Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • 13. Moto katika kielezi cha Paulo wawakilisha nini, na yawapasa Wakristo wote wajue nini?

      13 Kuna moto ambao sisi sote hukabili maishani—majaribu ya imani yetu. (Yohana 15:20; Yakobo 1:2, 3) Kama vile tunavyohitaji kujua leo, Wakristo katika Korintho walihitaji kujua kwamba kila mtu tunayefundisha kweli atajaribiwa. Tukifundisha vibaya, huenda matokeo yakawa yenye kusikitisha. Paulo alionya: “Kazi ya yeyote ambayo ameijenga juu ya huo ikibaki, atapokea thawabu; kazi ya yeyote ikichomwa kabisa, atapata hasara, lakini yeye mwenyewe ataokolewa; lakini, ikiwa ndivyo, itakuwa ni kama kupitia moto.”c—1 Wakorintho 3:14, 15.

      14. (a) Huenda wafanya-wanafunzi Wakristo ‘wakapataje hasara,’ hata hivyo huenda wao wakafikiaje wokovu kama kupitia moto? (b) Tunaweza kupunguzaje hatari ya kupata hasara?

      14 Ni maneno yenye kuamsha fikira kama nini! Inaweza kuumiza sana kujitahidi kusaidia mtu awe mwanafunzi, kisha kumwona huyo mtu akishindwa na jaribu au mnyanyaso na hatimaye kuacha ile kweli. Paulo anakubaliana na jambo hilo anaposema kwamba sisi hupata hasara katika visa kama hivyo. Jambo hilo linaweza kuwa lenye kuumiza sana hivi kwamba wokovu wetu unafafanuliwa kuwa ‘kama unapitia moto’—kama mtu aliyepoteza kila kitu motoni, naye mwenyewe akaponea chupuchupu. Tunaweza kupunguzaje hatari ya kupata hasara upande wetu? Jenga kwa vifaa vidumuvyo! Tukiwafundisha wanafunzi wetu ili kuwafikia mioyo, tukiwachochea wathamini sifa za Kikristo kama vile hekima, ufahamu, kumhofu Yehova, na imani ya kweli, basi tunajenga kwa vifaa vyenye kudumu, visivyoweza kushika moto. (Zaburi 19:9, 10; Mithali 3:13-15; 1 Petro 1:6, 7) Wanaojipatia sifa hizo wataendelea kufanya mapenzi ya Mungu; nao wana tumaini hakika la kuendelea kuwa hai milele. (1 Yohana 2:17) Ingawa hivyo, tunaweza kutumiaje kielezi hicho cha Paulo kwa njia ifaayo? Fikiria vielelezo kadhaa.

  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • Ni Nani Mwenye Daraka?

      18. Mwanafunzi anapokataa mafundisho yenye mafaa, kwa nini si lazima kosa liwe la wale wanaojaribu kumfundisha na kumzoeza?

      18 Mazungumzo haya huzusha swali muhimu. Ikiwa mtu tunayejitahidi kumsaidia ataacha kweli, je, hilo lamaanisha kwamba sisi kama walimu tumeshindwa—kwamba tulijenga kwa vifaa duni? Si lazima iwe hivyo. Maneno ya Paulo yatukumbusha kwamba ni daraka kubwa kushiriki katika kujenga wanafunzi. Tunahitaji kufanya yote tuwezayo ili kujenga vizuri. Lakini Neno la Mungu halituambii tujitwike daraka hilo lote kisha tulemewe na hatia wakati wale tunaojaribu kusaidia wanapoacha ile kweli. Kuna mambo mengine yanayohusika mbali na kuwajibika kwetu wenyewe tukiwa wajenzi. Kwa kielelezo, ona yale Paulo asemayo kumhusu hata yule mwalimu ambaye amefanya vibaya katika kazi hii ya kujenga: “Atapata hasara, lakini yeye mwenyewe ataokolewa.” (1 Wakorintho 3:15) Ikiwa mwalimu huyo hatimaye aweza kupata wokovu—ilhali utu wa Kikristo aliojaribu kujenga katika mwanafunzi wake waonyeshwa kuwa ‘unachomwa’ katika jaribu kali—je, tutafikia mkataa gani? Bila shaka, Yehova humhesabia mwanafunzi kuwa ndiye kimsingi mwenye daraka kuhusiana na uamuzi wake mwenyewe wa kama atafuata njia ya uaminifu au hatafuata.

  • Je, Kazi Yako Itastahimili Moto?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Novemba 1
    • c Paulo alishuku kuokoka kwa “kazi” ya mjenzi wala si mjenzi mwenyewe. Tafsiri ya The New English Bible yatafsiri mstari huo hivi: “Jengo la mtu likistahimili, atapokea thawabu; likichomeka, atapata hasara; na bado ataponyoka na uhai wake, kama vile mtu aponyokavyo kutoka motoni.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki