-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
6. (a) Maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi gani yenye kufariji? (b) Maono hayo pia yalitoa onyo gani? (Tazama maelezo ya chini.)
6 Maji yanayoleta uhai. Katika maono ya Ezekieli, mto uliingia kwenye Bahari ya Chumvi, na kuponya sehemu kubwa ya bahari hiyo. Ona kwamba maji hayo yalitokeza samaki wengi wa aina mbalimbali kama samaki walio katika Bahari Kuu, yaani, Bahari ya Mediterania. Pia, kulikuwa na biashara kubwa ya uvuvi kwenye ufuo wa Bahari ya Chumvi katika miji miwili ambayo haikuwa imekaribiana sana. Malaika alisema: “Mahali ambapo kijito hicho kinapita, kila kitu kitaishi.” Je, hilo linamaanisha kwamba maji yanayotoka katika nyumba ya Yehova yalifika kila mahali katika Bahari ya Chumvi? Hapana. Malaika alieleza kwamba kulikuwa na sehemu zenye matope ambazo hazikufikiwa na maji yanayoleta uhai. Sehemu hizo ‘zingebaki zikiwa sehemu za chumvi.’b (Eze. 47:8-11) Basi maono hayo ya kinabii yalitoa ahadi yenye kufariji kwamba ibada safi ingewafanya watu wawe hai, na wasitawi. Lakini pia onyo hili lililotolewa: Si watu wote ambao wangekubali baraka za Yehova; wala si wote wangeponywa.
-
-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
b Baadhi ya wasomi wanaelewa kwamba maneno haya yanatoa wazo zuri, wanasema kwamba kuvuna chumvi ili kuitumia kuhifadhi vitu ni biashara ya muda mrefu yenye faida katika eneo la Bahari ya Chumvi. Hata hivyo, ona kwamba simulizi hilo lilisema waziwazi kwamba sehemu hizo zenye matope “hazitaponywa.” Zinabaki bila uhai, bila kuponywa, kwa sababu maji yanayoleta uhai kutoka katika nyumba ya Yehova hayafiki huko. Basi inaonekana kwamba katika simulizi hili chumvi ya maeneo hayo yenye matope inatajwa kwa njia isiyo nzuri.—Zab. 107:33, 34; Yer. 17:6.
c Kuhusiana na hilo, kumbuka mfano wa Yesu wa wavu wa kukokotwa. Samaki wengi wananaswa na wavu, lakini si wote walio “wazuri.” Samaki wasiofaa wanatupwa. Basi Yesu alionya kwamba huenda baadaye idadi kubwa ya watu wanaoingia katika tengenezo la Yehova wakakosa kuwa waaminifu.—Mt. 13:47-50; 2 Tim. 2:20, 21.
-
-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
b Baadhi ya wasomi wanaelewa kwamba maneno haya yanatoa wazo zuri, wanasema kwamba kuvuna chumvi ili kuitumia kuhifadhi vitu ni biashara ya muda mrefu yenye faida katika eneo la Bahari ya Chumvi. Hata hivyo, ona kwamba simulizi hilo lilisema waziwazi kwamba sehemu hizo zenye matope “hazitaponywa.” Zinabaki bila uhai, bila kuponywa, kwa sababu maji yanayoleta uhai kutoka katika nyumba ya Yehova hayafiki huko. Basi inaonekana kwamba katika simulizi hili chumvi ya maeneo hayo yenye matope inatajwa kwa njia isiyo nzuri.—Zab. 107:33, 34; Yer. 17:6.
c Kuhusiana na hilo, kumbuka mfano wa Yesu wa wavu wa kukokotwa. Samaki wengi wananaswa na wavu, lakini si wote walio “wazuri.” Samaki wasiofaa wanatupwa. Basi Yesu alionya kwamba huenda baadaye idadi kubwa ya watu wanaoingia katika tengenezo la Yehova wakakosa kuwa waaminifu.—Mt. 13:47-50; 2 Tim. 2:20, 21.
-
-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
12. (a) Tumeona jinsi gani ujumbe wa kweli ukiwaletea watu uhai na afya ya kiroho? (b) Maono hayo yanatupatia onyo gani leo? (Pia, tazama maelezo ya chini.)
12 Maji yanayoleta uhai. Ezekieli aliambiwa: “Mahali ambapo kijito hicho kinapita, kila kitu kitaishi.” Fikiria jinsi ambavyo ujumbe wa kweli umetiririka kwa wote ambao wamekuja katika nchi yetu ya kiroho iliyorudishwa. Kweli za Biblia zimegusa mioyo ya mamilioni ya watu na kuwafanya wawe hai na wenye afya kiroho. Lakini maono hayo pia yanatoa onyo muhimu kwamba si watu wote wanaoendelea kufuata kweli hizo. Kama sehemu zenye majimaji na matope katika Bahari ya Chumvi kwenye maono ya Ezekieli, mioyo fulani inakuwa migumu, haikubali kweli na inakataa kuifuata.c Tusiwe hivyo kamwe!—Soma Kumbukumbu la Torati 10:16-18.
-
-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
14, 15. (a) Tunapata somo gani kutokana na sehemu zenye matope ambazo hazikuponywa katika maono ya Ezekieli? (b) Leo tunafaidikaje kutokana na maono ya Ezekieli kuhusu mto?
14 Wakati huohuo, tunajifunza somo kutokana na maeneo hayo yenye matope yasiyoweza kuponywa. Hatungependa kamwe kuzuia baraka za Yehova kutiririka kwenye maisha yetu. Lingekuwa jambo hatari kukataa kuponywa, kama ilivyo kwa wengi katika ulimwengu huu mgonjwa. (Mt. 13:15) Kinyume chake, tunafurahia na kufaidika kutokana na mto wa baraka. Tunapokunywa kwa bidii maji safi ya kweli za Neno la Mungu, tunapowahubiria wengine kweli hizo, tunapopokea mwongozo wenye upendo, faraja, na msaada kutoka kwa wazee waliozoezwa na mtumwa mwaminifu, tunaweza kukumbuka mto wa maono ya Ezekieli. Mto huo unaendeleza uhai na kuponya popote unapoenda!
-