Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakati wa Kunena”—Lini?
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 1
    • Mwongozo mwingine wa Biblia unaonekana kwenye Walawi 5:1, NW: “Basi ikitukia kwamba nafsi anafanya dhambi kwa kuwa amesikia kulaani kwa peupe naye ni shahidi au ameliona hilo au amejua habari zalo, kama haripoti hilo, hapo ni lazima ajibu kwa kosa lake.” Huku “kulaani kwa peupe” hakukuwa kusema machafu juu ya mambo matakatifu wala hakukuwa kukufuru. Bali, mara nyingi kulitukia wakati mtu fulani aliyekuwa amekosewa alipodai kwamba watu wo wote wanaoweza kuwa mashahidi wamsaidie kupata haki, na wakati huo yeye akiwa anatoa-toa laana—inaelekea kutoka kwa Yehova—juu ya mtu yule aliyekuwa amemkosea, ambaye labda hakuwa ametambulika. Hiyo ilikuwa namna ya kuweka wengine chini ya kiapo. Mashahidi wo wote wa kosa lile wangejua ni nani alikuwa ametendwa jambo lisilo la haki na wangekuwa na daraka la kujitokeza kuthibitisha hatia hiyo. Ama sivyo, wao wangelazimika ‘kujibu kwa kosa lao’ mbele za Yehova.b

      Amri hiyo kutoka kwa Kiwango Kikubwa Zaidi cha mamlaka katika ulimwengu wote iliweka daraka juu ya kila Mwisraeli la kuripoti kwa waamuzi kosa lo lote zito aliloona ili jambo hilo liweze kushughulikiwa. Ingawa Wakristo hawana wajibu unaowashurutisha kabisa kuwa chini ya Sheria ya Musa, kanuni zayo zingali zikitumika katika kundi la Kikristo. Kwa sababu hiyo, huenda zikawako nyakati ambapo Mkristo ana wajibu wa kupeleka jambo likafikiriwe na wazee. Ni kweli, katika nchi nyingi ni kinyume cha sheria kufunulia watu wasioruhusiwa na mamlaka jambo lililopatikana katika maandishi ya faragha. Lakini baada ya kufikiria jambo lile kwa sala, ikiwa Mkristo anahisi kwamba anaelekeana na hali ambapo sheria ya Mungu inamtaka aripoti jambo analojua yajapokuwako madai ya mamlaka zilizo ndogo zaidi, basi hilo ni daraka analolikubali mbele za Yehova. Kuna nyakati ambapo Mkristo ‘lazima atii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.’—Matendo 5:29, NW.

      Ingawa viapo au ahadi nzito-nzito hazipasi kamwe kuchukuliwa ki-hivi-hivi tu, huenda zikawako nyakati ambapo ahadi zinazotakwa na wanadamu zinapopingana na takwa la kwamba tujitolee kwa Mungu wetu peke yake tu. Wakati mtu anapotenda dhambi nzito, anakuwa kama matokeo, ni kama amekuja chini ya ‘laana ya peupe’ kutoka kwa Yule aliyekosewa, Yehova Mungu. (Kumbukumbu 27:26; Mithali 3:33) Wote wanaokuwa sehemu ya kundi la Kikristo wanajiweka wenyewe chini ya “kiapo” cha kutunza kundi likiwa safi, kwa yale wanayotenda kibinafsi na pia kwa jinsi wanavyosaidia wengine wabaki wakiwa safi.

  • “Wakati wa Kunena”—Lini?
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 1
    • b Katika kichapo chao Commentary on the Old Testament, Keil na Delitzsch wanasema kwamba mtu angekuwa mwenye hatia ya kosa au dhambi ikiwa ‘alijua uhalifu wa mwingine, awe alikuwa ameuona, au alikuwa amekuja kuujua kwa uhakika kwa njia nyingine yo yote, na hivyo akastahili kuonekana mahakamani akiwa shahidi wa kushtakiwa kwa mhalifu, lakini hakujali kufanya hivyo, na hakusema jambo alilokuwa ameona au kujua, wakati alipokisikia kiapisho kizito cha mwamuzi kwenye uchunguzi wa hadharani juu ya uhalifu ule, ambao kupitia huo watu wote waliopo, waliojua habari yo yote juu ya jambo hilo, walihimizwa wajitokeze kuwa mashahidi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki