni nini kitakachowasaidia wasivunjwe moyo na safari ndefu iliyo mbele yao? Ni mazungumzo yao wanapokuwa njiani. Bado wanakumbuka vizuri jambo la kustaajabisha lililotokea huko Filipi, jinsi yule mlinzi wa jela pamoja na familia yake walivyokuwa waamini. Tukio hilo limewachochea waazimie hata zaidi kuendelea kutangaza neno la Mungu. Hata hivyo, wanapokaribia jiji la Thesalonike lililo pwani, hawajui jinsi watakavyotendewa na Wayahudi katika jiji hilo. Je, watashambuliwa, na hata kupigwa kama ilivyokuwa Filipi?

      3. Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Paulo wa kujipa ujasiri ili kuhubiri?

      3 Baadaye Paulo alieleza hisia zake alipowaandikia Wakristo katika jiji la Thesalonike: “Ingawa kwanza tulikuwa tumeteseka na kudharauliwa huko Filipi, kama mnavyojua, tulijipa ujasiri kupitia Mungu wetu ili tuwatangazie ninyi habari njema ya Mungu licha ya upinzani.” (1 The. 2:2) Inaonekana Paulo alisitasita kwenda Thesalonike, hasa baada ya mambo yaliyotokea Filipi. Je, unaweza kuelewa hisia za Paulo? Je, kuna wakati unahisi ni vigumu kuhubiri habari njema? Paulo alimtegemea Yehova ili apate nguvu, na kumwezesha kujipa ujasiri. Mfano wake unaweza kukusaidia kufanya hivyo pia.​—1 Kor. 4:16.

      “Akajadiliana . . . Akitumia Maandiko” (Mdo. 17:1-3)

      4. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Paulo alikaa jijini Thesalonike kwa zaidi ya majuma matatu?

      4 Masimulizi yanasema kwamba Paulo alipokuwa Thesalonike, alihubiri katika sinagogi kwa Sabato tatu. Hilo halimaanishi kwamba alikaa jijini humo kwa majuma matatu tu. Huenda Paulo hakuweza kwenda kwenye sinagogi mara tu alipofika Thesalonike. Isitoshe, barua za Paulo zinaonyesha kwamba wakiwa Thesalonike, yeye na wenzake walifanya kazi ili kupata mahitaji yao. (1 The. 2:9; 2 The. 3:7, 8) Akiwa huko, Paulo alipokea vitu fulani mara mbili kwa ajili ya mahitaji yake kutoka kwa akina ndugu wa Filipi. (Flp. 4:16) Hivyo inaonekana alikaa jijini Thesalonike kwa zaidi ya majuma matatu.

      5. Paulo alichocheaje fikira za wasikilizaji wake?

      5 Baada ya kujipa ujasiri wa kuhubiri, Paulo alizungumza na watu waliokuwa wamekusanyika katika sinagogi. Kulingana na desturi yake, ‘akajadiliana nao akitumia Maandiko, akieleza na kuthibitisha kwa marejeo kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na kufufuliwa kutoka kwa wafu, akisema: “Huyu ndiye Kristo, Yesu huyu ninayewatangazia ninyi.”’ (Mdo. 17:2, 3) Lengo la Paulo halikuwa kuwasisimua tu wasikilizaji wake bali kuchochea fikira zao. Alijua kwamba watu waliokuwa katika sinagogi waliyajua Maandiko na kuyaheshimu lakini hawakuyaelewa. Hivyo, Paulo alijadili, akafafanua, na kuthibitisha kwa kutumia Maandiko kwamba Yesu wa Nazareti ndiye Masihi, au Kristo, aliyeahidiwa.

      6. Yesu aliwathibitishiaje wanafunzi wake kwa kutumia Maandiko, na matokeo yalikuwa nini?

      6 Paulo alifuata mfano wa Yesu wa kutumia Maandiko kama msingi wa mafundisho yake. Kwa mfano, katika huduma yake, Yesu aliwaambia wafuasi wake kwamba kulingana na Maandiko, lazima Mwana wa binadamu ateseke na kufa, kisha afufuliwe. (Mt. 16:21) Baada ya kufufuliwa, Yesu aliwatokea wanafunzi wake, na hivyo kuthibitisha kwamba alikuwa amesema kweli. Hata hivyo, Yesu aliwapa uthibitisho zaidi. Tunasoma hivi kuhusu mazungumzo yake na wanafunzi fulani: “Akawafafanulia kuanzia Musa na Manabii wote, mambo yote ambayo Maandiko yalisema kumhusu.” Ikawaje? Wanafunzi wakasema hivi kwa mshangao: “Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka alipokuwa akizungumza nasi barabarani, na alipokuwa akitufungulia Maandiko waziwazi?”​—Luka 24:13, 27, 32.

      7. Kwa nini ni muhimu kutumia Maandiko kama msingi wa mafundisho yetu?

      7 Ujumbe wa Neno la Mungu una nguvu. (Ebr. 4:12) Kama Yesu, Paulo, na mitume wengine, Wakristo leo hutegemea Neno la Mungu wanapowafundisha watu. Sisi pia hujadili, hufafanua Maandiko, na kuwathibitishia watu mambo tunayowafundisha kwa kuwafungulia Biblia na kuwaonyesha kile ambacho inasema. Ujumbe tunaohubiri si wetu. Tunapotumia Biblia, tunawasaidia kutambua kwamba hatufundishi maoni yetu, bali mafundisho ya Mungu. Pia, tunakumbuka kwamba msingi wa ujumbe wetu ni Neno la Mungu. Neno hilo linategemeka kabisa. Kwa kuwa tunajua kwamba ujumbe wetu unategemeka, tunahubiri kwa ujasiri kama Paulo.

      “Baadhi . . . Wakaamini” (Mdo. 17:4-9)

      8-10. (a) Watu jijini Thesalonike waliitikiaje habari njema? (b) Kwa nini baadhi ya Wayahudi walimwonea wivu Paulo? (c) Wapinzani Wayahudi walitendaje?

      8 Tayari Paulo alikuwa amejionea ukweli wa maneno haya ya Yesu: “Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia; ikiwa wamelishika neno langu, watalishika lenu pia.” (Yoh. 15:20) Jijini Thesalonike, Paulo alikutana na watu wenye maoni mbalimbali, baadhi yao walikuwa tayari kutii neno na wengine walipinga. Kuhusu wale waliokubali, Luka anaandika hivi: “Baadhi yao [Wayahudi] wakaamini [wakawa Wakristo] na kujiunga na Paulo na Sila, pia umati mkubwa wa Wagiriki waliomwabudu Mungu, vilevile wanawake wengi mashuhuri.” (Mdo. 17:4) Wanafunzi hao wapya walifurahi kusaidiwa kuyaelewa Maandiko.

      9 Ingawa baadhi yao walithamini maneno ya Paulo, wengine walimkasirikia sana. Wayahudi fulani jijini Thesalonike walimwonea wivu Paulo kwa sababu “umati mkubwa wa Wagiriki” ulikubali ujumbe wake. Wayahudi hao, wakiwa na lengo la kupata wafuasi, waliwafundisha Watu wa Mataifa waliokuwa Wagiriki mafundisho kutoka katika Maandiko ya Kiebrania, na waliwaona Wagiriki hao kuwa mali yao. Hata hivyo, ilianza kuonekana kana kwamba Paulo anawanyakua Wagiriki hao, tena hapohapo kwenye sinagogi! Wayahudi hao walikasirika sana.

      Paulo na Sila wakitoroka umati wenye hasira kupitia lango la nyuma. Mwanamume amesimama langoni akizungumza na umati wenye hasira.

      ‘Walitaka Paulo na Sila waletwe nje kwenye kile kikundi.’—Matendo 17:5

      10 Luka anatueleza kilichofuata: “Wayahudi wakawa na wivu, wakakusanya wanaume fulani waovu waliokuwa wakizurura sokoni, wakafanyiza kikundi chenye ghasia kisha wakazusha fujo jijini. Wakaishambulia nyumba ya Yasoni wakitaka Paulo na Sila waletwe nje kwenye kile kikundi. Walipowakosa wakamkokota Yasoni na baadhi ya akina ndugu mpaka kwa watawala wa jiji, wakisema kwa sauti kubwa: ‘Watu hawa ambao wameipindua dunia inayokaliwa wako hapa pia, naye Yasoni amewakaribisha. Watu hao wote wanapinga maagizo ya Kaisari, wakisema kuna mfalme mwingine, Yesu.’” (Mdo. 17:5-7) Mashambulizi hayo yangewaathirije Paulo na wenzake?

      11. Paulo na wenzake walishtakiwa kwa makosa gani, na huenda waliowashtaki walidai wamevunja amri gani? (Ona maelezo ya chini)

      11 Kikundi chenye ghasia ni kama mto uliovunja kingo zake, wenye nguvu nyingi na usiozuilika. Wayahudi walitumia kikundi hicho ili kujaribu kuwafukuza Paulo na Sila. Baada ya “kuzusha fujo jijini,” wakajaribu kuwasadikisha watawala kwamba mashtaka yao yalikuwa mazito. Shtaka la kwanza lilikuwa kwamba Paulo na wenzake “wameipindua dunia inayokaliwa,” ingawa Paulo na wenzake hawakusababisha fujo jijini Thesalonike! Shtaka la pili lilikuwa zito zaidi. Wayahudi walidai kwamba wamishonari hao wanamtangaza Mfalme mwingine, Yesu, na hivyo wanavunja sheria ya maliki.a

      12. Ni nini kinachoonyesha kwamba mashtaka dhidi ya Wakristo jijini Thesalonike yangeweza kuwa na matokeo mabaya?

      12 Kumbuka kwamba viongozi wa kidini walimshtaki Yesu kwa madai yanayofanana na hayo. Walimwambia Pilato: “Tulimkuta mtu huyu akipindua taifa letu . . . akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo mfalme.” (Luka 23:2) Huenda Pilato aliogopa kuwa maliki angefikiri ameachilia kosa kubwa la uhaini, ndio sababu alimhukumu Yesu kwamba anastahili kufa. Vivyo hivyo, mashtaka dhidi ya Wakristo jijini Thesalonike yangekuwa na matokeo mabaya. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema: “Mashtaka hayo yalikuwa hatari sana. Ikiwa mtu angetuhumiwa kuwa anataka kumsaliti Maliki, angeweza kuhukumiwa kifo.’” Je, mashtaka hayo yenye chuki yangefanikiwa?

      13, 14. (a) Kwa nini kikundi chenye ghasia hakikufanikiwa? (b) Paulo alifuata jinsi gani ushauri wa Kristo wa kuwa waangalifu, nasi tunawezaje kuiga mfano wake?

      13 Umati huo wenye ghasia ulishindwa kukomesha kazi ya kuhubiri jijini Thesalonike. Kwa nini? Kwanza, Paulo na Sila hawakupatikana. Isitoshe, inaonekana kwamba watawala wa jiji hilo hawakuamini mashtaka hayo. Baada ya kuchukua “dhamana ya kutosha,” walimwachilia Yasoni na ndugu wengine waliofikishwa mbele yao. (Mdo. 17:8, 9) Paulo alifuata ushauri wa Yesu wa kuwa ‘mwangalifu kama nyoka na asiye na hatia kama njiwa.’ (Mt. 10:16) Alifanya hivyo kwa kuondoka kwa busara mahali penye hatari na kwenda kuhubiri mahali pengine. Bila shaka, ujasiri wa Paulo haukuwa wa kijinga. Wakristo wanawezaje kuiga mfano wake?

      14 Leo, mara nyingi viongozi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo huwachochea watu wawafanyie fujo Mashahidi wa Yehova. Wamewachochea watawala wawatese kwa kudai kwamba Mashahidi wanaipinga serikali au si wazalendo. Kama karne ya kwanza, wapinzani wa leo huchochewa na wivu. Wakristo wa kweli hawajihatarishi bila sababu. Sisi huepuka kubishana na watu wenye hasira na wakaidi, badala yake tunaendelea kufanya kazi yetu kwa amani, na ikiwezekana tunawarudia baadaye wanapokuwa wametulia.

      KAISARI WANAOTAJWA KATIKA KITABU CHA MATENDO

      Matukio yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Matendo na katika Maandiko yote ya Kigiriki ya Kikristo, yalitokea katika Milki ya Roma. Kwa hiyo, sikuzote maliki Mroma ndiye aliyekuwa na mamlaka kuu zaidi. Wayahudi wa Thesalonike walipozungumzia “maagizo ya Kaisari” walikuwa wakimrejelea maliki (Mdo. 17:7) Maliki wanne walitawala wakati wa kipindi kinachozungumziwa katika kitabu cha Matendo—Tiberio, Gayo, Klaudio wa Kwanza, na Nero.

      • Tiberio (14-37 W.K.) alikuwa maliki wakati wa huduma ya Yesu na miaka michache ya kwanza ya kutaniko la Kikristo. Yesu alipohukumiwa, Wayahudi walikuwa wakirejelea Tiberio walipopiga kelele na kusema: “Ukimfungua mtu huyu, wewe si rafiki ya Kaisari. . . . Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.”​—Yoh. 19:12, 15.

      • Gayo, ambaye pia anaitwa Caligula (37-41 W.K.), hatajwi katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

      • Klaudio wa Kwanza (41-54 W.K.) anatajwa mara mbili katika kitabu cha Matendo. Kama ilivyotabiriwa na nabii Mkristo Agabo, “njaa kubwa” ya mwaka wa 46 hivi W.K., ilitokea “juu ya dunia yote inayokaliwa . . . wakati wa Klaudio.” Pia, mwaka wa 49 au mapema mwaka wa 50 W.K., Klaudio ‘aliagiza Wayahudi wote waondoke Roma,’ amri iliyofanya Akila na Prisila kuhamia Korintho, ambapo walikutana na mtume Paulo.​—Mdo. 11:28; 18:1, 2.

      • Nero (54-68 W.K.) ndiye Kaisari ambaye Paulo alikata rufaa kwake. (Mdo. 25:11) Inasemekana kwamba baadaye maliki huyo alidai kwamba Wakristo ndio waliowasha moto ulioharibu sehemu kubwa ya Roma mwaka wa 64 hivi W.K. Muda mfupi baadaye, mwaka wa 65 hivi W.K., mtume Paulo alifungwa jijini Roma na kuuawa.

      “Walikuwa Wasikivu” (Mdo. 17:10-15)

      15. Waberoya waliitikiaje habari njema?

      15 Kwa ajili ya usalama wao, Paulo na Sila walitumwa Beroya, kilomita 65 hivi kutoka Thesalonike. Walipofika huko, Paulo alienda katika sinagogi na kuanza kuzungumza na watu waliokusanyika huko. Walifurahi sana kwa sababu walipata watu waliosikiliza. Luka aliandika kwamba Wayahudi wa Beroya walikuwa “wasikivu kuliko wale wa Thesalonike, kwa maana walilikubali neno kwa hamu kubwa ya akili, wakiyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku ili kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo.” (Mdo. 17:10, 11) Hili halimaanishi kwamba Wathesalonike waliokubali kweli walikuwa na mtazamo mbaya. Baadaye Paulo aliwaandikia: “Tunamshukuru Mungu bila kuacha, kwa kuwa mlipolipokea neno la Mungu, ambalo mlilisikia kutoka kwetu, mlilikubali si kama neno la wanadamu, bali kama lilivyo kwa kweli, neno la Mungu, ambalo pia linafanya kazi ndani yenu waamini.” (1 The. 2:13) Hata hivyo, ni nini kilichowafanya Wayahudi waliokuwa Beroya kuwa wasikivu zaidi?

      16. Kwa nini Waberoya waliitwa “wasikivu”?

      16 Ingawa ilikuwa habari mpya kwa Waberoya, hawakutilia shaka au kuichambua. Haimaanishi walidanganyika kwa urahisi. Kwanza walimsikiliza Paulo kwa makini. Kisha, wakahakikisha mambo waliyojifunza kwa kusoma Maandiko ambayo Paulo aliwasaidia kuyaelewa. Isitoshe, walikuwa wakijifunza Neno la Mungu kila siku, si siku ya Sabato tu. Na walifanya hivyo “kwa hamu kubwa ya akili,” wakijitahidi kujua mambo ambayo Maandiko yanasema kuhusu mafundisho hayo mapya. Pia, walionyesha unyenyekevu kwa kufanya mabadiliko na “wengi wao wakawa waamini.” (Mdo. 17:12) Ndiyo sababu Luka anasema kwamba walikuwa “wasikivu”!

      17. Kwa nini Waberoya ni mfano mzuri wa kuigwa, na tunawezaje kudumisha mtazamo huo hata ikiwa tumekuwa katika kweli kwa muda mrefu?

      17 Waberoya hao hawakujua kwamba mtazamo wao mzuri kuelekea habari njema ungeandikwa katika Neno la Mungu kwa faida ya wengine. Walifanya kama vile Paulo alivyotarajia na jinsi Yehova Mungu alivyotaka wafanye. Leo, sisi huwatia moyo watu wachunguze Biblia kwa makini ili imani yao itegemee Neno la Mungu. Hata hivyo, baada ya kuwa waamini, je, huo ndio mwisho wa kuwa wasikivu? Hapana, usikivu ni muhimu hata zaidi nasi tunapaswa kuwa na hamu kubwa zaidi ya kujifunza kutoka kwa Yehova na kutumia mambo tunayojifunza maishani. Kwa kufanya hivyo, tunamruhusu Yehova atufinyange na kutuzoeza kulingana na mapenzi yake. (Isa. 64:8) Hivyo, tunampendeza Baba yetu wa mbinguni naye ataendelea kututumia kutimiza makusudi yake.

      18, 19. (a) Kwa nini Paulo aliondoka Beroya, na tunajifunza nini kutokana na mfano wake? (b) Paulo anapaswa kuwahubiria nani sasa, na wapi?

      18 Paulo hakukaa Beroya kwa muda mrefu. Tunasoma hivi: “Wayahudi kutoka Thesalonike waliposikia kwamba Paulo alikuwa akitangaza pia neno la Mungu huko Beroya, wakaja huko ili kuchochea na kuuvuruga umati. Mara moja akina ndugu wakamsindikiza Paulo mpaka baharini, lakini Sila na Timotheo wakabaki huko. Hata hivyo, wale waliomsindikiza Paulo wakaenda naye mpaka Athene, kisha wakarudi baada ya kupokea maagizo kwamba Sila na Timotheo wamfuate Paulo haraka iwezekanavyo.” (Mdo. 17:13-15) Adui hao wa habari njema hawakukata tamaa! Hawakutosheka kwamba Paulo ameondoka Thesalonike; walimfuata mpaka Beroya na kujaribu kuwachochea watu wa huko pia, lakini hawakufanikiwa. Paulo alijua kwamba eneo ni kubwa, kwa hiyo alienda kuhubiri eneo lingine. Sisi pia, tuazimie kusimama imara dhidi ya wale wanaotaka kukomesha kazi yetu ya kuhubiri!

      19 Baada ya kutoa ushahidi kamili kwa Wayahudi wa Thesalonike na Beroya, Paulo alikuwa amejifunza mengi kuhusu umuhimu wa kuhubiri kwa ujasiri na kujadiliana na watu kwa kutumia Maandiko. Sisi pia tumejifunza mengi. Hata hivyo, sasa Paulo anakutana na wasikilizaji tofauti—Watu wa Mataifa jijini Athene. Mambo yatakuwaje katika jiji hilo? Tutaona katika sura inayofuata.

      a Kulingana na msomi mmoja, wakati huo kulikuwa na sheria ya Kaisari iliyokataza utabiri wowote kuhusu “kuja kwa mfalme au ufalme mpya, hasa mfalme anayeweza kumwondoa au kumhukumu maliki anayetawala.” Huenda adui za Paulo walifanya ujumbe wa mtume huyo uonekane kana kwamba unakiuka sheria hiyo. Ona sanduku lenye kichwa “Kaisari Wanaotajwa Katika Kitabu cha Matendo.”

  • “Akajadiliana Nao Akitumia Maandiko”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • SURA YA 17

      “Akajadiliana Nao Akitumia Maandiko”

      Msingi mzuri wa kufundisha; mfano mzuri uliowekwa na Waberoya

      Matendo 17:1-15

      1, 2. Ni nani wanaosafiri kutoka Filipi kwenda Thesalonike, na huenda wanafikiria nini?

      BARABARA nzuri sana iliyojengwa na wahandisi stadi kutoka Roma. Barabara hiyo iliyojipinda inapitia milimani. Kuna kelele nyingi—milio ya punda, kelele za magurudumu ya magari ya kukokotwa, na kelele za wasafiri. Huenda wasafiri walitia ndani wanajeshi, wafanyabiashara, na mafundi. Paulo, Sila na Timotheo wanatumia barabara hiyo kusafiri kutoka Filipi kwenda Thesalonike, umbali wa zaidi ya kilomita 130. Safari hiyo si rahisi, hasa kwa Paulo na Sila kwa kuwa bado walikuwa na majeraha waliyopata Filipi, ambako walipigwa kwa fimbo.​—Mdo. 16:22, 23.

      2 Ni nini kitakachowasaidia wasivunjwe moyo na safari ndefu iliyo mbele yao? Ni mazungumzo yao wanapokuwa njiani. Bado wanakumbuka vizuri jambo la kustaajabisha lililotokea huko Filipi, jinsi yule mlinzi wa jela pamoja na familia yake walivyokuwa waamini. Tukio hilo limewachochea waazimie hata zaidi kuendelea kutangaza neno la Mungu. Hata hivyo, wanapokaribia jiji la Thesalonike lililo pwani, hawajui jinsi watakavyotendewa na Wayahudi katika jiji hilo. Je, watashambuliwa, na hata kupigwa kama ilivyokuwa Filipi?

      3. Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Paulo wa kujipa ujasiri ili kuhubiri?

      3 Baadaye Paulo alieleza hisia zake alipowaandikia Wakristo katika jiji la Thesalonike: “Ingawa kwanza tulikuwa tumeteseka na kudharauliwa huko Filipi, kama mnavyojua, tulijipa ujasiri kupitia Mungu wetu ili tuwatangazie ninyi habari njema ya Mungu licha ya upinzani.” (1 The. 2:2) Inaonekana Paulo alisitasita kwenda Thesalonike, hasa baada ya mambo yaliyotokea Filipi. Je, unaweza kuelewa hisia za Paulo? Je, kuna wakati unahisi ni vigumu kuhubiri habari njema? Paulo alimtegemea Yehova ili apate nguvu, na kumwezesha kujipa ujasiri. Mfano wake unaweza kukusaidia kufanya hivyo pia.​—1 Kor. 4:16.

      “Akajadiliana . . . Akitumia Maandiko” (Mdo. 17:1-3)

      4. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Paulo alikaa jijini Thesalonike kwa zaidi ya majuma matatu?

      4 Masimulizi yanasema kwamba Paulo alipokuwa Thesalonike, alihubiri katika sinagogi kwa Sabato tatu. Hilo halimaanishi kwamba alikaa jijini humo kwa majuma matatu tu. Huenda Paulo hakuweza kwenda kwenye sinagogi mara tu alipofika Thesalonike. Isitoshe, barua za Paulo zinaonyesha kwamba wakiwa Thesalonike, yeye na wenzake walifanya kazi ili kupata mahitaji yao. (1 The. 2:9; 2 The. 3:7, 8) Akiwa huko, Paulo alipokea vitu fulani mara mbili kwa ajili ya mahitaji yake kutoka kwa akina ndugu wa Filipi. (Flp. 4:16) Hivyo inaonekana alikaa jijini Thesalonike kwa zaidi ya majuma matatu.

      5. Paulo alichocheaje fikira za wasikilizaji wake?

      5 Baada ya kujipa ujasiri wa kuhubiri, Paulo alizungumza na watu waliokuwa wamekusanyika katika sinagogi. Kulingana na desturi yake, ‘akajadiliana nao akitumia Maandiko, akieleza na kuthibitisha kwa marejeo kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na kufufuliwa kutoka kwa wafu, akisema: “Huyu ndiye Kristo, Yesu huyu ninayewatangazia ninyi.”’ (Mdo. 17:2, 3) Lengo la Paulo halikuwa kuwasisimua tu wasikilizaji wake bali kuchochea fikira zao. Alijua kwamba watu waliokuwa katika sinagogi waliyajua Maandiko na kuyaheshimu lakini hawakuyaelewa. Hivyo, Paulo alijadili, akafafanua, na kuthibitisha kwa kutumia Maandiko kwamba Yesu wa Nazareti ndiye Masihi, au Kristo, aliyeahidiwa.

      6. Yesu aliwathibitishiaje wanafunzi wake kwa kutumia Maandiko, na matokeo yalikuwa nini?

      6 Paulo alifuata mfano wa Yesu wa kutumia Maandiko kama msingi wa mafundisho yake. Kwa mfano, katika huduma yake, Yesu aliwaambia wafuasi wake kwamba kulingana na Maandiko, lazima Mwana wa binadamu ateseke na kufa, kisha afufuliwe. (Mt. 16:21) Baada ya kufufuliwa, Yesu aliwatokea wanafunzi wake, na hivyo kuthibitisha kwamba alikuwa amesema kweli. Hata hivyo, Yesu aliwapa uthibitisho zaidi. Tunasoma hivi kuhusu mazungumzo yake na wanafunzi fulani: “Akawafafanulia kuanzia Musa na Manabii wote, mambo yote ambayo Maandiko yalisema kumhusu.” Ikawaje? Wanafunzi wakasema hivi kwa mshangao: “Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka alipokuwa akizungumza nasi barabarani, na alipokuwa akitufungulia Maandiko waziwazi?”​—Luka 24:13, 27, 32.

      7. Kwa nini ni muhimu kutumia Maandiko kama msingi wa mafundisho yetu?

      7 Ujumbe wa Neno la Mungu una nguvu. (Ebr. 4:12) Kama Yesu, Paulo, na mitume wengine, Wakristo leo hutegemea Neno la Mungu wanapowafundisha watu. Sisi pia hujadili, hufafanua Maandiko, na kuwathibitishia watu mambo tunayowafundisha kwa kuwafungulia Biblia na kuwaonyesha kile ambacho inasema. Ujumbe tunaohubiri si wetu. Tunapotumia Biblia, tunawasaidia kutambua kwamba hatufundishi maoni yetu, bali mafundisho ya Mungu. Pia, tunakumbuka kwamba msingi wa ujumbe wetu ni Neno la Mungu. Neno hilo linategemeka kabisa. Kwa kuwa tunajua kwamba ujumbe wetu unategemeka, tunahubiri kwa ujasiri kama Paulo.

      “Baadhi . . . Wakaamini” (Mdo. 17:4-9)

      8-10. (a) Watu jijini Thesalonike waliitikiaje habari njema? (b) Kwa nini baadhi ya Wayahudi walimwonea wivu Paulo? (c) Wapinzani Wayahudi walitendaje?

      8 Tayari Paulo alikuwa amejionea ukweli wa maneno haya ya Yesu: “Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia; ikiwa wamelishika neno langu, watalishika lenu pia.” (Yoh. 15:20) Jijini Thesalonike, Paulo alikutana na watu wenye maoni mbalimbali, baadhi yao walikuwa tayari kutii neno na wengine walipinga. Kuhusu wale waliokubali, Luka anaandika hivi: “Baadhi yao [Wayahudi] wakaamini [wakawa Wakristo] na kujiunga na Paulo na Sila, pia umati mkubwa wa Wagiriki waliomwabudu Mungu, vilevile wanawake wengi mashuhuri.” (Mdo. 17:4) Wanafunzi hao wapya walifurahi kusaidiwa kuyaelewa Maandiko.

      9 Ingawa baadhi yao walithamini maneno ya Paulo, wengine walimkasirikia sana. Wayahudi fulani jijini Thesalonike walimwonea wivu Paulo kwa sababu “umati mkubwa wa Wagiriki” ulikubali ujumbe wake. Wayahudi hao, wakiwa na lengo la kupata wafuasi, waliwafundisha Watu wa Mataifa waliokuwa Wagiriki mafundisho kutoka katika Maandiko ya Kiebrania, na waliwaona Wagiriki hao kuwa mali yao. Hata hivyo, ilianza kuonekana kana kwamba Paulo anawanyakua Wagiriki hao, tena hapohapo kwenye sinagogi! Wayahudi hao walikasirika sana.

      Paulo na Sila wakitoroka umati wenye hasira kupitia lango la nyuma. Mwanamume amesimama langoni akizungumza na umati wenye hasira.

      ‘Walitaka Paulo na Sila waletwe nje kwenye kile kikundi.’—Matendo 17:5

      10 Luka anatueleza kilichofuata: “Wayahudi wakawa na wivu, wakakusanya wanaume fulani waovu waliokuwa wakizurura sokoni, wakafanyiza kikundi chenye ghasia kisha wakazusha fujo jijini. Wakaishambulia nyumba ya Yasoni wakitaka Paulo na Sila waletwe nje kwenye kile kikundi. Walipowakosa wakamkokota Yasoni na baadhi ya akina ndugu mpaka kwa watawala wa jiji, wakisema kwa sauti kubwa: ‘Watu hawa ambao wameipindua dunia inayokaliwa wako hapa pia, naye Yasoni amewakaribisha. Watu hao wote wanapinga maagizo ya Kaisari, wakisema kuna mfalme mwingine, Yesu.’” (Mdo. 17:5-7) Mashambulizi hayo yangewaathirije Paulo na wenzake?

      11. Paulo na wenzake walishtakiwa kwa makosa gani, na huenda waliowashtaki walidai wamevunja amri gani? (Ona maelezo ya chini)

      11 Kikundi chenye ghasia ni kama mto uliovunja kingo zake, wenye nguvu nyingi na usiozuilika. Wayahudi walitumia kikundi hicho ili kujaribu kuwafukuza Paulo na Sila. Baada ya “kuzusha fujo jijini,” wakajaribu kuwasadikisha watawala kwamba mashtaka yao yalikuwa mazito. Shtaka la kwanza lilikuwa kwamba Paulo na wenzake “wameipindua dunia inayokaliwa,” ingawa Paulo na wenzake hawakusababisha fujo jijini Thesalonike! Shtaka la pili lilikuwa zito zaidi. Wayahudi walidai kwamba wamishonari hao wanamtangaza Mfalme mwingine, Yesu, na hivyo wanavunja sheria ya maliki.a

      12. Ni nini kinachoonyesha kwamba mashtaka dhidi ya Wakristo jijini Thesalonike yangeweza kuwa na matokeo mabaya?

      12 Kumbuka kwamba viongozi wa kidini walimshtaki Yesu kwa madai yanayofanana na hayo. Walimwambia Pilato: “Tulimkuta mtu huyu akipindua taifa letu . . . akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo mfalme.” (Luka 23:2) Huenda Pilato aliogopa kuwa maliki angefikiri ameachilia kosa kubwa la uhaini, ndio sababu alimhukumu Yesu kwamba anastahili kufa. Vivyo hivyo, mashtaka dhidi ya Wakristo jijini Thesalonike yangekuwa na matokeo mabaya. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema: “Mashtaka hayo yalikuwa hatari sana. Ikiwa mtu angetuhumiwa kuwa anataka kumsaliti Maliki, angeweza kuhukumiwa kifo.’” Je, mashtaka hayo yenye chuki yangefanikiwa?

      13, 14. (a) Kwa nini kikundi chenye ghasia hakikufanikiwa? (b) Paulo alifuata jinsi gani ushauri wa Kristo wa kuwa waangalifu, nasi tunawezaje kuiga mfano wake?

      13 Umati huo wenye ghasia ulishindwa kukomesha kazi ya kuhubiri jijini Thesalonike. Kwa nini? Kwanza, Paulo na Sila hawakupatikana. Isitoshe, inaonekana kwamba watawala wa jiji hilo hawakuamini mashtaka hayo. Baada ya kuchukua “dhamana ya kutosha,” walimwachilia Yasoni na ndugu wengine waliofikishwa mbele yao. (Mdo. 17:8, 9) Paulo alifuata ushauri wa Yesu wa kuwa ‘mwangalifu kama nyoka na asiye na hatia kama njiwa.’ (Mt. 10:16) Alifanya hivyo kwa kuondoka kwa busara mahali penye hatari na kwenda kuhubiri mahali pengine. Bila shaka, ujasiri wa Paulo haukuwa wa kijinga. Wakristo wanawezaje kuiga mfano wake?

      14 Leo, mara nyingi viongozi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo huwachochea watu wawafanyie fujo Mashahidi wa Yehova. Wamewachochea watawala wawatese kwa kudai kwamba Mashahidi wanaipinga serikali au si wazalendo. Kama karne ya kwanza, wapinzani wa leo huchochewa na wivu. Wakristo wa kweli hawajihatarishi bila sababu. Sisi huepuka kubishana na watu wenye hasira na wakaidi, badala yake tunaendelea kufanya kazi yetu kwa amani, na ikiwezekana tunawarudia baadaye wanapokuwa wametulia.

      KAISARI WANAOTAJWA KATIKA KITABU CHA MATENDO

      Matukio yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Matendo na katika Maandiko yote ya Kigiriki ya Kikristo, yalitokea katika Milki ya Roma. Kwa hiyo, sikuzote maliki Mroma ndiye aliyekuwa na mamlaka kuu zaidi. Wayahudi wa Thesalonike walipozungumzia “maagizo ya Kaisari” walikuwa wakimrejelea maliki (Mdo. 17:7) Maliki wanne walitawala wakati wa kipindi kinachozungumziwa katika kitabu cha Matendo—Tiberio, Gayo, Klaudio wa Kwanza, na Nero.

      • Tiberio (14-37 W.K.) alikuwa maliki wakati wa huduma ya Yesu na miaka michache ya kwanza ya kutaniko la Kikristo. Yesu alipohukumiwa, Wayahudi walikuwa wakirejelea Tiberio walipopiga kelele na kusema: “Ukimfungua mtu huyu, wewe si rafiki ya Kaisari. . . . Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.”​—Yoh. 19:12, 15.

      • Gayo, ambaye pia anaitwa Caligula (37-41 W.K.), hatajwi katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

      • Klaudio wa Kwanza (41-54 W.K.) anatajwa mara mbili katika kitabu cha Matendo. Kama ilivyotabiriwa na nabii Mkristo Agabo, “njaa kubwa” ya mwaka wa 46 hivi W.K., ilitokea “juu ya dunia yote inayokaliwa . . . wakati wa Klaudio.” Pia, mwaka wa 49 au mapema mwaka wa 50 W.K., Klaudio ‘aliagiza Wayahudi wote waondoke Roma,’ amri iliyofanya Akila na Prisila kuhamia Korintho, ambapo walikutana na mtume Paulo.​—Mdo. 11:28; 18:1, 2.

      • Nero (54-68 W.K.) ndiye Kaisari ambaye Paulo alikata rufaa kwake. (Mdo. 25:11) Inasemekana kwamba baadaye maliki huyo alidai kwamba Wakristo ndio waliowasha moto ulioharibu sehemu kubwa ya Roma mwaka wa 64 hivi W.K. Muda mfupi baadaye, mwaka wa 65 hivi W.K., mtume Paulo alifungwa jijini Roma na kuuawa.

      “Walikuwa Wasikivu” (Mdo. 17:10-15)

      15. Waberoya waliitikiaje habari njema?

      15 Kwa ajili ya usalama wao, Paulo na Sila walitumwa Beroya, kilomita 65 hivi kutoka Thesalonike. Walipofika huko, Paulo alienda katika sinagogi na kuanza kuzungumza na watu waliokusanyika huko. Walifurahi sana kwa sababu walipata watu waliosikiliza. Luka aliandika kwamba Wayahudi wa Beroya walikuwa “wasikivu kuliko wale wa Thesalonike, kwa maana walilikubali neno kwa hamu kubwa ya akili, wakiyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku ili kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo.” (Mdo. 17:10, 11) Hili halimaanishi kwamba Wathesalonike waliokubali kweli walikuwa na mtazamo mbaya. Baadaye Paulo aliwaandikia: “Tunamshukuru Mungu bila kuacha, kwa kuwa mlipolipokea neno la Mungu, ambalo mlilisikia kutoka kwetu, mlilikubali si kama neno la wanadamu, bali kama lilivyo kwa kweli, neno la Mungu, ambalo pia linafanya kazi ndani yenu waamini.” (1 The. 2:13) Hata hivyo, ni nini kilichowafanya Wayahudi waliokuwa Beroya kuwa wasikivu zaidi?

      16. Kwa nini Waberoya waliitwa “wasikivu”?

      16 Ingawa ilikuwa habari mpya kwa Waberoya, hawakutilia shaka au kuichambua. Haimaanishi walidanganyika kwa urahisi. Kwanza walimsikiliza Paulo kwa makini. Kisha, wakahakikisha mambo waliyojifunza kwa kusoma Maandiko ambayo Paulo aliwasaidia kuyaelewa. Isitoshe, walikuwa wakijifunza Neno la Mungu kila siku, si siku ya Sabato tu. Na walifanya hivyo “kwa hamu kubwa ya akili,” wakijitahidi kujua mambo ambayo Maandiko yanasema kuhusu mafundisho hayo mapya. Pia, walionyesha unyenyekevu kwa kufanya mabadiliko na “wengi wao wakawa waamini.” (Mdo. 17:12) Ndiyo sababu Luka anasema kwamba walikuwa “wasikivu”!

      17. Kwa nini Waberoya ni mfano mzuri wa kuigwa, na tunawezaje kudumisha mtazamo huo hata ikiwa tumekuwa katika kweli kwa muda mrefu?

      17 Waberoya hao hawakujua kwamba mtazamo wao mzuri kuelekea habari njema ungeandikwa katika Neno la Mungu kwa faida ya wengine. Walifanya kama vile Paulo alivyotarajia na jinsi Yehova Mungu alivyotaka wafanye. Leo, sisi huwatia moyo watu wachunguze Biblia kwa makini ili imani yao itegemee Neno la Mungu. Hata hivyo, baada ya kuwa waamini, je, huo ndio mwisho wa kuwa wasikivu? Hapana, usikivu ni muhimu hata zaidi nasi tunapaswa kuwa na hamu kubwa zaidi ya kujifunza kutoka kwa Yehova na kutumia mambo tunayojifunza maishani. Kwa kufanya hivyo, tunamruhusu Yehova atufinyange na kutuzoeza kulingana na mapenzi yake. (Isa. 64:8) Hivyo, tunampendeza Baba yetu wa mbinguni naye ataendelea kututumia kutimiza makusudi yake.

      18, 19. (a) Kwa nini Paulo aliondoka Beroya, na tunajifunza nini kutokana na mfano wake? (b) Paulo anapaswa kuwahubiria nani sasa, na wapi?

      18 Paulo hakukaa Beroya kwa muda mrefu. Tunasoma hivi: “Wayahudi kutoka Thesalonike waliposikia kwamba Paulo alikuwa akitangaza pia neno la Mungu huko Beroya, wakaja huko ili kuchochea na kuuvuruga umati. Mara moja akina ndugu wakamsindikiza Paulo mpaka baharini, lakini Sila na Timotheo wakabaki huko. Hata hivyo, wale waliomsindikiza Paulo wakaenda naye mpaka Athene, kisha wakarudi baada ya kupokea maagizo kwamba Sila na Timotheo wamfuate Paulo haraka iwezekanavyo.” (Mdo. 17:13-15) Adui hao wa habari njema hawakukata tamaa! Hawakutosheka kwamba Paulo ameondoka Thesalonike; walimfuata mpaka Beroya na kujaribu kuwachochea watu wa huko pia, lakini hawakufanikiwa. Paulo alijua kwamba eneo ni kubwa, kwa hiyo alienda kuhubiri eneo lingine. Sisi pia, tuazimie kusimama imara dhidi ya wale wanaotaka kukomesha kazi yetu ya kuhubiri!

      19 Baada ya kutoa ushahidi kamili kwa Wayahudi wa Thesalonike na Beroya, Paulo alikuwa amejifunza mengi kuhusu umuhimu wa kuhubiri kwa ujasiri na kujadiliana na watu kwa kutumia Maandiko. Sisi pia tumejifunza mengi. Hata hivyo, sasa Paulo anakutana na wasikilizaji tofauti—Watu wa Mataifa jijini Athene. Mambo yatakuwaje katika jiji hilo? Tutaona katika sura inayofuata.

      a Kulingana na msomi mmoja, wakati huo kulikuwa na sheria ya Kaisari iliyokataza utabiri wowote kuhusu “kuja kwa mfalme au ufalme mpya, hasa mfalme anayeweza kumwondoa au kumhukumu maliki anayetawala.” Huenda adui za Paulo walifanya ujumbe wa mtume huyo uonekane kana kwamba unakiuka sheria hiyo. Ona sanduku lenye kichwa “Kaisari Wanaotajwa Katika Kitabu cha Matendo.”

  • “Wamtafute Mungu, . . . na kwa Kweli Wampate”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • SURA YA 18

      “Wamtafute Mungu, . . . na kwa Kweli Wampate”

      Paulo aweka msingi mzuri wa mazungumzo na kubadilika kulingana na hali ya wasikilizaji wake

      Matendo 17:16-34

      1-3. (a) Ni nini kilichomkasirisha mtume Paulo akiwa Athene? (b) Tunaweza kujifunza nini kwa kuchunguza mfano wa Paulo?

      PAULO amekasirika sana. Yuko jijini Athene, kitovu cha elimu nchini Ugiriki, ambako wakati fulani wanafalsafa kama vile Sokratesi, Plato, na Aristoto walifundisha. Athene ni jiji la kidini. Pande zote—mahekaluni, katika viwanja vya watu wote, na barabarani—Paulo anaona sanamu nyingi, kwa sababu Waathene huabudu miungu mingi sana. Paulo anajua maoni ya Mungu wa kweli, Yehova, kuhusiana na ibada ya sanamu. (Kut. 20:4, 5) Mtume huyo mwaminifu ana maoni kama ya Yehova—anachukia sanamu!

      2 Paulo anashangazwa sana na mambo anayoona anapoingia sokoni. Kuna sanamu nyingi za mungu Herme zenye umbo la kiungo cha uzazi cha kiume zilizowekwa upande wa kaskazini-magharibi, karibu na lango kuu. Soko hilo lina madhabahu nyingi. Mtume huyo mwenye bidii atahubiri jinsi gani katika jiji hilo ambalo ibada ya sanamu imekita mizizi? Je, ataonyesha sifa ya kujizuia na kuweka msingi mzuri wa mazungumzo kwa wasikilizaji wake? Je, atafaulu kumsaidia yeyote amtafute Mungu wa kweli na kumwabudu?

      3 Hotuba ya Paulo, iliyo katika Matendo 17:22-31, ambayo aliitoa mbele za watu hao wenye elimu inaonyesha kwamba alitumia ushawishi, busara, na utambuzi. Mfano wa Paulo unaweza kutusaidia sana kujua jinsi ya kuweka msingi mzuri wa mazungumzo na kuwasaidia wasikilizaji wetu kufikiri.

      Kufundisha “Sokoni” (Mdo. 17:16-21)

      4, 5. Paulo alihubiri wapi akiwa Athene, naye alikutana na watu wa aina gani?

      4 Katika safari yake ya pili ya umishonari, mwaka wa 50 hivi W.K., Paulo alitembelea jiji la Athene.a Alipokuwa akiwasubiri Sila na Timotheo wafike kutoka Beroya, Paulo “akaanza kujadiliana katika sinagogi pamoja na Wayahudi,” kama ilivyokuwa desturi yake. Pia alienda “sokoni,” mahali ambapo angeweza kuwapata watu wa Athene wasio Wayahudi. (Mdo. 17:17) Soko hilo lililokuwa na ukubwa wa ekari 12 hivi, lilikuwa upande wa kaskazini-magharibi mwa Ngome ya Athene. Halikuwa mahali pa kuuza na kununua tu, bali pia uwanja wa watu wote. Kitabu fulani cha marejeo kinasema kwamba mahali hapo palikuwa “kituo cha kibiashara, kisiasa na kitamaduni jijini humo.” Waathene walipenda kukusanyika hapo na kuzungumzia mambo mbalimbali ya kitaalamu.

      ATHENE—KITUO CHA UTAMADUNI KATIKA ULIMWENGU WA KALE

      Watu walianza kuandika historia ya jiji la Athene katika karne ya saba K.W.K. Hata hivyo, jiji hilo lilikuwa jiji lenye ngome hata kabla ya wakati huo. Athene lilikuja kuwa jiji kuu la wilaya ya Attica na lilikuwa na ukubwa wa kilomita za mraba 2,500. Jiji hilo lilizungukwa na milima na bahari. Inaonekana kuna uhusiano kati ya jina la jiji hilo na jina la mungu wa jiji hilo, Athena.

      Katika karne ya sita K.W.K., Solon, mtunga sheria Mwathene, alianzisha mabadiliko ya kijamii, kisiasa, kisheria, na kiuchumi katika jiji hilo. Aliboresha maisha ya maskini na kuweka msingi wa mfumo wa serikali za kidemokrasia. Hata hivyo, ilikuwa demokrasia ya watu huru tu, walio wengi bado walikuwa watumwa.

      Baada ya ushindi mbalimbali wa Wagiriki dhidi ya Waajemi katika karne ya tano K.W.K., Athene likawa jiji kuu la milki ndogo iliyokuwa ikifanya biashara kupitia bahari kuanzia Italia na Sisili upande wa magharibi hadi Kipro na Siria upande wa mashariki. Jiji hilo lilipofanya maendeleo makubwa, likawa kituo cha utamaduni katika ulimwengu wa kale, likifanya vizuri katika sanaa, michezo ya kuigiza, falsafa, ufasaha wa kusema, uandishi, na sayansi. Jiji hilo lilikuwa na majengo ya umma na mahekalu mengi. Kutoka mbali, mtu angeweza kukiona kilima kilichokuwa kwenye jiji hilo, ambacho juu yake kulikuwa na hekalu la Parthenon, lililokuwa na sanamu ya Athena, yenye urefu wa mita 12, iliyotengenezwa kwa dhahabu na pembe za tembo.

      Jiji la Athene lilishindwa na kuporwa, kwanza na Wasparta, kisha Wamakedonia, na mwishowe Waroma. Hata hivyo, wakati wa mtume Paulo, bado Athene lilikuwa jiji maarufu kwa sababu ya sifa zake za wakati uliopita. Jiji hilo halikuwa kamwe sehemu ya mikoa ya Roma, bali lilipewa mamlaka ya kujitawala na kutunga sheria zake na halikuhitajika kulipa kodi zilizotozwa na serikali ya Roma. Ingawa Athene lilipoteza umashuhuri, liliendelea kuwa jiji lenye chuo kikuu, ambako watoto wa matajiri walienda kusoma.

      5 Akiwa sokoni, Paulo alikutana na watu ambao hawakuwa tayari kumsikiliza. Baadhi ya wasikilizaji wake walikuwa Waepikurea na Wastoa, ambao waliamini falsafa mbili tofauti.b Waepikurea waliamini kwamba uhai ulijitokeza wenyewe tu. Kwa ufupi, waliamini hivi: “Mungu hawezi kutufanya lolote; Hakuna maumivu yoyote katika kifo; Mambo mema yanaweza kufanywa; Mambo mabaya yanaweza kuvumiliwa.” Wastoa walikazia falsafa za kibinadamu nao hawakuamini kwamba kuna Mungu. Waepikurea na Wastoa hawakuamini ufufuo ambao wanafunzi wa Kristo walifundisha. Ni wazi kwamba maoni ya kifalsafa ya vikundi hivyo viwili hayakupatana hata kidogo na Ukristo wa kweli, ambao Paulo alikuwa akitangaza.

      6, 7. Wasomi Wagiriki waliyaonaje mafundisho ya Paulo, na hali ikoje leo?

      6 Wasomi Wagiriki walionaje mafundisho ya Paulo? Baadhi yao walimwita “mpigadomo.” (Mdo. 17:18) Kuhusu neno la Kigiriki linalotumika katika mstari huo, msomi mmoja anasema hivi: “Mwanzoni neno hilo lilitumiwa kurejelea ndege mdogo anayerukaruka akiokota punje, pia lilitumiwa kurejelea watu waliokuwa wakiokota masalio ya vyakula na vitu vingine vilivyoanguka sokoni. Baadaye, neno hilo lilianza kutumiwa kwa njia ya mfano kurejelea mtu anayekusanya habari hapa na pale, na hasa yule ambaye haelewi habari zenyewe.” Kwa kumwita “mpiga-domo,” ni kana kwamba wasomi hao walisema kwamba Paulo ni mtu anayerudia-rudia mambo asiyoelewa, ambayo amesikia kutoka kwa wengine. Kama tutakavyoona, Paulo hakuvunjika moyo kwa kuitwa jina hilo.

      7 Ndivyo ilivyo leo. Tukiwa Mashahidi wa Yehova, mara nyingi tunasemwa vibaya kwa sababu ya imani yetu inayotegemea Biblia. Kwa mfano, walimu fulani hudai kwamba fundisho la mageuzi ni la kweli na kwamba ikiwa una akili, utaliamini. Ni kana kwamba wanadai wote wanaopinga fundisho hilo ni wajinga. Wasomi hao wanataka watu wengine watuone sisi kuwa wajinga kwa sababu tunafundisha mambo ambayo Biblia inasema na kuthibitisha kwamba vitu vyote viliumbwa. Hata hivyo, hilo halituvunji moyo. Badala yake, tunasema tukiwa na uhakika kwamba uhai uliopo duniani ulitokana na Muumba mwenye akili, Yehova Mungu.​—Ufu. 4:11.

      8. (a) Baadhi ya watu waliomsikia Paulo akihubiri walikuwa na maoni gani? (b) Kwa nini Paulo alipelekwa Areopago? (Ona maelezo ya chini katika ukurasa wa 142.)

      8 Wengine waliomsikiliza Paulo akihubiri sokoni walikuwa na maoni tofauti. Walisema: “Inaonekana anatangaza miungu ya kigeni.” (Mdo. 17:18) Je, ni kweli Paulo alikuwa akiwatangazia Waathene miungu ya kigeni? Hilo lilikuwa jambo zito. Karne kadhaa mapema, Sokratesi alihukumiwa kifo kwa mashtaka kama hayo. Hivyo, haishangazi kwamba Paulo alipelekwa Areopago na kuambiwa afafanue mafundisho hayo yaliyokuwa mageni kwa Waathene.c Paulo angeuteteaje ujumbe wake mbele ya watu hao wasiojua Maandiko?

      WAEPIKUREA NA WASTOA

      Waepikurea na Wastoa walikuwa na falsafa mbili zinazotofautiana. Vikundi vyote viwili havikuamini ufufuo.

      Waepikurea waliamini kwamba kuna miungu lakini walifikiri kwamba miungu hiyo haipendezwi na wanadamu, nayo haingewathawabisha wala kuwaadhibu, kwa hiyo kusali au kutoa dhabihu ni kazi bure. Waepikurea waliona kwamba anasa ndilo jambo kuu maishani. Fikira na matendo yao hayakuzingatia maadili hata kidogo. Watu walihimizwa wawe na kiasi ili tu kuepuka madhara ya kufanya mambo kupita kiasi. Waliamini kwamba elimu ni muhimu ikiwa tu inamsaidia mtu asiamini mafundisho ya dini yanayosababisha hofu na ya ushirikina.

      Kwa upande mwingine, Wastoa waliamini kwamba vitu vyote ni sehemu ya mungu asiye na utu na kwamba nafsi ya binadamu inatoka katika chanzo kama hicho. Wastoa fulani waliamini kwamba hatimaye nafsi ingeharibiwa pamoja na ulimwengu. Wastoa wengine waliamini kwamba hatimaye nafsi ingechukuliwa tena na mungu huyo. Kulingana na wanafalsafa Wastoa, furaha ingeweza kupatikana kwa kutii sheria za asili.

      “Wanaume wa Athene, Ninaona” (Mdo. 17:22, 23)

      9-11. (a) Paulo aliwekaje msingi mzuri wa mazungumzo? (b) Tunawezaje kufuata mfano wa Paulo katika huduma?

      9 Kumbuka kwamba Paulo alikasirika kwa sababu ya ibada ya sanamu aliyojionea, ambayo ilienea sana. Badala ya kuanza kuishambulia ibada ya sanamu, alikuwa mtulivu. Alitumia busara, na kujitahidi kuwavutia wasikilizaji wake kwa kuweka msingi mzuri wa mazungumzo. Alianza kwa kusema hivi: “Wanaume wa Athene, ninaona kwamba katika mambo yote mnaonekana kuwa mnaogopa sana miungu kuliko watu wengine.” (Mdo. 17:22) Ni kana kwamba Paulo alikuwa akisema ‘Naona mnapenda sana mambo ya dini.’ Paulo alitenda kwa hekima alipowapongeza kwa sababu walipendezwa na mambo ya dini. Alitambua kwamba baadhi ya watu waliopofushwa na imani za uwongo wanaweza kusikiliza. Isitoshe, alijua kwamba wakati fulani hata yeye mwenyewe ‘alitenda bila ujuzi na hakuwa na imani.’​—1 Tim. 1:13.

      10 Baada ya kuweka msingi mzuri, Paulo alieleza kwamba ameona jambo linalothibitisha kuwa watu wa Athene wanapenda mambo ya dini. Aliona madhabahu iliyotengwa kwa ajili ya “Mungu Asiyejulikana.” Kulingana na kitabu kimoja, “Wagiriki walikuwa na mazoea ya kutenga madhabahu kwa ajili ya ‘miungu isiyojulikana,’ ili wasimsahau mungu fulani katika ibada yao, na hivyo kumkasirisha.” Kwa kutenga madhabahu hiyo, Waathene walikiri kwamba kuna Mungu ambaye hawamjui. Paulo alitumia madhabahu hiyo kuwa msingi wa kuwahubiria habari njema. Alieleza: “Kile mnachoabudu bila kujua, hicho ndicho ninachowatangazia.” (Mdo. 17:23) Paulo alitoa hoja zenye nguvu kwa busara. Hakuwa akiwahubiria mungu mpya au wa kigeni, kama watu fulani walivyodai. Alikuwa akiwaeleza kuhusu Mungu ambaye hawakumjua—Mungu wa kweli.

      11 Tunawezaje kumwiga Paulo katika huduma yetu? Tukiwa wenye utambuzi, tunaweza kugundua ikiwa mtu anapendezwa na mambo ya dini, labda kwa kuona vitu fulani vya kidini ambavyo amevaa au vilivyo katika nyumba yake au kwenye uwanja wake. Tunaweza kusema: ‘Naona unapendezwa na mambo ya dini. Nilitaka kuzungumza na mtu kama wewe.’ Kwa kumpongeza, tunaweza kuweka msingi mzuri wa mazungumzo. Kumbuka kwamba lengo letu si kuwahukumu watu kwa sababu ya imani yao. Wakati fulani, baadhi ya waabudu wenzetu waliamini mafundisho ya uwongo kwa kutojua.

      Mvulana akiwaeleza jambo fulani mwalimu na wanafunzi wenzake katika darasa la Sayansi.

      Jitahidi kuweka msingi mzuri wa mazungumzo

      Mungu “Hayuko Mbali na Kila Mmoja Wetu” (Mdo. 17:24-28)

      12. Paulo alibadili mazungumzo yake jinsi gani ili yawafae wasikilizaji wake?

      12 Tayari Paulo aliweka msingi mzuri wa mazungumzo, lakini je, alijenga vizuri juu ya msingi huo? Akijua kwamba wasikilizaji wake wamefunzwa falsafa za Kigiriki na hawayajui Maandiko, alitumia mbinu mbalimbali. Kwanza alitaja mafundisho ya Biblia bila kunukuu Maandiko moja kwa moja. Pili, alijihusisha kwenye mazungumzo, nyakati nyingine alitumia maneno kama vile “sisi,” na “tuna-.” Tatu, alinukuu vitabu vya Kigiriki ili kuonyesha kwamba mambo fulani aliyokuwa akifundisha yalikuwa katika vitabu vyao wenyewe. Acheni sasa tuchanganue hotuba ya Paulo iliyokuwa na matokeo mazuri. Aliwajulisha Waathene kweli gani muhimu kuhusu Mungu ambaye hawakumjua?

      13. Paulo alieleza nini kuhusu ulimwengu, na maneno yake yalikuwa na ujumbe gani?

      13 Mungu aliumba ulimwengu. Paulo alisema hivi: “Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, akiwa, kama alivyo, Bwana wa mbingu na dunia, hakai katika mahekalu yaliyotengenezwa kwa mikono.”d (Mdo. 17:24) Ulimwengu haukujitokeza wenyewe. Mungu wa kweli ndiye Muumba wa vitu vyote. (Zab. 146:6) Tofauti na Athena au miungu mingine ambayo utukufu wao ulitegemea mahekalu na madhabahu, mahekalu yaliyojengwa na mikono ya wanadamu hayawezi kumtosha Bwana Mwenye Enzi Kuu wa mbingu na dunia. (1 Fal. 8:27) Ujumbe wa Paulo ulikuwa wazi: Mungu wa kweli ni mkuu kuliko sanamu yoyote iliyotengenezwa na mwanadamu iliyo katika mahekalu yaliyojengwa na wanadamu.​—Isa. 40:18-26.

      14. Paulo alionyeshaje kwamba Mungu hawategemei wanadamu?

      14 Mungu hawategemei wanadamu. Waabudu-sanamu walipamba sanamu zao kwa nguo maridadi, walizipatia zawadi za bei ghali, au kuzipelekea vyakula na vinywaji—kana kwamba sanamu zilihitaji vitu hivyo! Hata hivyo, huenda baadhi ya wanafalsafa Wagiriki waliomsikiliza Paulo hawakuamini kwamba mungu anahitaji chochote kutoka kwa wanadamu. Ikiwa ndivyo, basi walikubaliana na maneno ya Paulo kwamba Mungu “hatumikiwi kwa mikono ya binadamu kana kwamba anahitaji kitu chochote.” Hakuna kitu chochote cha kimwili ambacho wanadamu wanaweza kumpa Muumba! Badala yake, Mungu huwapa wanadamu wanachohitaji—“uhai na pumzi na vitu vyote,” kutia ndani jua, mvua, na udongo wenye rutuba. (Mdo. 17:25; Mwa. 2:7) Kwa hiyo, Mungu aliye Mpaji, hawezi kuwategemea wanadamu ambao ni wapokeaji.

      15. Paulo alishughulikiaje maoni ya Waathene kwamba wao ni bora kuliko watu wasio Wagiriki, nasi tunajifunza nini kutokana na mfano wake?

      15 Mungu alimuumba mwanadamu. Waathene waliamini kwamba wao ni bora kuliko watu wasio Wagiriki. Lakini ubaguzi haupatani na kweli ya Biblia. (Kum. 10:17) Paulo alizungumzia kwa busara na ustadi jambo hilo ambalo lingeweza kutokeza ubishi. Huenda waliomsikiliza walitulia na kufikiri aliposema, “[Mungu] alifanyiza kila taifa la watu kutoka kwa mtu mmoja.” (Mdo. 17:26) Alikuwa akirejelea masimulizi ya Mwanzo kuhusu Adamu, baba ya wanadamu wote. (Mwa. 1:26-28) Kwa kuwa wanadamu wote wana baba mmoja, hakuna jamii au taifa bora kuliko lingine. Wasikilizaji wa Paulo walielewa vizuri hoja yake. Mfano huu unatufundisha jambo muhimu. Ingawa tunapaswa kutumia busara na kuwa wenye usawaziko katika kazi yetu ya kuhubiri, hatupaswi kamwe kupunguza uzito wa kweli ya Biblia ili kufanya watu wakubali ujumbe wetu.

      16. Muumba ana kusudi gani kwa wanadamu?

      16 Mungu alikusudia wanadamu wawe na uhusiano wa karibu pamoja naye. Hata ikiwa wanafalsafa waliomsikiliza Paulo walikuwa wamejadiliana kwa muda mrefu kuhusu kusudi la uhai wa binadamu, hawangeweza kamwe kutoa jibu sahihi na linaloeleweka. Hata hivyo, Paulo alieleza waziwazi kusudi la Muumba kwa wanadamu, kwamba “wamtafute Mungu, ikiwa watapapasa-papasa wakimtafuta na kwa kweli wampate, ingawa, kwa hakika, hayuko mbali na kila mmoja wetu.” (Mdo. 17:27) Mungu ambaye Waathene hawakumjua anaweza kujulikana. Hayuko mbali na wale ambao kwa kweli wanataka kumtafuta na kumjua. (Zab. 145:18) Ona kwamba Paulo anatumia maneno “kila mmoja wetu,” akijitia ndani kati ya wale wanaohitaji ‘kumtafuta’ na ‘kupapasa-papasa wakimtafuta’ Mungu.

      17, 18. Kwa nini wanadamu wanapaswa kumkaribia Mungu, nasi tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Paulo alivyozungumza na wasikilizaji wake?

      17 Wanadamu wanapaswa kumkaribia Mungu. Paulo alisema kwamba, kwa sababu ya Mungu “tuko hai, tunatembea, na tunaishi.” Wasomi fulani husema kwamba Paulo alikuwa akirejelea maneno ya Epimenide, mshairi Mgiriki wa karne ya sita K.W.K. “aliyeheshimiwa sana katika utamaduni wa dini ya Waathene.” Paulo alitaja sababu nyingine inayopaswa kuwafanya wanadamu wahisi wako karibu na Mungu, aliposema: “Baadhi ya washairi wenu wamesema, ‘Kwa maana sisi pia ni watoto wake.’” (Mdo. 17:28) Wanadamu wanapaswa kujiona kuwa na uhusiano wa karibu sana na Mungu, kwa kuwa Yeye ndiye Baba ya mwanadamu wa kwanza ambaye wanadamu wote walitoka kwake. Ili kuwavutia wasikilizaji wake, Paulo alitumia busara kwa kunukuu moja kwa moja vitabu vya Kigiriki ambavyo bila shaka watu waliomsikiliza waliviheshimu sana.e Kama Paulo, nyakati nyingine tunaweza kunukuu vitabu vya historia, ensaiklopedia, au vitabu vingine vya marejeo vinavyoheshimika. Kwa mfano, nukuu inayofaa kutoka katika chanzo kinachotegemeka, inaweza kumsaidia mtu ambaye si Shahidi kujua chanzo cha mazoea au maadhimisho fulani ya dini za uwongo.

      18 Kufikia hapa, Paulo ameeleza kweli za msingi kumhusu Mungu, akitumia maneno yake kwa ustadi ili yawafae wasikilizaji wake. Mtume huyo alitaka Waathene hao watumie jinsi gani habari hizo muhimu? Bila kukawia, aliendelea kutoa hotuba yake na kuwaambia wanalopaswa kufanya.

      “Wanadamu Wote Kila Mahali . . . Wanapaswa Kutubu” (Mdo. 17:29-31)

      19, 20. (a) Paulo alitumia busara jinsi gani kuonyesha ubatili wa kuabudu sanamu zilizotengenezwa na wanadamu? (b) Waliomsikiliza Paulo walihitaji kuchukua hatua gani?

      19 Paulo alikuwa tayari kuwahimiza wasikilizaji wake wachukue hatua. Akirejelea tena nukuu kutoka kwa waandishi Wagiriki, alisema: “Kwa hiyo, kwa kuwa sisi ni watoto wa Mungu, hatupaswi kufikiri kwamba Mungu ni kama dhahabu au fedha au jiwe, kama kitu kilichochongwa kwa ufundi na ubunifu wa wanadamu.” (Mdo. 17:29) Kwa kweli, ikiwa wanadamu wametoka kwa Mungu, inawezekanaje Mungu awe sanamu zinazotengenezwa na wanadamu? Njia ya Paulo ya kujadiliana nao ilionyesha ubatili wa kuabudu sanamu zilizotengenezwa na wanadamu. (Zab. 115:4-8; Isa. 44:9-20) Huenda Paulo alifanya iwe rahisi kwa wasikilizaji wake kukubali ushauri wake kwa kujihusisha katika mazungumzo na kusema, “hatupaswi.”

      20 Paulo alionyesha wazi kabisa kwamba wanahitaji kuchukua hatua. Alisema: “Mungu ameachilia nyakati hizo za kutojua [za kufikiri kwamba Mungu angependezwa na watu wanaoabudu sanamu]; lakini sasa anawatangazia wanadamu wote kila mahali kwamba wanapaswa kutubu.” (Mdo. 17:30) Huenda baadhi wa wasikilizaji wa Paulo walishangaa kusikia kwamba wanapaswa kutubu. Hata hivyo, hotuba yake yenye nguvu ilionyesha wazi kwamba Mungu ndiye chanzo cha uhai wao na kwa sababu hiyo wanawajibika mbele Zake. Wanahitaji kumtafuta Mungu, kujifunza ukweli kumhusu, na kupatanisha maisha yao na ukweli huo. Kwa Waathene, hilo lilimaanisha kutambua na kuacha kabisa dhambi ya kuabudu sanamu.

      21, 22. Paulo alimaliza hotuba yake kwa maneno gani yenye kuchochea, nayo yanatuhusu jinsi gani?

      21 Paulo alimaliza hotuba yake kwa maneno yenye kuchochea sana: “[Mungu] ameweka siku ambayo anakusudia kuihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa kupitia mwanamume ambaye amemweka rasmi, naye ametoa uhakikisho kamili kwa watu wote kwa kuwa amemfufua kutoka kwa wafu.” (Mdo. 17:31) Siku ya Hukumu inayokuja—hiyo ni sababu nzuri ya kumtafuta na kumpata Mungu wa kweli! Paulo hakutaja jina la Hakimu huyo aliyewekwa rasmi. Badala yake, alisema jambo la kustaajabisha kumhusu Hakimu huyo: Aliishi akiwa mwanadamu, akafa, na kufufuliwa na Mungu!

      22 Umalizio huo wenye kuchochea una umuhimu mkubwa kwetu. Tunajua kwamba Yesu Kristo aliyefufuliwa ndiye Hakimu aliyewekwa rasmi na Mungu. (Yoh. 5:22) Pia tunajua kwamba Siku ya Hukumu ina urefu wa miaka elfu moja, nayo inakaribia sana. (Ufu. 20:4, 6) Hatuogopi Siku ya Hukumu, kwa kuwa tunajua itawaletea baraka nyingi wale watakaohukumiwa kuwa waaminifu. Kufufuliwa kwa Yesu Kristo kunatuhakikishia kwamba tumaini letu la kuwa na maisha bora ya wakati ujao litatimia hakika!

      “Wanaume . . . [Wakawa] Waamini” (Mdo. 17:32-34)

      23. Watu waliitikia hotuba ya Paulo katika njia gani mbalimbali?

      23 Watu waliitikia hotuba ya Paulo kwa njia mbalimbali. Waliposikia kuhusu ufufuo, “baadhi yao wakaanza kumdhihaki.” Wengine walikuwa watulivu lakini hawakutaka kuchukua hatua yoyote, nao wakamwambia: “Tutakusikiliza kuhusu jambo hili wakati mwingine.” (Mdo. 17:32) Hata hivyo, wachache kati yao waliitikia vizuri: “Wanaume fulani wakajiunga naye na kuwa waamini. Miongoni mwao kulikuwa na Dionisio, aliyekuwa mwamuzi wa mahakama ya Areopago, na mwanamke aliyeitwa Damari, na wengineo.” (Mdo. 17:34) Ndivyo inavyokuwa pia katika huduma yetu. Huenda watu fulani wakatudhihaki, na wengine ingawa wanatuheshimu, lakini hawataki kuchukua hatua yoyote. Hata hivyo, sisi hufurahi sana baadhi yao wanapokubali ujumbe wa Ufalme na kuwa waamini.

      24. Tunaweza kujifunza nini kutokana na hotuba aliyotoa Paulo alipokuwa amesimama Areopago?

      24 Tunapochanganua hotuba ya Paulo, tunaweza kujifunza mengi kuhusu mpangilio mzuri wa habari, hoja zenye kusadikisha, na jinsi ya kubadilika kulingana na hali za wasikilizaji wetu. Pia, tunaweza kujifunza faida ya kuwa na subira na busara tunapozungumza na watu ambao wamepofushwa na imani za uwongo za kidini. Pia, tunaweza kujifunza somo hili muhimu: Hatupaswi kamwe kupunguza uzito wa kweli za Biblia ili tu kuwafurahisha wasikilizaji wetu. Hata hivyo, tukifuata mfano wa Paulo, tunaweza kuwa walimu wenye matokeo mazuri katika utumishi wa shambani. Isitoshe, waangalizi wanaweza kuwa walimu stadi kutanikoni. Hivyo, tutakuwa tayari kuwasaidia wengine “wamtafute Mungu . . . na kwa kweli wampate.”​—Mdo. 17:27.

      a Ona sanduku lenye kichwa “Athene—Kituo cha Utamaduni Katika Ulimwengu wa Kale.”

      b Ona sanduku lenye kichwa “Waepikurea na Wastoa.”

      c Kilima cha Areopago kilikuwa upande wa kaskazini-magharibi mwa Ngome ya Athene, mahali ambapo baraza kuu la Athene lilikutana. Huenda jina “Areopago” lilirejelea baraza hilo au kilima chenyewe. Hivyo, wasomi hawajui kihususa ikiwa Paulo alipelekwa kwenye kilima hicho au karibu na eneo, au mahali pengine ambapo baraza hilo lilikutana, labda sokoni.

      d Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “ulimwengu” ni koʹsmos. Ijapokuwa Wagiriki walilitumia neno hilo kurejelea ulimwengu halisi, neno koʹsmos kwa kawaida hutumika katika Biblia kurejelea watu. Inawezekana kwamba Paulo, aliyekuwa akijaribu kuweka msingi mzuri wa mazungumzo kati yake na Wagiriki waliomsikiliza, alitumia neno hilo katika maana hiyo.

      e Paulo alinukuu shairi linaloitwa Phaenomena, la Arato, mshairi Mstoa. Maneno kama hayo yanapatikana katika vitabu vingine vya Kigiriki kutia ndani wimbo unaoitwa Hymn to Zeus, uliotungwa na Kleanthe, mwandikaji Mstoa.

  • “Endelea Kusema na Usinyamaze”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • SURA YA 19

      “Endelea Kusema na Usinyamaze”

      Paulo ajitegemeza kimwili na kutanguliza huduma

      Matendo 18:1-22

      1-3. Mtume Paulo ameenda Korintho kufanya nini, na anakabili changamoto gani?

      NI MWISHONI mwa mwaka wa 50 W.K. Mtume Paulo yuko Korintho, jiji tajiri lenye wakaaji wengi Wagiriki, Waroma, na Wayahudi.a Paulo hakwenda kununua wala kuuza bidhaa au kutafuta kazi ya kimwili. Ameenda hapo ili kufanya kazi muhimu zaidi—kutoa ushahidi kuhusu Ufalme wa Mungu. Hata hivyo, Paulo anahitaji mahali pa kuishi, na hataki kuwa mzigo kwa wengine. Hataki mtu yeyote afikiri kwamba anajiruzuku kutokana na neno la Mungu. Atafanya nini?

      2 Paulo ana ujuzi wa kutengeneza mahema. Kazi ya kutengeneza mahema si rahisi, hata hivyo, yuko tayari kufanya kazi kwa mikono yake ili ajitegemeze. Je, atapata kazi katika jiji hili lenye shughuli nyingi? Je, atapata mahali pazuri pa kuishi? Ingawa ana mahitaji mengi, Paulo hasahau kamwe kazi yake kuu, kazi ya kuhubiri.

      3 Paulo alikaa Korintho kwa muda fulani, naye alipata matokeo mazuri katika huduma yake. Ni mambo gani tunayoweza kujifunza kutokana na utendaji mbalimbali wa Paulo alipokuwa Korintho ambayo yanaweza kutusaidia kutoa ushahidi kamili kuhusu Ufalme wa Mungu katika eneo letu?

      KORINTHO—JIJI LENYE BAHARI MBILI

      Jiji la kale la Korintho lilikuwa kwenye kipande cha eneo kinachounganisha nchi ya Ugiriki na rasi ya kusini inayoitwa Peloponesia. Sehemu nyembamba zaidi ya eneo hilo ilikuwa na upana usiozidi kilomita sita, na kwa sababu hiyo Korintho lilikuwa na bandari mbili. Bandari ya Lekayo, ilikuwa kwenye Ghuba ya Korintho, na ilitumiwa na meli zilizokuwa zikielekea magharibi hadi Hispania, Italia, na Sisili. Na bandari ya Kenkrea, iliyokuwa katika Ghuba ya Saroni, ilitumiwa na meli zinazoenda na zinazotoka eneo la Aegea, Asia Ndogo, Siria, na Misri.

      Kwa kuwa kulikuwa na upepo mkali kwenye eneo la kusini la Ugiriki, ilikuwa hatari kusafiri kwa meli. Ndio sababu manahodha walipendelea kutia nanga katika mojawapo ya bandari hizo mbili za Korintho, kisha kusafirisha shehena yao juu ya nchi kavu, na kuipakia tena katika bandari ya pili. Ikiwa meli ilikuwa nyepesi ingeweza kuvushwa kupitia barabara ya pekee kutoka bandari moja hadi bandari nyingine. Kwa sababu ya mahali lilipokuwa, jiji hilo lilitawala biashara za meli pande zote mbili za bahari, mashariki na magharibi, na pia za nchi kavu, kaskazini na kusini. Mbali na utajiri, jiji la Korintho lilikuwa na ufisadi mwingi ambao hupatikana katika bandari nyingi.

      Katika siku za Paulo, Korintho lilikuwa jiji kuu la mkoa wa Roma ya Akaya na kituo muhimu cha kuendesha shughuli za serikali. Kulikuwa na dini nyingi sana katika jiji hilo. Kwa mfano kulikuwa na hekalu la kumwabudu Maliki wa Roma, maeneo mengi ya ibada kwa ajili ya kuabudu miungu ya Wagiriki na Wamisri, na pia sinagogi la Wayahudi.​—Mdo. 18:4.

      Mashindano ya mbio yaliyofanywa Isthmia kila baada ya miaka miwili yalikuwa ya pili kwa umaarufu, Michezo ya Olimpiki ikiwa katika nafasi ya kwanza. Huenda mtume Paulo alikuwa Korintho mashindano ya mwaka wa 51 W.K. yalipokuwa yakiendelea. Kamusi moja ya Biblia inasema, “haishangazi kwamba Paulo alitumia mfano wa mashindano ya mbio kwa mara ya kwanza katika barua yake kwa Wakorintho.”​—1 Kor. 9:24-27.

      “Kazi Yao Ilikuwa ya Kutengeneza Mahema” (Mdo. 18:1-4)

      4, 5. (a) Paulo aliishi wapi alipokuwa Korintho, naye alifanya kazi gani ya kimwili? (b) Huenda Paulo alijifunzaje kazi ya kutengeneza mahema?

      4 Baada ya kufika Korintho, Paulo alikutana na wenzi wa ndoa wakarimu—Akila mwenye asili ya Kiyahudi, na mke wake, Prisila, au Priska. Akila na Prisila walihamia Korintho kwa sababu Maliki Klaudio aliagiza “Wayahudi wote waondoke Roma.” (Mdo. 18:1, 2) Akila na Prisila walimkaribisha Paulo nyumbani kwao na pia katika kazi yao ya kimwili. Tunasoma: “Kwa sababu [Paulo alifanya] kazi ileile, akakaa nyumbani kwao na kufanya kazi pamoja nao, kwa maana kazi yao ilikuwa ya kutengeneza mahema.” (Mdo. 18:3) Kipindi chote cha huduma yake jijini Korintho, Paulo alikaa nyumbani kwa wenzi hao wenye fadhili na wakarimu. Inawezekana Paulo aliandika baadhi ya barua ambazo baadaye zilikuwa sehemu ya Biblia alipokuwa akiishi nyumbani kwa Akila na Prisila.b

      5 Paulo, mtu aliyeelimishwa “miguuni pa Gamalieli,” angewezaje kuwa na ujuzi wa kutengeneza mahema? (Mdo. 22:3) Inaonekana kwamba Wayahudi wa karne ya kwanza hawakuona aibu kuwafundisha watoto wao kazi fulani ya mikono, ingawa watoto hao walipata elimu ya ziada pia. Kwa kuwa alikuwa mwenyeji wa Tarso ya Kilikia, eneo lililojulikana sana kwa sababu ya kitambaa kinachoitwa cilicium kilichotumiwa kutengeneza mahema, inaelekea Paulo alijifunza kazi hiyo alipokuwa kijana. Kazi hiyo ya kutengeneza mahema ilifanywaje? Huenda ilitia ndani kufuma kitambaa cha hema au kukata na kushona kitambaa hicho kigumu ili kutengeneza mahema. Bila shaka, kazi hiyo ilikuwa ngumu sana.

      6, 7. (a) Paulo aliionaje kazi ya kutengeneza mahema, na ni nini kinachoonyesha kwamba Akila na Prisila walikuwa na maoni hayohayo? (b) Wakristo leo wanafuataje mfano wa Paulo, Akila, na Prisila?

      6 Paulo hakuiona kazi ya kutengeneza mahema kuwa kazi muhimu sana maishani mwake. Alifanya kazi hiyo ili kujitegemeza na lengo lake lilikuwa kuhubiri habari njema “bila gharama.” (2 Kor. 11:7) Akila na Prisila waliionaje kazi yao ya kimwili? Kwa kuwa walikuwa Wakristo, bila shaka walikuwa na maoni kama ya Paulo. Isitoshe, Paulo alipoondoka Korintho mwaka wa 52 W.K., Akila na Prisila waliacha biashara yao na kusafiri pamoja na Paulo hadi Efeso, ambapo nyumba yao ilitumiwa kwa ajili ya mikutano ya kutaniko. (1 Kor. 16:19) Baadaye, walirudi Roma, halafu wakaenda tena Efeso. Wenzi hao wenye bidii walitanguliza Ufalme na walijitoa kwa hiari ili kuwatumikia wengine. Kwa sababu hiyo “makutaniko yote ya mataifa” yaliwashukuru.​—Rom. 16:3-5; 2 Tim. 4:19.

      7 Leo, Wakristo hufuata mfano wa Paulo, Akila, na Prisila. Wahubiri wenye bidii leo hufanya yote wawezayo ili ‘wasimpe yeyote kati yetu mzigo wenye gharama.’ (1 The. 2:9) Mapainia wengi wanatuwekea mfano mzuri kwa kufanya kazi kwa siku kadhaa katika juma au miezi fulani katika mwaka ili waweze kulipia gharama zao za maisha. Hata hivyo, wanatanguliza kazi ya upainia. Kama Akila na Prisila, watumishi wengi wa Yehova huonyesha ukarimu kwa kuwakaribisha nyumbani kwao waangalizi wa mzunguko. ‘Wakaribishaji wageni’ wanajua kwamba kuwa wakarimu hutia moyo na kujenga.​—Rom. 12:13.

      BARUA ZENYE KUTIA MOYO ZILIZOONGOZWA NA ROHO YA MUNGU

      Katika kipindi cha miezi 18 ambacho mtume Paulo alikaa Korintho, mwaka wa 50-52 hivi W.K., aliandika barua mbili zilizokuja kuwa sehemu ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo—Barua ya Kwanza na ya Pili kwa Wathesalonike. Huenda pia aliandika barua yake kwa Wagalatia wakati huohuo au muda mfupi baadaye.

      Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike ndiyo maandishi ya kwanza ambayo Paulo aliongozwa na roho kuyaandika. Paulo alitembelea Thesalonike mwaka wa 50 hivi W.K., alipokuwa katika safari yake ya pili ya kuhubiri. Muda mfupi baadaye, kutaniko jipya lililokuwa limeanzishwa lilikumbwa na upinzani uliowalazimu Paulo na Sila kuondoka jijini humo. (Mdo. 17:1-10, 13) Akihangaikia hali ya kutaniko hilo jipya, Paulo alijaribu mara mbili kurudi huko lakini “Shetani aliifunga njia [yake].” Hivyo Paulo akamtuma Timotheo awafariji na kuwaimarisha akina ndugu. Mwishoni mwa mwaka wa 50 hivi W.K., Timotheo aliungana na Paulo jijini Korintho na kumweleza habari njema kuhusu kutaniko la Thesalonike. Kisha, Paulo akawaandikia barua ya kwanza.​—1 The. 2:17–3:7.

      Huenda Barua ya Pili kwa Wathesalonike iliandikwa muda mfupi baada ya ile ya kwanza, mnamo mwaka wa 51 hivi W.K. Katika barua zote mbili, Timotheo na Silvano (anayeitwa Sila katika kitabu cha Matendo) walituma salamu zao pamoja na Paulo, na hakuna uthibitisho wowote unaoonyesha kwamba watu hao watatu walikuwa pamoja tena baada ya wakati huo ambao Paulo alikuwa akikaa Korintho. (Mdo. 18:5, 18; 1 The. 1:1; 2 The. 1:1) Kwa nini Paulo aliwaandikia Wathesalonike barua ya pili? Inaonekana alipata habari zaidi kuhusu kutaniko, labda kupitia mtu aliyemtuma apeleke barua ya kwanza. Habari alizopata zilimchochea Paulo kuwapongeza akina ndugu kwa upendo na uvumilivu wao na pia kurekebisha maoni ya baadhi ya Wathesalonike ya kwamba kuwapo kwa Bwana kumefika.​—2 The. 1:3-12; 2:1, 2.

      Kutokana na barua ya Paulo kwa Wagalatia inaonekana alikuwa amewatembelea angalau mara mbili kabla ya kuwaandikia. Mwaka wa 47-48 W.K., Paulo na Barnaba walitembelea Antiokia ya Pisidia, Ikoniamu, Listra, na Derbe, majiji yaliyokuwa katika jimbo la Roma lililoitwa Galatia. Mwaka wa 49 W.K., Paulo alirudi katika eneo hilo akiwa na Sila. (Mdo. 13:1–14:23; 16:1-6) Paulo aliandika barua hii kwa sababu ndugu wa uwongo, waliotokea mara tu baada ya ziara ya Paulo, walikuwa wakifundisha kwamba Wakristo wanapaswa kutahiriwa na kushika Sheria ya Musa. Bila shaka, Paulo aliwaandikia Wagalatia mara tu aliposikia kuhusu mafundisho hayo ya uongo. Huenda aliandika barua hiyo akiwa Korintho, lakini inawezekana pia aliiandika akiwa Efeso, muda mfupi alipofika huko akiwa safarini kurudi Antiokia ya Siria au akitoka Antiokia kwenyewe.​—Mdo. 18:18-23.

      “Wakorintho Wengi . . . Wakaanza Kuamini” (Mdo. 18:5-8)

      8, 9. Paulo alifanya nini alipopingwa na Wayahudi aliowahubiria, naye alienda kuhubiri wapi?

      8 Paulo aliiona kazi ya kimwili kuwa njia ya kumtegemeza katika huduma yake. Hilo lilionekana wazi Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia wakiwa na zawadi nyingi. (2 Kor. 11:9) Mara moja, Paulo “akaanza kushughulika sana na lile neno [“alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri,” Biblia Habari Njema].” (Mdo. 18:5) Hata hivyo, Wayahudi aliowahubiria walimpinga. Alijiondolea lawama kwa sababu walikataa ujumbe unaookoa uhai kumhusu Kristo. Paulo alikung’uta mavazi yake na kuwaambia Wayahudi hao waliompinga: “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe. Mimi ni safi. Kuanzia sasa nitaenda kwa watu wa mataifa.”​—Mdo. 18:6; Eze. 3:18, 19.

      9 Paulo angehubiri wapi? Mtu anayeitwa Titio Yusto, huenda alikuwa Myahudi mgeuzwa imani na ambaye nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi, alimkaribisha Paulo. Hivyo, Paulo akaacha kuhubiri kwenye Sinagogi na kuendelea kuhubiri akiwa kwenye nyumba ya Yusto. (Mdo. 18:7) Paulo aliendelea kuishi katika nyumba ya Akila na Prisila alipokuwa Korintho, lakini aliitumia nyumba ya Yusto kwa ajili ya huduma yake.

      10. Ni nini kinachoonyesha kwamba Paulo hakuazimia kuwahubiria tu watu wa mataifa?

      10 Paulo aliposema angeenda kwa watu wa mataifa, je alimaanisha hangewahubiria kabisa Wayahudi na Wayahudi wageuzwa imani, kutia ndani wale waliokubali ujumbe wake? Hapana. Kwa mfano, “Krispo, ofisa msimamizi wa sinagogi akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake.” Inaonekana kwamba wengi kati ya wale waliokuwa wakienda katika sinagogi walijiunga na Krispo, kwa sababu Biblia inasema: “Wakorintho wengi waliosikia wakaanza kuamini na kubatizwa.” (Mdo. 18:8) Basi, kutaniko jipya la Kikristo lililoanzishwa jijini Korintho likaanza kukutanika katika nyumba ya Titio Yusto. Ikiwa masimulizi ya kitabu cha Matendo yanafuata mtindo wa Luka—yaani, yanafuatana kulingana na wakati yalipotukia—basi hilo linamaanisha kwamba Wayahudi hao au Wayahudi wageuzwa imani walikuwa Wakristo baada ya Paulo kukung’uta mavazi yake. Ikiwa ndivyo, basi ni wazi kwamba Paulo alikuwa tayari kubadilika kulingana na hali.

      11. Mashahidi wa Yehova leo wanafuata mfano wa Paulo jinsi gani wanapowahubiria watu walio katika dini zinazodai kuwa za Kikristo?

      11 Leo watu katika nchi nyingi wanadai kwamba wao ni washiriki wa kanisa fulani linalomfuata Kristo. Na makanisa hayo yana uvutano mkubwa katika maisha yao. Wamishonari wa dini hizo wamepata wafuasi wengi. Watu wanaodai kuwa Wakristo mara nyingi huwa watumwa wa desturi, kama walivyokuwa Wayahudi wa karne ya kwanza jijini Korintho. Hata hivyo, kama Paulo, sisi hujitahidi kuwasaidia watu hao waelewe mambo wanayosoma katika Biblia zao. Hata wanapotupinga, au viongozi wao wa kidini wanapotunyanyasa, hatukati tamaa. Huenda kuna wapole kadhaa miongoni mwa watu wenye “bidii kwa ajili ya Mungu, lakini si kulingana na ujuzi sahihi.” Tunahitaji kuwatafuta wapole hao.​—Rom. 10:2.

      “Nina Watu Wengi Katika Jiji Hili” (Mdo. 18:9-17)

      12. Paulo alihakikishiwa nini katika maono?

      12 Ikiwa Paulo alikuwa na mashaka yoyote kuhusu kuendelea na huduma yake jijini Korintho, mashaka hayo yaliisha Bwana Yesu alipomtokea katika maono ya usiku na kumwambia: “Usiogope, bali endelea kusema na usinyamaze, kwa sababu niko pamoja nawe na hakuna mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana nina watu wengi katika jiji hili.” (Mdo. 18:9, 10) Hayo yalikuwa maono yenye kutia moyo sana! Bwana mwenyewe alimhakikishia Paulo kwamba angelindwa ili asipatwe na madhara na kuna wengi wanaostahili katika jiji hilo. Paulo alitendaje baada ya kuona maono hayo? Tunasoma hivi: “Akakaa huko kwa mwaka mmoja na miezi sita, akifundisha neno la Mungu kati yao.”​—Mdo. 18:11.

      13. Huenda Paulo alikumbuka tukio gani alipokaribia kiti cha hukumu, lakini kwa nini hali yake ingekuwa tofauti?

      13 Baada ya kukaa Korintho mwaka mmoja hivi, Paulo alipata uthibitisho zaidi kwamba Bwana angemsaidia. “Wayahudi wakaungana, wakamshambulia Paulo na kumpeleka kwenye kiti cha hukumu,” kinachoitwa beʹma. (Mdo. 18:12) Baadhi ya watu husema kwamba kiti hicho cha hukumu kilikuwa juu ya jukwaa lililokuwa karibu na eneo la katikati ya soko la Korintho. Kiti hicho kilitengenezwa kwa marumaru za rangi ya bluu na nyeupe zilizochongwa vizuri. Eneo la mbele la beʹma lilikuwa kubwa na umati mkubwa wa watu ungeweza kukusanyika hapo. Uvumbuzi wa vitu vya kale unaonyesha kwamba huenda kiti hicho cha hukumu kilikuwa karibu sana na sinagogi, na ikiwa ndivyo, basi hakikuwa mbali na nyumba ya Yusto. Paulo alipokaribia beʹma, huenda alikumbuka jinsi Stefano, ambaye huitwa mfia-imani wa kwanza, alivyopigwa mawe. Paulo, ambaye wakati huo aliitwa Sauli, aliunga mkono “kuuawa kwa Stefano.” (Mdo. 8:1) Je, sasa jambo hilohilo lingempata Paulo? Hapana, kwa kuwa Yesu alimwahidi hivi: “Hakuna mtu atakayekushambulia ili kukudhuru.”​—Mdo. 18:10.

      Galio akitupilia mbali kesi ya Paulo mbele ya watu wenye hasira wanaomshtaki. Askari Waroma wakijaribu kutuliza umati wa wanaume wenye hasira.

      “Ndipo akawafukuza kutoka mbele ya kiti cha hukumu.”—Matendo 18:16

      14, 15. (a) Wayahudi walimshtaki Paulo kwa kosa gani, na kwa nini Galio aliitupilia mbali kesi hiyo? (b) Ni nini kilichompata Sosthene, na huenda baadaye alifanya nini?

      14 Ni nini kilichotokea Paulo alipofika kwenye kiti cha hukumu? Hakimu aliyekuwa ameketi juu ya kiti hicho alikuwa liwali Akaya, anayeitwa Galio—kaka ya mwanafalsafa Mroma Seneka. Wayahudi wakamshtaki Paulo: “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kwa njia iliyo kinyume cha sheria.” (Mdo. 18:13) Walidai kwamba Paulo anageuza imani ya watu kinyume cha sheria. Hata hivyo, Galio akaona kwamba Paulo hajafanya “kosa” lolote na hana hatia ya “uhalifu mkubwa.” (Mdo. 18:14) Galio hakuwa na nia yoyote ya kujiingiza katika mizozo ya Wayahudi. Hata kabla ya Paulo kusema neno lolote ili kujitetea, Galio akaitupilia mbali kesi hiyo! Washtaki hao wakakasirika sana. Walimalizia hasira yao kwa Sosthene, ofisa msimamizi wa sinagogi, ambaye huenda alichukua nafasi ya Krispo. Walimkamata Sosthene “na kuanza kumpiga mbele ya kiti cha hukumu.”​—Mdo. 18:17.

      15 Kwa nini Galio hakuuzuia umati usimpige Sosthene? Huenda Galio alifikiri kwamba Sosthene ndiye aliyeuchochea umati huo dhidi ya Paulo na kwa hiyo anapata haki yake. Iwe ndivyo ilivyokuwa au la, kulikuwa na matokeo mazuri. Katika barua yake ya kwanza kwa kutaniko la Korintho, iliyoandikwa miaka kadhaa baadaye, Paulo alimtaja mtu fulani anayeitwa Sosthene akimwita ndugu. (1 Kor. 1:1, 2) Je, huyo ni Sosthene yuleyule aliyepigwa jijini Korintho? Ikiwa ndiye, kisa hicho kilimsaidia Sosthene kuukubali Ukristo.

      16. Maneno ya Bwana, “endelea kusema na usinyamaze, kwa sababu niko pamoja nawe,” yanatutiaje moyo katika huduma yetu?

      16 Kumbuka kwamba baada ya Wayahudi kumpinga Paulo, Bwana Yesu alimwimarisha na kumwambia, “Usiogope, bali endelea kusema na usinyamaze, kwa sababu niko pamoja nawe.” (Mdo. 18:9, 10) Tusisahau kamwe maneno hayo, hasa watu wanapokataa ujumbe wetu. Usisahau kamwe kwamba Yehova anasoma mioyo na huwavuta watu wanyofu kwake. (1 Sam. 16:7; Yoh. 6:44) Jambo hilo linatutia moyo tuendelee kuwa na bidii katika huduma! Kila mwaka, mamia ya maelfu ya watu hubatizwa, hilo linamaanisha kila siku mamia ya watu hubatizwa. Wale wanaotii amri ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ Yesu anawahakikishia hivi: “Mimi nipo pamoja nanyi sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”​—Mt. 28:19, 20.

      “Yehova Akipenda” (Mdo. 18:18-22)

      17, 18. Huenda Paulo alitafakari nini alipokuwa njiani kuelekea Efeso?

      17 Hatujui ikiwa maoni ya Galio kuelekea watu waliomshtaki Paulo yaliliwezesha kutaniko hilo changa la Kikristo jijini Korintho kukaa kwa amani kwa muda. Hata hivyo, Paulo alikaa “siku kadhaa” kabla ya kuwaaga ndugu zake wa Korintho. Mwaka wa 52 W.K., alipanga kusafiri hadi Siria kutoka bandari ya Kenkrea, kilomita 11 hivi upande wa mashariki wa Korintho. Hata hivyo, kabla ya kuondoka Kenkrea, Paulo “alikuwa amekata nywele zake . . . , kwa sababu alikuwa ameweka nadhiri.”c (Mdo. 18:18) Baadaye, aliwachukua Akila na Prisila na kusafiri katika bahari ya Aegea hadi Efeso katika Asia Ndogo.

      18 Paulo aliposafiri kutoka Kenkrea, inawezekana alikuwa akitafakari maisha yake jijini Korintho. Alikuwa na kumbukumbu kadhaa nzuri na sababu nyingi za kuridhika. Huduma yake ya miezi 18 jijini humo ilikuwa na matokeo mazuri. Kutaniko la kwanza jijini Korintho lilianzishwa, na lilikutana katika nyumba ya Yusto. Yusto, Krispo na familia yake, na wengine wengi walikuwa waamini. Paulo aliwapenda sana waamini hao wapya, kwa sababu aliwasaidia kuwa Wakristo. Baadaye aliwaandikia barua na kuwaita barua za pendekezo zilizoandikwa moyoni mwake. Sisi pia huwa na uhusiano wa karibu na watu tunaowasaidia kukubali ibada ya kweli. Ni jambo lenye kuridhisha sana kuona ‘barua hizo za pendekezo!’​—2 Kor. 3:1-3.

      19, 20. Paulo alifanya nini alipofika Efeso, na tunaweza kujifunza nini kutoka kwake kuhusu kufuatia malengo ya kiroho?

      19 Alipofika Efeso, Paulo alianza kazi yake mara moja. “Akaingia ndani ya sinagogi na kujadiliana na Wayahudi.” (Mdo. 18:19) Pindi hiyo, Paulo alikaa Efeso kwa muda mfupi tu. Ingawa aliombwa akae muda mrefu, “hakukubali.” Alipokuwa akiwaaga, aliwaambia Waefeso: “Nitarudi kwenu tena, Yehova akipenda.” (Mdo. 18:20, 21) Paulo alijua kwamba bado kulikuwa na kazi kubwa ya kuhubiri jijini Efeso. Alipanga kurudi, hata hivyo aliamua kuacha mambo mikononi mwa Yehova. Je, huo si mfano mzuri tunaoweza kuiga? Tunapofuatia malengo ya kiroho, lazima tuchukue hatua zinazohitajika. Hata hivyo, lazima sikuzote tutegemee mwongozo wa Yehova na kujitahidi kutenda kupatana na mapenzi yake.​—Yak. 4:15.

      20 Akiwaacha Akila na Prisila, Paulo alisafiri baharini hadi Kaisaria. Huenda ‘alipanda’ kwenda Yerusalemu na kulisalimu kutaniko lililokuwa huko. (Mdo. 18:22) Kisha Paulo akarudi nyumbani kwake—Antiokia ya Siria. Alikuwa ameimaliza kwa mafanikio safari yake ya pili ya umishonari. Ni nini kinachomsubiri katika safari yake ya mwisho ya umishonari?

      NADHIRI YA PAULO

      Andiko la Matendo 18:18 linasema kwamba alipokuwa Kenkrea, Paulo “alikuwa amekata nywele zake . . . , kwa sababu alikuwa ameweka nadhiri.” Hiyo ilikuwa nadhiri ya aina gani?

      Kwa kawaida, nadhiri ni ahadi nzito ambayo mtu huweka kwa Mungu kwa hiari, akiahidi kufanya jambo fulani, kutoa toleo, au kuingia katika utumishi fulani. Watu fulani husema kwamba Paulo alikata nywele zake ili kutimiza nadhiri ya Wanadhiri. Hata hivyo, kulingana na Maandiko, baada ya Mnadhiri kumaliza kipindi cha utumishi fulani wa pekee kwa Yehova, alipaswa kunyoa kichwa chake “kwenye mlango wa hema la mkutano.” Inaonekana takwa hilo lingeweza kutekelezwa Yerusalemu wala si Kenkrea.​—Hes. 6:5, 18.

      Masimulizi ya kitabu cha Matendo hayataji Paulo aliweka nadhiri yake wakati gani. Huenda hata aliiweka kabla ya kuwa Mkristo. Pia, masimulizi hayo hayataji iwapo Paulo alimwomba Yehova jambo lolote hususa. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema kwamba huenda Paulo alikata nywele zake ili “kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake, uliomwezesha kutimiza huduma yake huko Korintho.”

      a Ona Sanduku lenye kichwa “Korintho—Jiji Lenye Bahari Mbili.”

      b Ona Sanduku lenye kichwa “Barua Zenye Kutia Moyo Zilizoongozwa na Roho ya Mungu.”

      c Ona sanduku lenye kichwa “Nadhiri ya Paulo.”

  • “Endelea Kusema na Usinyamaze”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • SURA YA 19

      “Endelea Kusema na Usinyamaze”

      Paulo ajitegemeza kimwili na kutanguliza huduma

      Matendo 18:1-22

      1-3. Mtume Paulo ameenda Korintho kufanya nini, na anakabili changamoto gani?

      NI MWISHONI mwa mwaka wa 50 W.K. Mtume Paulo yuko Korintho, jiji tajiri lenye wakaaji wengi Wagiriki, Waroma, na Wayahudi.a Paulo hakwenda kununua wala kuuza bidhaa au kutafuta kazi ya kimwili. Ameenda hapo ili kufanya kazi muhimu zaidi—kutoa ushahidi kuhusu Ufalme wa Mungu. Hata hivyo, Paulo anahitaji mahali pa kuishi, na hataki kuwa mzigo kwa wengine. Hataki mtu yeyote afikiri kwamba anajiruzuku kutokana na neno la Mungu. Atafanya nini?

      2 Paulo ana ujuzi wa kutengeneza mahema. Kazi ya kutengeneza mahema si rahisi, hata hivyo, yuko tayari kufanya kazi kwa mikono yake ili ajitegemeze. Je, atapata kazi katika jiji hili lenye shughuli nyingi? Je, atapata mahali pazuri pa kuishi? Ingawa ana mahitaji mengi, Paulo hasahau kamwe kazi yake kuu, kazi ya kuhubiri.

      3 Paulo alikaa Korintho kwa muda fulani, naye alipata matokeo mazuri katika huduma yake. Ni mambo gani tunayoweza kujifunza kutokana na utendaji mbalimbali wa Paulo alipokuwa Korintho ambayo yanaweza kutusaidia kutoa ushahidi kamili kuhusu Ufalme wa Mungu katika eneo letu?

      KORINTHO—JIJI LENYE BAHARI MBILI

      Jiji la kale la Korintho lilikuwa kwenye kipande cha eneo kinachounganisha nchi ya Ugiriki na rasi ya kusini inayoitwa Peloponesia. Sehemu nyembamba zaidi ya eneo hilo ilikuwa na upana usiozidi kilomita sita, na kwa sababu hiyo Korintho lilikuwa na bandari mbili. Bandari ya Lekayo, ilikuwa kwenye Ghuba ya Korintho, na ilitumiwa na meli zilizokuwa zikielekea magharibi hadi Hispania, Italia, na Sisili. Na bandari ya Kenkrea, iliyokuwa katika Ghuba ya Saroni, ilitumiwa na meli zinazoenda na zinazotoka eneo la Aegea, Asia Ndogo, Siria, na Misri.

      Kwa kuwa kulikuwa na upepo mkali kwenye eneo la kusini la Ugiriki, ilikuwa hatari kusafiri kwa meli. Ndio sababu manahodha walipendelea kutia nanga katika mojawapo ya bandari hizo mbili za Korintho, kisha kusafirisha shehena yao juu ya nchi kavu, na kuipakia tena katika bandari ya pili. Ikiwa meli ilikuwa nyepesi ingeweza kuvushwa kupitia barabara ya pekee kutoka bandari moja hadi bandari nyingine. Kwa sababu ya mahali lilipokuwa, jiji hilo lilitawala biashara za meli pande zote mbili za bahari, mashariki na magharibi, na pia za nchi kavu, kaskazini na kusini. Mbali na utajiri, jiji la Korintho lilikuwa na ufisadi mwingi ambao hupatikana katika bandari nyingi.

      Katika siku za Paulo, Korintho lilikuwa jiji kuu la mkoa wa Roma ya Akaya na kituo muhimu cha kuendesha shughuli za serikali. Kulikuwa na dini nyingi sana katika jiji hilo. Kwa mfano kulikuwa na hekalu la kumwabudu Maliki wa Roma, maeneo mengi ya ibada kwa ajili ya kuabudu miungu ya Wagiriki na Wamisri, na pia sinagogi la Wayahudi.​—Mdo. 18:4.

      Mashindano ya mbio yaliyofanywa Isthmia kila baada ya miaka miwili yalikuwa ya pili kwa umaarufu, Michezo ya Olimpiki ikiwa katika nafasi ya kwanza. Huenda mtume Paulo alikuwa Korintho mashindano ya mwaka wa 51 W.K. yalipokuwa yakiendelea. Kamusi moja ya Biblia inasema, “haishangazi kwamba Paulo alitumia mfano wa mashindano ya mbio kwa mara ya kwanza katika barua yake kwa Wakorintho.”​—1 Kor. 9:24-27.

      “Kazi Yao Ilikuwa ya Kutengeneza Mahema” (Mdo. 18:1-4)

      4, 5. (a) Paulo aliishi wapi alipokuwa Korintho, naye alifanya kazi gani ya kimwili? (b) Huenda Paulo alijifunzaje kazi ya kutengeneza mahema?

      4 Baada ya kufika Korintho, Paulo alikutana na wenzi wa ndoa wakarimu—Akila mwenye asili ya Kiyahudi, na mke wake, Prisila, au Priska. Akila na Prisila walihamia Korintho kwa sababu Maliki Klaudio aliagiza “Wayahudi wote waondoke Roma.” (Mdo. 18:1, 2) Akila na Prisila walimkaribisha Paulo nyumbani kwao na pia katika kazi yao ya kimwili. Tunasoma: “Kwa sababu [Paulo alifanya] kazi ileile, akakaa nyumbani kwao na kufanya kazi pamoja nao, kwa maana kazi yao ilikuwa ya kutengeneza mahema.” (Mdo. 18:3) Kipindi chote cha huduma yake jijini Korintho, Paulo alikaa nyumbani kwa wenzi hao wenye fadhili na wakarimu. Inawezekana Paulo aliandika baadhi ya barua ambazo baadaye zilikuwa sehemu ya Biblia alipokuwa akiishi nyumbani kwa Akila na Prisila.b

      5 Paulo, mtu aliyeelimishwa “miguuni pa Gamalieli,” angewezaje kuwa na ujuzi wa kutengeneza mahema? (Mdo. 22:3) Inaonekana kwamba Wayahudi wa karne ya kwanza hawakuona aibu kuwafundisha watoto wao kazi fulani ya mikono, ingawa watoto hao walipata elimu ya ziada pia. Kwa kuwa alikuwa mwenyeji wa Tarso ya Kilikia, eneo lililojulikana sana kwa sababu ya kitambaa kinachoitwa cilicium kilichotumiwa kutengeneza mahema, inaelekea Paulo alijifunza kazi hiyo alipokuwa kijana. Kazi hiyo ya kutengeneza mahema ilifanywaje? Huenda ilitia ndani kufuma kitambaa cha hema au kukata na kushona kitambaa hicho kigumu ili kutengeneza mahema. Bila shaka, kazi hiyo ilikuwa ngumu sana.

      6, 7. (a) Paulo aliionaje kazi ya kutengeneza mahema, na ni nini kinachoonyesha kwamba Akila na Prisila walikuwa na maoni hayohayo? (b) Wakristo leo wanafuataje mfano wa Paulo, Akila, na Prisila?

      6 Paulo hakuiona kazi ya kutengeneza mahema kuwa kazi muhimu sana maishani mwake. Alifanya kazi hiyo ili kujitegemeza na lengo lake lilikuwa kuhubiri habari njema “bila gharama.” (2 Kor. 11:7) Akila na Prisila waliionaje kazi yao ya kimwili? Kwa kuwa walikuwa Wakristo, bila shaka walikuwa na maoni kama ya Paulo. Isitoshe, Paulo alipoondoka Korintho mwaka wa 52 W.K., Akila na Prisila waliacha biashara yao na kusafiri pamoja na Paulo hadi Efeso, ambapo nyumba yao ilitumiwa kwa ajili ya mikutano ya kutaniko. (1 Kor. 16:19) Baadaye, walirudi Roma, halafu wakaenda tena Efeso. Wenzi hao wenye bidii walitanguliza Ufalme na walijitoa kwa hiari ili kuwatumikia wengine. Kwa sababu hiyo “makutaniko yote ya mataifa” yaliwashukuru.​—Rom. 16:3-5; 2 Tim. 4:19.

      7 Leo, Wakristo hufuata mfano wa Paulo, Akila, na Prisila. Wahubiri wenye bidii leo hufanya yote wawezayo ili ‘wasimpe yeyote kati yetu mzigo wenye gharama.’ (1 The. 2:9) Mapainia wengi wanatuwekea mfano mzuri kwa kufanya kazi kwa siku kadhaa katika juma au miezi fulani katika mwaka ili waweze kulipia gharama zao za maisha. Hata hivyo, wanatanguliza kazi ya upainia. Kama Akila na Prisila, watumishi wengi wa Yehova huonyesha ukarimu kwa kuwakaribisha nyumbani kwao waangalizi wa mzunguko. ‘Wakaribishaji wageni’ wanajua kwamba kuwa wakarimu hutia moyo na kujenga.​—Rom. 12:13.

      BARUA ZENYE KUTIA MOYO ZILIZOONGOZWA NA ROHO YA MUNGU

      Katika kipindi cha miezi 18 ambacho mtume Paulo alikaa Korintho, mwaka wa 50-52 hivi W.K., aliandika barua mbili zilizokuja kuwa sehemu ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo—Barua ya Kwanza na ya Pili kwa Wathesalonike. Huenda pia aliandika barua yake kwa Wagalatia wakati huohuo au muda mfupi baadaye.

      Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike ndiyo maandishi ya kwanza ambayo Paulo aliongozwa na roho kuyaandika. Paulo alitembelea Thesalonike mwaka wa 50 hivi W.K., alipokuwa katika safari yake ya pili ya kuhubiri. Muda mfupi baadaye, kutaniko jipya lililokuwa limeanzishwa lilikumbwa na upinzani uliowalazimu Paulo na Sila kuondoka jijini humo. (Mdo. 17:1-10, 13) Akihangaikia hali ya kutaniko hilo jipya, Paulo alijaribu mara mbili kurudi huko lakini “Shetani aliifunga njia [yake].” Hivyo Paulo akamtuma Timotheo awafariji na kuwaimarisha akina ndugu. Mwishoni mwa mwaka wa 50 hivi W.K., Timotheo aliungana na Paulo jijini Korintho na kumweleza habari njema kuhusu kutaniko la Thesalonike. Kisha, Paulo akawaandikia barua ya kwanza.​—1 The. 2:17–3:7.

      Huenda Barua ya Pili kwa Wathesalonike iliandikwa muda mfupi baada ya ile ya kwanza, mnamo mwaka wa 51 hivi W.K. Katika barua zote mbili, Timotheo na Silvano (anayeitwa Sila katika kitabu cha Matendo) walituma salamu zao pamoja na Paulo, na hakuna uthibitisho wowote unaoonyesha kwamba watu hao watatu walikuwa pamoja tena baada ya wakati huo ambao Paulo alikuwa akikaa Korintho. (Mdo. 18:5, 18; 1 The. 1:1; 2 The. 1:1) Kwa nini Paulo aliwaandikia Wathesalonike barua ya pili? Inaonekana alipata habari zaidi kuhusu kutaniko, labda kupitia mtu aliyemtuma apeleke barua ya kwanza. Habari alizopata zilimchochea Paulo kuwapongeza akina ndugu kwa upendo na uvumilivu wao na pia kurekebisha maoni ya baadhi ya Wathesalonike ya kwamba kuwapo kwa Bwana kumefika.​—2 The. 1:3-12; 2:1, 2.

      Kutokana na barua ya Paulo kwa Wagalatia inaonekana alikuwa amewatembelea angalau mara mbili kabla ya kuwaandikia. Mwaka wa 47-48 W.K., Paulo na Barnaba walitembelea Antiokia ya Pisidia, Ikoniamu, Listra, na Derbe, majiji yaliyokuwa katika jimbo la Roma lililoitwa Galatia. Mwaka wa 49 W.K., Paulo alirudi katika eneo hilo akiwa na Sila. (Mdo. 13:1–14:23; 16:1-6) Paulo aliandika barua hii kwa sababu ndugu wa uwongo, waliotokea mara tu baada ya ziara ya Paulo, walikuwa wakifundisha kwamba Wakristo wanapaswa kutahiriwa na kushika Sheria ya Musa. Bila shaka, Paulo aliwaandikia Wagalatia mara tu aliposikia kuhusu mafundisho hayo ya uongo. Huenda aliandika barua hiyo akiwa Korintho, lakini inawezekana pia aliiandika akiwa Efeso, muda mfupi alipofika huko akiwa safarini kurudi Antiokia ya Siria au akitoka Antiokia kwenyewe.​—Mdo. 18:18-23.

      “Wakorintho Wengi . . . Wakaanza Kuamini” (Mdo. 18:5-8)

      8, 9. Paulo alifanya nini alipopingwa na Wayahudi aliowahubiria, naye alienda kuhubiri wapi?

      8 Paulo aliiona kazi ya kimwili kuwa njia ya kumtegemeza katika huduma yake. Hilo lilionekana wazi Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia wakiwa na zawadi nyingi. (2 Kor. 11:9) Mara moja, Paulo “akaanza kushughulika sana na lile neno [“alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri,” Biblia Habari Njema].” (Mdo. 18:5) Hata hivyo, Wayahudi aliowahubiria walimpinga. Alijiondolea lawama kwa sababu walikataa ujumbe unaookoa uhai kumhusu Kristo. Paulo alikung’uta mavazi yake na kuwaambia Wayahudi hao waliompinga: “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe. Mimi ni safi. Kuanzia sasa nitaenda kwa watu wa mataifa.”​—Mdo. 18:6; Eze. 3:18, 19.

      9 Paulo angehubiri wapi? Mtu anayeitwa Titio Yusto, huenda alikuwa Myahudi mgeuzwa imani na ambaye nyumba yake ilikuwa karibu na sinagogi, alimkaribisha Paulo. Hivyo, Paulo akaacha kuhubiri kwenye Sinagogi na kuendelea kuhubiri akiwa kwenye nyumba ya Yusto. (Mdo. 18:7) Paulo aliendelea kuishi katika nyumba ya Akila na Prisila alipokuwa Korintho, lakini aliitumia nyumba ya Yusto kwa ajili ya huduma yake.

      10. Ni nini kinachoonyesha kwamba Paulo hakuazimia kuwahubiria tu watu wa mataifa?

      10 Paulo aliposema angeenda kwa watu wa mataifa, je alimaanisha hangewahubiria kabisa Wayahudi na Wayahudi wageuzwa imani, kutia ndani wale waliokubali ujumbe wake? Hapana. Kwa mfano, “Krispo, ofisa msimamizi wa sinagogi akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake.” Inaonekana kwamba wengi kati ya wale waliokuwa wakienda katika sinagogi walijiunga na Krispo, kwa sababu Biblia inasema: “Wakorintho wengi waliosikia wakaanza kuamini na kubatizwa.” (Mdo. 18:8) Basi, kutaniko jipya la Kikristo lililoanzishwa jijini Korintho likaanza kukutanika katika nyumba ya Titio Yusto. Ikiwa masimulizi ya kitabu cha Matendo yanafuata mtindo wa Luka—yaani, yanafuatana kulingana na wakati yalipotukia—basi hilo linamaanisha kwamba Wayahudi hao au Wayahudi wageuzwa imani walikuwa Wakristo baada ya Paulo kukung’uta mavazi yake. Ikiwa ndivyo, basi ni wazi kwamba Paulo alikuwa tayari kubadilika kulingana na hali.

      11. Mashahidi wa Yehova leo wanafuata mfano wa Paulo jinsi gani wanapowahubiria watu walio katika dini zinazodai kuwa za Kikristo?

      11 Leo watu katika nchi nyingi wanadai kwamba wao ni washiriki wa kanisa fulani linalomfuata Kristo. Na makanisa hayo yana uvutano mkubwa katika maisha yao. Wamishonari wa dini hizo wamepata wafuasi wengi. Watu wanaodai kuwa Wakristo mara nyingi huwa watumwa wa desturi, kama walivyokuwa Wayahudi wa karne ya kwanza jijini Korintho. Hata hivyo, kama Paulo, sisi hujitahidi kuwasaidia watu hao waelewe mambo wanayosoma katika Biblia zao. Hata wanapotupinga, au viongozi wao wa kidini wanapotunyanyasa, hatukati tamaa. Huenda kuna wapole kadhaa miongoni mwa watu wenye “bidii kwa ajili ya Mungu, lakini si kulingana na ujuzi sahihi.” Tunahitaji kuwatafuta wapole hao.​—Rom. 10:2.

      “Nina Watu Wengi Katika Jiji Hili” (Mdo. 18:9-17)

      12. Paulo alihakikishiwa nini katika maono?

      12 Ikiwa Paulo alikuwa na mashaka yoyote kuhusu kuendelea na huduma yake jijini Korintho, mashaka hayo yaliisha Bwana Yesu alipomtokea katika maono ya usiku na kumwambia: “Usiogope, bali endelea kusema na usinyamaze, kwa sababu niko pamoja nawe na hakuna mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana nina watu wengi katika jiji hili.” (Mdo. 18:9, 10) Hayo yalikuwa maono yenye kutia moyo sana! Bwana mwenyewe alimhakikishia Paulo kwamba angelindwa ili asipatwe na madhara na kuna wengi wanaostahili katika jiji hilo. Paulo alitendaje baada ya kuona maono hayo? Tunasoma hivi: “Akakaa huko kwa mwaka mmoja na miezi sita, akifundisha neno la Mungu kati yao.”​—Mdo. 18:11.

      13. Huenda Paulo alikumbuka tukio gani alipokaribia kiti cha hukumu, lakini kwa nini hali yake ingekuwa tofauti?

      13 Baada ya kukaa Korintho mwaka mmoja hivi, Paulo alipata uthibitisho zaidi kwamba Bwana angemsaidia. “Wayahudi wakaungana, wakamshambulia Paulo na kumpeleka kwenye kiti cha hukumu,” kinachoitwa beʹma. (Mdo. 18:12) Baadhi ya watu husema kwamba kiti hicho cha hukumu kilikuwa juu ya jukwaa lililokuwa karibu na eneo la katikati ya soko la Korintho. Kiti hicho kilitengenezwa kwa marumaru za rangi ya bluu na nyeupe zilizochongwa vizuri. Eneo la mbele la beʹma lilikuwa kubwa na umati mkubwa wa watu ungeweza kukusanyika hapo. Uvumbuzi wa vitu vya kale unaonyesha kwamba huenda kiti hicho cha hukumu kilikuwa karibu sana na sinagogi, na ikiwa ndivyo, basi hakikuwa mbali na nyumba ya Yusto. Paulo alipokaribia beʹma, huenda alikumbuka jinsi Stefano, ambaye huitwa mfia-imani wa kwanza, alivyopigwa mawe. Paulo, ambaye wakati huo aliitwa Sauli, aliunga mkono “kuuawa kwa Stefano.” (Mdo. 8:1) Je, sasa jambo hilohilo lingempata Paulo? Hapana, kwa kuwa Yesu alimwahidi hivi: “Hakuna mtu atakayekushambulia ili kukudhuru.”​—Mdo. 18:10.

      Galio akitupilia mbali kesi ya Paulo mbele ya watu wenye hasira wanaomshtaki. Askari Waroma wakijaribu kutuliza umati wa wanaume wenye hasira.

      “Ndipo akawafukuza kutoka mbele ya kiti cha hukumu.”—Matendo 18:16

      14, 15. (a) Wayahudi walimshtaki Paulo kwa kosa gani, na kwa nini Galio aliitupilia mbali kesi hiyo? (b) Ni nini kilichompata Sosthene, na huenda baadaye alifanya nini?

      14 Ni nini kilichotokea Paulo alipofika kwenye kiti cha hukumu? Hakimu aliyekuwa ameketi juu ya kiti hicho alikuwa liwali Akaya, anayeitwa Galio—kaka ya mwanafalsafa Mroma Seneka. Wayahudi wakamshtaki Paulo: “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kwa njia iliyo kinyume cha sheria.” (Mdo. 18:13) Walidai kwamba Paulo anageuza imani ya watu kinyume cha sheria. Hata hivyo, Galio akaona kwamba Paulo hajafanya “kosa” lolote na hana hatia ya “uhalifu mkubwa.” (Mdo. 18:14) Galio hakuwa na nia yoyote ya kujiingiza katika mizozo ya Wayahudi. Hata kabla ya Paulo kusema neno lolote ili kujitetea, Galio akaitupilia mbali kesi hiyo! Washtaki hao wakakasirika sana. Walimalizia hasira yao kwa Sosthene, ofisa msimamizi wa sinagogi, ambaye huenda alichukua nafasi ya Krispo. Walimkamata Sosthene “na kuanza kumpiga mbele ya kiti cha hukumu.”​—Mdo. 18:17.

      15 Kwa nini Galio hakuuzuia umati usimpige Sosthene? Huenda Galio alifikiri kwamba Sosthene ndiye aliyeuchochea umati huo dhidi ya Paulo na kwa hiyo anapata haki yake. Iwe ndivyo ilivyokuwa au la, kulikuwa na matokeo mazuri. Katika barua yake ya kwanza kwa kutaniko la Korintho, iliyoandikwa miaka kadhaa baadaye, Paulo alimtaja mtu fulani anayeitwa Sosthene akimwita ndugu. (1 Kor. 1:1, 2) Je, huyo ni Sosthene yuleyule aliyepigwa jijini Korintho? Ikiwa ndiye, kisa hicho kilimsaidia Sosthene kuukubali Ukristo.

      16. Maneno ya Bwana, “endelea kusema na usinyamaze, kwa sababu niko pamoja nawe,” yanatutiaje moyo katika huduma yetu?

      16 Kumbuka kwamba baada ya Wayahudi kumpinga Paulo, Bwana Yesu alimwimarisha na kumwambia, “Usiogope, bali endelea kusema na usinyamaze, kwa sababu niko pamoja nawe.” (Mdo. 18:9, 10) Tusisahau kamwe maneno hayo, hasa watu wanapokataa ujumbe wetu. Usisahau kamwe kwamba Yehova anasoma mioyo na huwavuta watu wanyofu kwake. (1 Sam. 16:7; Yoh. 6:44) Jambo hilo linatutia moyo tuendelee kuwa na bidii katika huduma! Kila mwaka, mamia ya maelfu ya watu hubatizwa, hilo linamaanisha kila siku mamia ya watu hubatizwa. Wale wanaotii amri ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ Yesu anawahakikishia hivi: “Mimi nipo pamoja nanyi sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”​—Mt. 28:19, 20.

      “Yehova Akipenda” (Mdo. 18:18-22)

      17, 18. Huenda Paulo alitafakari nini alipokuwa njiani kuelekea Efeso?

      17 Hatujui ikiwa maoni ya Galio kuelekea watu waliomshtaki Paulo yaliliwezesha kutaniko hilo changa la Kikristo jijini Korintho kukaa kwa amani kwa muda. Hata hivyo, Paulo alikaa “siku kadhaa” kabla ya kuwaaga ndugu zake wa Korintho. Mwaka wa 52 W.K., alipanga kusafiri hadi Siria kutoka bandari ya Kenkrea, kilomita 11 hivi upande wa mashariki wa Korintho. Hata hivyo, kabla ya kuondoka Kenkrea, Paulo “alikuwa amekata nywele zake . . . , kwa sababu alikuwa ameweka nadhiri.”c (Mdo. 18:18) Baadaye, aliwachukua Akila na Prisila na kusafiri katika bahari ya Aegea hadi Efeso katika Asia Ndogo.

      18 Paulo aliposafiri kutoka Kenkrea, inawezekana alikuwa akitafakari maisha yake jijini Korintho. Alikuwa na kumbukumbu kadhaa nzuri na sababu nyingi za kuridhika. Huduma yake ya miezi 18 jijini humo ilikuwa na matokeo mazuri. Kutaniko la kwanza jijini Korintho lilianzishwa, na lilikutana katika nyumba ya Yusto. Yusto, Krispo na familia yake, na wengine wengi walikuwa waamini. Paulo aliwapenda sana waamini hao wapya, kwa sababu aliwasaidia kuwa Wakristo. Baadaye aliwaandikia barua na kuwaita barua za pendekezo zilizoandikwa moyoni mwake. Sisi pia huwa na uhusiano wa karibu na watu tunaowasaidia kukubali ibada ya kweli. Ni jambo lenye kuridhisha sana kuona ‘barua hizo za pendekezo!’​—2 Kor. 3:1-3.

      19, 20. Paulo alifanya nini alipofika Efeso, na tunaweza kujifunza nini kutoka kwake kuhusu kufuatia malengo ya kiroho?

      19 Alipofika Efeso, Paulo alianza kazi yake mara moja. “Akaingia ndani ya sinagogi na kujadiliana na Wayahudi.” (Mdo. 18:19) Pindi hiyo, Paulo alikaa Efeso kwa muda mfupi tu. Ingawa aliombwa akae muda mrefu, “hakukubali.” Alipokuwa akiwaaga, aliwaambia Waefeso: “Nitarudi kwenu tena, Yehova akipenda.” (Mdo. 18:20, 21) Paulo alijua kwamba bado kulikuwa na kazi kubwa ya kuhubiri jijini Efeso. Alipanga kurudi, hata hivyo aliamua kuacha mambo mikononi mwa Yehova. Je, huo si mfano mzuri tunaoweza kuiga? Tunapofuatia malengo ya kiroho, lazima tuchukue hatua zinazohitajika. Hata hivyo, lazima sikuzote tutegemee mwongozo wa Yehova na kujitahidi kutenda kupatana na mapenzi yake.​—Yak. 4:15.

      20 Akiwaacha Akila na Prisila, Paulo alisafiri baharini hadi Kaisaria. Huenda ‘alipanda’ kwenda Yerusalemu na kulisalimu kutaniko lililokuwa huko. (Mdo. 18:22) Kisha Paulo akarudi nyumbani kwake—Antiokia ya Siria. Alikuwa ameimaliza kwa mafanikio safari yake ya pili ya umishonari. Ni nini kinachomsubiri katika safari yake ya mwisho ya umishonari?

      NADHIRI YA PAULO

      Andiko la Matendo 18:18 linasema kwamba alipokuwa Kenkrea, Paulo “alikuwa amekata nywele zake . . . , kwa sababu alikuwa ameweka nadhiri.” Hiyo ilikuwa nadhiri ya aina gani?

      Kwa kawaida, nadhiri ni ahadi nzito ambayo mtu huweka kwa Mungu kwa hiari, akiahidi kufanya jambo fulani, kutoa toleo, au kuingia katika utumishi fulani. Watu fulani husema kwamba Paulo alikata nywele zake ili kutimiza nadhiri ya Wanadhiri. Hata hivyo, kulingana na Maandiko, baada ya Mnadhiri kumaliza kipindi cha utumishi fulani wa pekee kwa Yehova, alipaswa kunyoa kichwa chake “kwenye mlango wa hema la mkutano.” Inaonekana takwa hilo lingeweza kutekelezwa Yerusalemu wala si Kenkrea.​—Hes. 6:5, 18.

      Masimulizi ya kitabu cha Matendo hayataji Paulo aliweka nadhiri yake wakati gani. Huenda hata aliiweka kabla ya kuwa Mkristo. Pia, masimulizi hayo hayataji iwapo Paulo alimwomba Yehova jambo lolote hususa. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema kwamba huenda Paulo alikata nywele zake ili “kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake, uliomwezesha kutimiza huduma yake huko Korintho.”

      a Ona Sanduku lenye kichwa “Korintho—Jiji Lenye Bahari Mbili.”

      b Ona Sanduku lenye kichwa “Barua Zenye Kutia Moyo Zilizoongozwa na Roho ya Mungu.”

      c Ona sanduku lenye kichwa “Nadhiri ya Paulo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki