-
Unaweza Kumpata Ndugu YakoMnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 15
-
-
5, 6. Kulingana na muktadha, andiko la Mathayo 18:15 linarejezea dhambi za aina gani, na ni nini kinachoonyesha jambo hilo?
5 Shauri la Yesu hasa lilihusu mambo mazito zaidi. Yesu alisema: “Ndugu yako akifanya dhambi.” Kwa ujumla, “dhambi” inaweza kuwa kosa lolote au kasoro yoyote. (Ayubu 2:10; Mithali 21:4; Yakobo 4:17) Lakini, muktadha wadokeza kwamba ni lazima Yesu alimaanisha dhambi nzito. Ilikuwa nzito kiasi cha kwamba ingeweza kufanya mkosaji aonwe “kama vile mtu wa mataifa na kama mkusanya-kodi.” Maneno hayo yadokeza nini?
6 Wanafunzi wa Yesu waliosikia maneno hayo walijua kwamba Wayahudi wenzao hawakuwa na shughuli na watu wasio Wayahudi. (Yohana 4:9; 18:28; Matendo 10:28) Nao bila shaka waliwaepuka wakusanya-kodi, wanaume Wayahudi ambao waligeuka wakawa wanawadhulumu watu. Basi andiko la Mathayo 18:15-17 lilikuwa likirejezea hasa dhambi nzito, si kuumizwa au makosa madogo-madogo ya kibinafsi ambayo unaweza kusamehe tu na kusahau.—Mathayo 18:21, 22.a
-
-
Unaweza Kumpata Ndugu YakoMnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 15
-
-
a Kitabu Cyclopedia cha McClintock na Strong chasema: “Wakusanya-kodi wa Agano Jipya walionwa kuwa wahaini na waasi-imani, waliochafuliwa kwa kuchangamana sana na wapagani, na walio tayari kutumiwa na waonezi. Wao walionwa kuwa sehemu ya watenda-dhambi . . . Wakiwa wametengwa, watu wenye heshima waliwaepuka, na rafiki zao au waandamani wao wa pekee walikuwa watu ambao pia walikuwa wametengwa.”
-