-
MatangazoHuduma ya Ufalme—2005 | Desemba
-
-
Matangazo
◼ Desemba: Tutatoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Unaweza kutoa vitabu vingine kama vile kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani iwapo vinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Januari 2006: Kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi inayochujuka rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991 kinaweza kutolewa. Makutaniko ambayo hayana vitabu hivyo vya zamani akibani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu ikiwa kinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Februari: Tutatoa kitabu Mkaribie Yehova. Makutaniko ambayo hayana kitabu hiki yanaweza kutoa kitabu kingine cha zamani kinachopatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inaweza kutolewa pia. Machi: Toeni kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidini kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Mialiko ya Ukumbusho ya 2006 itatumwa hivi karibuni.
◼ Tungependa kuwajulisha kwamba Ukumbusho wa mwaka wa 2007 utakuwa Jumatatu, Aprili 2, baada ya jua kutua. Taarifa hii imetolewa mapema ili akina ndugu waweze kufanya mapatano ya kukodi majumba mengine mahali ambapo makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme. Wazee wanapaswa kufanya maagano pamoja na wasimamizi wa jumba watakalokodi ili kuhakikisha kwamba Ukumbusho unaadhimishwa kwa njia ya amani na kwa utaratibu bila kuvurugwa na utendaji mwingine katika jengo hilo.
◼ Kwa sababu Ukumbusho ni tukio muhimu, baraza la wazee linapaswa kumteua mzee anayestahili zaidi atoe hotuba ya Ukumbusho badala ya kupokezana zamu tu au kutumia ndugu yuleyule kila mwaka. Ikiwa kuna mzee mwenye uwezo ambaye ni mtiwa-mafuta, apewe mgawo huo.
◼ Vitabu na magazeti yote yaliyopo yahesabiwe Desemba 31, 2005 au haraka iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Hesabu hiyo ni kama ile inayofanywa kila mwezi na mratibu wa vitabu, na jumla ziandikwe kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Jumla ya idadi ya magazeti yaliyopo inaweza kupatikana kutoka kwa watumishi wa magazeti. Mwandishi wa kutaniko linaloratibu anapaswa kusimamia kazi hiyo. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi wa kutaniko linaloratibu watie sahihi fomu hiyo. Kila kutaniko linaloratibu litapokea nakala tatu za fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Tafadhali tumeni nakala ya kwanza kwa ofisi ya tawi kabla ya Januari 6. Wekeni nakala ya kaboni kwenye faili zenu. Nakala ya tatu inaweza kutumiwa ili kufanyia hesabu.
-
-
Shule Ambayo Hutusaidia Kutumia Mambo TunayojifunzaHuduma ya Ufalme—2005 | Desemba
-
-
Shule Ambayo Hutusaidia Kutumia Mambo Tunayojifunza
1 Tunapochunguza habari iliyoonyeshwa katika Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2006, tunapaswa kujitahidi kunufaika na mafundisho ya Biblia yatakayotolewa kwa kuyatumia katika utumishi wetu mtakatifu na katika maisha yetu ya kila siku. Tunaazimia kutumia mambo tunayojifunza.—Yoh. 13:17; Flp. 4:9.
2 Kutoa Maelezo: Ratiba ya mwaka huu inawapa wasikilizaji dakika moja zaidi ya kutoa maelezo katika mambo makuu ya Biblia. Hii inamaanisha kwamba ndugu aliyepewa mgawo wa kutoa mambo makuu anapaswa kuwa mwangalifu amalize sehemu yake kwa dakika tano badala ya dakika sita. Wale wanaotoa maelezo wanapaswa kuwa waangalifu pia wasipitishe wakati. Kwa kufikiria maelezo yake kimbele, yule anayetoa maelezo anaweza kutaja habari muhimu kwa sekunde 30 hivi. Kufanya hivyo kutawawezesha watu kumi hivi watoe maelezo katika ule muda wa dakika tano uliotengwa kwa kusudi hilo.
3 Hotuba Zinazofundisha: Mambo makuu ya Biblia na hotuba ya maagizo inapaswa kukazia jinsi habari hiyo inavyohusu huduma yetu na sehemu nyingine za maisha yetu ya kila siku. Msemaji hapaswi tu kuwachochea wasikilizaji wake watende. Anapaswa kuonyesha waziwazi hatua inayopaswa kuchukuliwa, jinsi inavyoweza kuchukuliwa, na kuonyesha faida za kufanya hivyo. Anaweza kusema, “Andiko hili linatoa mwongozo huu,” au “Tunaweza kutumia mistari hii kwa njia hii katika huduma.” Wazee na watumishi wa huduma wanaofahamu hali za kwao wanapaswa kujitahidi kuonyesha kihususa jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa.
4 Kutaja mifano iliyo katika Biblia kunaweza kuwa na matokeo sana katika kuonyesha jinsi mambo tunayojifunza yanavyoweza kutumiwa. Baada ya kutaja mfano fulani katika Biblia, msemaji anaweza kusema, “Huenda wewe pia ukajikuta katika hali kama hiyo.” Anapaswa kuhakikisha kwamba mfano wowote wa Biblia unapatana na muktadha, Biblia nzima, na pia habari ambayo imechapishwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”—Mt. 24:45.
5 Hekima ni uwezo wa kutumia ujuzi na uelewaji kwa mafanikio. “Hekima ndilo jambo kuu.” (Met. 4:7) Tunapoendelea kujipatia hekima kupitia mambo tunayojifunza katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, na tuboreshe pia uwezo wetu wa kuwapa wengine hekima.
-