-
Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
-
-
13. Moto katika kielezi cha Paulo wawakilisha nini, na yawapasa Wakristo wote wajue nini?
13 Kuna moto ambao sisi sote hukabili maishani—majaribu ya imani yetu. (Yohana 15:20; Yakobo 1:2, 3) Kama vile tunavyohitaji kujua leo, Wakristo katika Korintho walihitaji kujua kwamba kila mtu tunayefundisha kweli atajaribiwa. Tukifundisha vibaya, huenda matokeo yakawa yenye kusikitisha. Paulo alionya: “Kazi ya yeyote ambayo ameijenga juu ya huo ikibaki, atapokea thawabu; kazi ya yeyote ikichomwa kabisa, atapata hasara, lakini yeye mwenyewe ataokolewa; lakini, ikiwa ndivyo, itakuwa ni kama kupitia moto.”c—1 Wakorintho 3:14, 15.
14. (a) Huenda wafanya-wanafunzi Wakristo ‘wakapataje hasara,’ hata hivyo huenda wao wakafikiaje wokovu kama kupitia moto? (b) Tunaweza kupunguzaje hatari ya kupata hasara?
14 Ni maneno yenye kuamsha fikira kama nini! Inaweza kuumiza sana kujitahidi kusaidia mtu awe mwanafunzi, kisha kumwona huyo mtu akishindwa na jaribu au mnyanyaso na hatimaye kuacha ile kweli. Paulo anakubaliana na jambo hilo anaposema kwamba sisi hupata hasara katika visa kama hivyo. Jambo hilo linaweza kuwa lenye kuumiza sana hivi kwamba wokovu wetu unafafanuliwa kuwa ‘kama unapitia moto’—kama mtu aliyepoteza kila kitu motoni, naye mwenyewe akaponea chupuchupu. Tunaweza kupunguzaje hatari ya kupata hasara upande wetu? Jenga kwa vifaa vidumuvyo! Tukiwafundisha wanafunzi wetu ili kuwafikia mioyo, tukiwachochea wathamini sifa za Kikristo kama vile hekima, ufahamu, kumhofu Yehova, na imani ya kweli, basi tunajenga kwa vifaa vyenye kudumu, visivyoweza kushika moto. (Zaburi 19:9, 10; Mithali 3:13-15; 1 Petro 1:6, 7) Wanaojipatia sifa hizo wataendelea kufanya mapenzi ya Mungu; nao wana tumaini hakika la kuendelea kuwa hai milele. (1 Yohana 2:17) Ingawa hivyo, tunaweza kutumiaje kielezi hicho cha Paulo kwa njia ifaayo? Fikiria vielelezo kadhaa.
-
-
Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
-
-
c Paulo alishuku kuokoka kwa “kazi” ya mjenzi wala si mjenzi mwenyewe. Tafsiri ya The New English Bible yatafsiri mstari huo hivi: “Jengo la mtu likistahimili, atapokea thawabu; likichomeka, atapata hasara; na bado ataponyoka na uhai wake, kama vile mtu aponyokavyo kutoka motoni.”
-