Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Serikali pia iliongoza mambo hivi kwamba Hakimu Harland B. Howe, kutoka Vermont, ambaye John Lord O’Brian alijua alikubaliana na maoni yake katika mambo kama hayo, angekuwa mwamuzi wa kesi katika Mahakama ya Wilaya ya Marekani kwa Wilaya ya Mashariki ya New York. Kesi ilianza Juni 5, washtaki wakiwa Isaac R. Oeland na Charles J. Buchner wa Katoliki ya Roma. Wakati kesi ilipokuwa ikiendelea, kama vile Ndugu Rutherford alivyoona, mapadri Wakatoliki walishauriana mara kwa mara na Buchner na Oeland.

      Kadiri kesi ilivyoendelea, ilionyeshwa kwamba maofisa wa Sosaiti na watungaji wa kile kitabu hawakuwa na madhumuni ya kuingilia shughuli za vita za nchi. Ushahidi uliotolewa wakati wa mashtaka ulionyesha kwamba mipango kwa ajili ya kuandikwa kwa kitabu hicho—kwa kweli, uandishi wa sehemu kubwa ya kitabu hicho—ulikuwa umefanywa kabla ya Marekani kutangaza vita (Aprili 6, 1917) na kwamba maafikiano ya kwanza ya kukichapa yalikuwa yametiwa sahihi kabla ya Marekani kupitisha sheria (mnamo Juni 15) ambayo ilisemwa walikuwa wamekiuka.

      Mashtaka yalikazia nyongeza kwenye kitabu hicho iliyofanywa wakati wa Aprili na Juni wa 1917, katika shughuli za kutayarisha nakala na kusoma zile zilizokamilishwa. Hiyo ilitia ndani nukuu kutoka kwa John Haynes Holmes, kasisi aliyekuwa amejulisha kwa nguvu kwamba vita ilikuwa kukiuka Ukristo. Kama ilivyoonyeshwa na mmojawapo mawakili watetezi, maelezo hayo ya kasisi, yaliyochapwa katika kitabu chenye kichwa A Statement to My People on the Eve of War, kilikuwa bado kikiuzwa katika Marekani wakati wa kesi hiyo. Wala kasisi huyo wala mchapaji wacho hawakushtakiwa. Lakini Wanafunzi wa Biblia waliorejezea hotuba yake ndio walioshtakiwa kwa mambo yaliyosemwa ndani yacho.

      Kitabu The Finished Mystery hakikuwaambia watu wa ulimwengu kwamba hawakuwa na haki ya kushiriki vitani. Lakini, katika kueleza unabii, kilinukuu madondoo kutoka matoleo ya The Watch Tower la 1915 ili kuonyesha kutopatana kwa makasisi waliodai kuwa wahudumu wa Kristo lakini walikuwa wakitenda wakiwa wajumbe wa kuandikisha majeshi ya mataifa yaliyo vitani.

      Ilipofahamika kwamba serikali ilipinga kitabu hicho, Ndugu Rutherford alikuwa amepeleka telegramu mara hiyo kwa mchapaji ili aache kukitokeza, na wakati uleule, mwakilishi wa Sosaiti alikuwa ametumwa kwenye idara ya upelelezi ya Jeshi la Marekani ili kujua sababu ya wao kukipinga. Ilipojulikana kwamba kwa sababu ya vita iliyokuwa ikiendelea, kurasa 247-253 za kitabu hicho zilionwa kuwa zisizofaa, Sosaiti ilielekeza kwamba kurasa hizo ziondolewe katika nakala zote za kitabu hicho kabla ya umma kupewa. Na wakati serikali ilipojulisha mawakili wa wilaya kwamba kugawanywa kwacho zaidi kungekuwa ni kukiuka Sheria ya Ujasusi (ingawa serikali ilikataa kutoa maoni kwa Sosaiti juu ya kitabu hicho kikiwa kimebadilishwa), Sosaiti ilielekeza kwamba kugawanywa kote kwa kitabu hicho kwa umma kukomeshwe.

      Kwa Nini Hukumu Kali Jinsi Hiyo?

      Kujapokuwa na yote hayo, katika Juni 20, 1918, wasaidizi wa hakimu walifanya uamuzi na wakampata kila mshtakiwa kuwa na kosa kwa kila shtaka. Siku iliyofuata, sabab kati yao walihukumiwa vifungo vinne vya miaka 20 kila moja, vinavyotumika pamoja. Julai 10, yule wa nanec alihukumiwa vipindi vinne vyenye kutumika pamoja vya miaka 10. Hukumu hiyo ilikuwa kali jinsi gani? Katika barua kwa mkuu wa sheria katika Machi 12, 1919, rais wa Marekani Woodrow Wilson alikiri kwamba “vifungo hivyo kwa wazi vinapita kiasi.” Kwa kweli, yule mtu aliyefyatua risasi katika Sarajevo ambazo zilimwua maliki mwana-mfalme wa Milki ya Austria na Hungaria—jambo lililochochea matukio yaliyoingiza mataifa katika Vita ya Ulimwengu 1—hakuwa amepata hukumu kali jinsi hiyo. Hukumu yake ilikuwa miaka 20 gerezani—si vifungo vinne vya miaka 20, kama ilivyokuwa kwa Wanafunzi wa Biblia!

      Ni nini kilichochea kuwekwa kwa vifungo hivyo vikali vya Wanafunzi wa Biblia? Hakimu Harland B. Howe alijulisha: “Kwa maoni ya Mahakama, propaganda ya kidini ambayo washtakiwa hawa wametetea kwa bidii na kuieneza kotekote katika taifa na miongoni mwa mataifa rafiki, ni hatari kubwa zaidi ya kikosi kimoja cha Jeshi la Ujerumani. . . . Mtu anayehubiri dini mara nyingi huwa na uvutano mwingi, na ikiwa ni mnyoofu, yeye ni mwenye matokeo hata zaidi. Hilo linazidisha badala ya kupunguza kosa walilofanya. Kwa hiyo, likiwa jambo lifaalo zaidi kufanyia watu kama hao, Mahakama imekata kauli kwamba hukumu lazima iwe kali.” Hata hivyo, inastahili kuangaliwa pia kwamba kabla ya kupitisha hukumu, Hakimu Howe alisema kwamba taarifa zilizotolewa na mawakili wa washtakiwa zilikuwa zimetia shuku na kutendea isivyofaa si maofisa wa sheria wa serikali tu bali pia “wahudumu wote wa kidini kotekote nchini.”

      Baada ya uamuzi huo, rufani ilikatwa mara hiyo kwa mahakama ya mzunguko ya rufani ya Marekani. Lakini Hakimu Howe alikataa kuwaachilia kwa dhamana wakisubiri kusikizwa kwa rufani hiyo,d na katika Julai 4, kabla ya rufani ya tatu iliyokuwa ya mwisho ya kupata dhamana kusikizwa, ndugu saba wa kwanza walihamishwa upesi wakapelekwa kwenye gereza la kitaifa la Atlanta, Georgia. Baada ya hapo, ilidhihirishwa kwamba kulikuwa na makosa 130 ya kimahakama katika hukumu hiyo yenye kupendelea upande mmoja sana. Kazi ya miezi mingi ilifanywa ili kutayarisha karatasi zilizotakikana katika kusikizwa kwa rufani. Wakati uo huo, vita ilikwisha. Mnamo Februari 19, 1919, ndugu wanane walio gerezani walipeleka rufani ili wahurumiwe rasmi na rais wa Marekani, Woodrow Wilson. Barua nyinginezo zilizohimiza kuachiliwa kwa ndugu hao zilipelekwa na wananchi wengi kwa mkuu wa sheria mpya. Kisha, mnamo Machi 1, 1919, katika kujibu maulizo ya mkuu wa sheria, Hakimu Howe alipendekeza “kubadilishwa mara hiyo” kwa hukumu hiyo. Ingawa hilo lingepunguza hukumu, pia lingethibitisha kosa la washtakiwa. Kabla ya hilo kufanywa, mawakili wa akina ndugu walimpelekea wakili mkuu wa Marekani agizo la mahakama lililoleta kesi hiyo mbele ya mahakama ya rufani.

      Miezi tisa baada ya Rutherford na washiriki wake kuhukumiwa—na vita ikiwa imekwisha—Machi 21, 1919, mahakama ya rufani iliagiza washtakiwa wote wanane wapate dhamana, na Machi 26, waliachiliwa katika Brooklyn kwa dhamana ya dola 10,000 kila mmoja. Katika Mei 14, 1919, mahakama ya mzunguko ya Marekani ya rufani katika New York ilikata kauli: “Washtakiwa katika kesi hii hawakupewa hukumu ya kiasi na isiyopendelea upande wowote ambayo walistahili kupewa, na kwa sababu hiyo hukumu hiyo imebatilishwa.” Kesi hiyo iliahirishwa ili ifanywe upya. Hata hivyo, Mei 5, 1920, baada ya washtakiwa kuja mahakamani, baada ya kupewa samansi, wakili wa serikali katika mahakama ya wazi katika Brooklyn, alitangaza mara tano kuondolewa kwa mashtaka.e Kwa nini? Kama ilivyofunuliwa na barua zilizohifadhiwa katika Jumba la Hati za Kitaifa la Marekani, Idara ya Sheria ilihofu kwamba ikiwa masuala hayo yangepelekwa mbele ya wasaidizi wa hakimu wasiopendelea upande wowote, huku harara ya vita ikiwa imekwisha, wangeshindwa kesi hiyo. Wakili wa Marekani aitwaye L. W. Ross alisema katika barua kwa mkuu wa sheria: “Ninafikiri ingekuwa afadhali, kwa uhusiano wetu na umma, ikiwa kwa hiari yetu wenyewe” tungesema kwamba kesi imefungwa.

      Siku iyo hiyo, Mei 5, 1920, shtaka lile jingine lililokuwa limefanywa katika Mei 1918 dhidi ya J. F. Rutherford na wanne kati ya washirika wake lilifutiliwa mbali pia.

  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • b Joseph F. Rutherford, msimamizi wa Watch Tower Society; William E. Van Amburgh, katibu-mweka-hazina wa Sosaiti; Robert J. Martin, meneja wa ofisi; Frederick H. Robison, mshiriki wa halmashauri ya uhariri wa The Watch Tower; A. Hugh Macmillan, mkurugenzi wa Sosaiti; George H. Fisher na Clayton J. Woodworth, watungaji wa The Finished Mystery.

      c Giovanni DeCecca, aliyefanya kazi katika Idara ya Italia katika ofisi ya Watch Tower Society.

  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 651]

      Wakati wa kuhukumiwa hapa kwa washiriki wa wafanyakazi wa makao makuu ya Sosaiti, fikira nyingi zilielekezwa kwenye kitabu “The Finished Mystery”

      Mahakama kuu na posta, Brooklyn, N.Y.

      [Picha katika ukurasa wa 653]

      Wahukumiwa kwa kifungo kikubwa zaidi ya kile cha muuaji aliyepiga risasi na kuanzisha Vita ya Ulimwengu 1. Kutoka kushoto kwenda kulia: W. E. Van Amburgh, J. F. Rutherford, A. H. Macmillan, R. J. Martin, F. H. Robison, C. J. Woodworth, G. H. Fisher, G. DeCecca

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki