Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mambo Haya Lazima Yatukie”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
    • Wayahudi wa Wakati Huo Wangetambua

      11. Yesu alisema nini kuhusu “kizazi hiki”?

      11 Wayahudi wengi walidhani kwamba mfumo wao wa ibada, uliotegemea hekalu, ungeendelea kwa muda mrefu. Lakini Yesu alisema hivi: “Jifunzeni jambo hili kutokana na mtini . . . Mara tu tawi lao changa likuapo kuwa jororo na kutoa majani, mwajua kwamba kiangazi kiko karibu. Hivyohivyo nyinyi pia, mwonapo mambo yote hayo, jueni kwamba yuko karibu milangoni. Kweli nawaambia nyinyi kwamba kizazi hiki hakitapitilia mbali kwa vyovyote mpaka mambo yote haya yatukie. Mbingu na dunia zitapitilia mbali, lakini maneno yangu hayatapitilia mbali kwa vyovyote.”—Mathayo 24:32-35.

      12, 13. Wanafunzi wangeelewaje fungu “kizazi hiki” kama Yesu alivyolirejezea?

      12 Katika miaka iliyotangulia mwaka wa 66 W.K., huenda Wakristo waliona sehemu nyingi za mwanzo-mwanzo za ishara yenye mambo mengi zikitimizwa—vita, njaa kuu, na hata kuhubiriwa kwa habari njema za Ufalme kotekote. (Matendo 11:28; Wakolosai 1:23) Hata hivyo, je, mwisho ungekuja lini? Yesu alimaanisha nini aliposema hivi: “Kizazi [Kigiriki, ge·ne·aʹ] hiki hakitapitilia mbali”? Mara nyingi Yesu aliuita umati wa Wayahudi wa wakati huo waliompinga, kutia ndani viongozi wa kidini, ‘kizazi kiovu, chenye uzinzi.’ (Mathayo 11:16; 12:39, 45; 16:4; 17:17; 23:36) Hivyo basi, wakati aliposema juu ya “kizazi hiki” akiwa kwenye Mlima wa Mizeituni, kwa wazi hakuwa akimaanisha jamii nzima ya Wayahudi kwa muda wote wa historia; wala hakumaanisha wafuasi wake, hata ingawa walikuwa “jamii iliyochaguliwa.” (1 Petro 2:9) Wala Yesu hakuwa akimaanisha kwamba “kizazi hiki” ni kipindi cha wakati.

      13 Badala yake, Yesu alimaanisha Wayahudi wenye upinzani wa wakati huo ambao wangeona utimizo wa ishara aliyotoa. Profesa Joel B. Green atoa hoja hii kuhusu kurejezewa kwa kifungu “kizazi hiki” katika Luka 21:32: “Katika Gospeli ya Tatu, fungu ‘kizazi hiki’ (na mafungu mengine yanayofanana nalo) tayari lamaanisha kikundi cha watu wanaopinga kusudi la Mungu. . . . [Fungu hilo larejezea] watu wanaopinga kwa dhati kusudi la kimungu.”b

      14. “Kizazi” hicho kilipatwa na mambo gani, lakini ni jinsi gani kulikuwako matokeo tofauti kwa Wakristo?

      14 Kizazi kiovu cha Wayahudi wenye kupinga ambao wangeweza kuona ishara ikitimizwa pia kingeona mwisho. (Mathayo 24:6, 13, 14) Nao waliuona! Jeshi la Waroma lilirudi mwaka wa 70 W.K. likiongozwa na Tito, mwana wa maliki Vespasian. Ni vigumu sana kuamini yale mateso yaliyowapata Wayahudi ambao walizuiliwa katika jiji hilo.c Flavio Yosefo, ambaye alijionea mambo hayo, anaripoti kwamba kufikia wakati ambapo Waroma walilibomoa jiji, karibu Wayahudi 1,100,000 walikuwa wamekufa na 100,000 hivi wakachukuliwa mateka, na upesi wengi wa mateka hao wakaangamia kwa njia yenye kutisha kutokana na njaa au katika mahali pa michezo pa Waroma. Kwa kweli, dhiki ya kipindi cha mwaka wa 66-70 W.K. ilikuwa ndiyo kubwa kupita zote ambayo Yerusalemu na mfumo wa mambo wa Kiyahudi ulikuwa umewahi kuona au ungewahi kuona. Matokeo yalikuwa tofauti kama nini kwa Wakristo waliotii onyo la kiunabii la Yesu na kuondoka Yerusalemu baada ya majeshi ya Waroma kuondoka mwaka wa 66 W.K.! Wakristo watiwa-mafuta ‘waliochaguliwa’ ‘waliokolewa,’ au wakasalimika, mwaka wa 70 W.K.—Mathayo 24:16, 22.

  • “Mambo Haya Lazima Yatukie”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
    • b Msomi Mwingereza G. R. Beasley-Murray asema hivi: “Fungu ‘kizazi hiki’ halipaswi kusababisha ugumu wowote kwa wafasiri. Ingawa ni kweli kwamba neno genea katika Kigiriki cha mapema lilimaanisha uzazi, uzao, na kwa hivyo jamii, . . . hilo mara nyingi lilitumiwa katika [Septuagint ya Kigiriki] kutafsiri neno la Kiebrania dôr, linalomaanisha umri, umri wa jamii ya kibinadamu, au kizazi katika maana ya watu walioishi wakati mmoja. . . . Katika maneno ya Yesu, neno hilo laonekana kuwa ladokeza maana mbili: kwa upande mmoja sikuzote hilo linamaanisha watu walioishi wakati mmoja naye, na kwa upande mwingine linamaanisha ule unaoeleweka kuwa uchambuzi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki