-
Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na KiuHuduma ya Ufalme—1998 | Februari
-
-
2 Kwa kuwa watu wengi wanahangaishwa na mambo ya kiafya, huenda ukaona mfikio huu kuwa wenye matokeo:
◼ “Wengi wanahangaishwa na gharama yenye kuongezeka ya utunzaji wa afya ulio bora. Labda umewaza kwa kiasi fulani kuhusu jambo hilo. [Ruhusu itikio.] Je, kuna utatuzi wa kudumu wa tatizo hili? [Ngojea itikio.] Hapa pana tazamio la ajabu sana.” Soma Ufunuo 22:1, 2. Kisha fungua kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye picha iliyo kwenye ukurasa wa 308-309, na utumie fungu la 22 kwenye ukurasa wa 311 kuieleza. Malizia kwa kusema: “Kichapo hiki huzungumzia kila mstari katika Ufunuo.” Mwenye nyumba akionyesha kupendezwa kikweli, toa kitabu hicho kwa mchango ulioagizwa. Fanya mipango ya kurudi.
-
-
Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na KiuHuduma ya Ufalme—1998 | Februari
-
-
4 Ikiwa habari ya sasa inayohusu kifo kisichotazamiwa imekuwa akilini mwa watu, unaweza kujaribu mfikio huu:
◼ “Huenda ukawa umesikia kuhusu [taja habari hiyo]. Maisha yafupishwapo kwa njia ya kuhuzunisha, wengi hujiuliza ni faraja gani iwezayo kutolewa familia za wahasiriwa. Wafikirije?” Ruhusu itikio. Kisha fungua ukurasa wa 299 katika kitabu Upeo wa Ufunuo, na uonyeshe mandhari ya ufufuo iliyotolewa kielezi. Endelea kwa kusema hivi: “Watu wengi hushangaa kupata kujua kwamba watu waadilifu na wasio waadilifu watarudishwa kwenye uhai katika Paradiso duniani. [Soma Matendo 24:15 kama ilivyonukuliwa katika fungu la 9 kwenye ukurasa wa 297, kisha utoe ufafanuzi unaopatikana katika fungu la 10.] Kitabu hiki huzungumzia mambo mengine mengi yenye kupendeza kuhusu kusudi la Mungu la wakati ujao. Ikiwa ungependa kujifunza mengi zaidi kulihusu, unaweza kuchukua nakala hii.” Fanya mipango ya kurudi, ukiangalia mapendezi na mahangaiko mahususi ya mtu huyo.
-
-
Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na KiuHuduma ya Ufalme—1998 | Februari
-
-
6 Ukipendelea utoaji uliofanywa sahili ukaziao trakti, labda waweza kusema hivi:
◼ “Ningependa kukuachia trakti hii yenye kichwa Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?” Mpe mwenye nyumba, na umwalike afuatane nawe unaposoma fungu la kwanza. Mruhusu ajibu swali lililotokezwa katika sentensi ya mwisho. Soma fungu la pili, kisha ufungue kwenye picha iliyo kwenye ukurasa wa 299 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Endelea kwa kusema: “Kitabu hiki hutoa mambo mengi zaidi kuhusu ufufuo na ahadi zile nyingine za ajabu za Biblia kwa wakati ujao. Ikiwa utakisoma, unaweza kubaki na nakala hii kwa mchango mdogo wa——.” Panga kufanya ziara ya kurudia.
-