Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 3/15 uku. 7
  • Muono-Ndani Juu ya Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Muono-Ndani Juu ya Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ishara ya Kuonya
  • “Serikali ya Ulimwengu”
  • Ushauri Mbaya
  • Matetemeko ya Ardhi Ni Ishara ya Ule Mwisho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Matetemeko ya Dunia—Taabu Juu ya Taabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Matetemeko ya Ardhi, Unabii wa Biblia, na Wewe
    Amkeni!—2002
  • Matetemeko Makubwa ya Ardhi—Biblia Ilitabiri Nini?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 3/15 uku. 7

Muono-Ndani Juu ya Habari

Ishara ya Kuonya

Desemba uliopita tetemeko la dunia la kiwango cha 6.9 kulingana na kipimo cha Richter liliharibu sana Armenia ya Urusi. Tetemeko hilo lililosemwa kuwa “moja la yaliyo mabaya zaidi katika historia ya Urusi” liliua watu kama 25,000 na kuacha 500,000 bila makao. Liliharibu theluthi mbili za Leninakan, jiji la pili kwa ukubwa katika Armenia, lenye wakaaji 290,000, na likaharibu kabisa Spitak, mji wenye wakaaji karibu 30,000. Mitaa mingi midogo-midogo ilitandazwa pia na tetemeko hilo. Waokokaji angalau 5,400 walivutwa na vikundi vya waokoaji kutoka kwenye mabomoko, na kulingana na wenye mamlaka wa Urusi, hesabu ya wajeruhiwa ilifika 13,000.

Ingawa wanasayansi wanajua kidogo visababishi vya msingi vinavyofanya ardhi itokeze matetemeko ya dunia, hawawezi kutabiri kwa usahihi yatatukia lini. Hata hivyo, uharibifu mkubwa unaotokezwa-tokezwa na matetemeko ya dunia katika karne hii haushangazi wanafunzi wa Biblia wanaojua vizuri “ishara” iliyotabiriwa na Yesu Kristo iwe alama ya “kuwapo” kwake kusikoonekana na “umalizio wa mfumo wa mambo.” Kwa nini? Kwa sababu hata ingawa Yesu hakueleza kisababishi cha matetemeko, alionya kwamba kungekuwako “matetemeko ya dunia mahali pamoja baada ya pengine,” yakiwa sehemu ya “ishara” hiyo yenye mambo mengi.​—Mathayo 24:3, 7, NW.

“Serikali ya Ulimwengu”

Njia pekee ya kuzuia usawa wa bahari usije kufurika na kuleta madhara kwa sababu ya halianga kufanyiza joto jingi mno kutokana na moshi unaojazana humo, na ya kuzuia misiba mingine ya kimazingira inayoendelea kutokea, ni kuwa na serikali moja ya ulimwengu, anasema Dakt. Kenneth Hare, mjiografia maarufu aliye mchunguzi stadi wa mabadiliko ya hali-hewa ya nchi. Wanadamu wanaangamiza sana maumbile, Hare akaonya. Sayari hii haitishwi na angamizi kuu la kinyukilia tu “bali na utumizi mbaya wa mazingira” pia, inaripoti Calgary Herald, nyusipepa moja ya Kanada. Hare anadai kwamba tani bilioni tatu za karboni hujazwa katika hewa ya anga kila mwaka na mioshi ya motakaa na viwanda. Machunguzi ya kompyuta yaonyesha kwamba hata uchumi ukisitawi kwa kiasi tu, karboni dayoksaidi ingekuwa maradufu kufikia mwaka 2075. “Tumefanyiza tatizo la duniani pote,” na mazingira yasiporekebishwa-rekebishwa duniani pote, “tutakuwa mashakani,” akasema Hare.

Analopendekeza Dakt. Hare ni jambo la kiakili kweli kweli. Hata hivyo, je! mwanadamu anaweza kweli kutumainia kwamba kuna wakati ataanzisha serikali ya duniani pote iweze kufanya mambo kama kurekebisha-rekebisha ukuzi wa uchumi, kutokeza vyanzo vya nishati visivyo na uchafuzi, na kusadikisha aina ya binadamu ifuate programu ya kutunza mazingira ulimwenguni pote?

Sivyo! Neno la Mungu linasema wazi hivi: “Njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” (Yeremia 10:23) Ijapokuwa hivyo, uwezo wa jambo hilo umo katika mikono ya Mungu. Mwana wake, Yesu Kristo, akiwa “Mwana-Mfalme wa Amani” atasimamia serikali ya ulimwengu itakayotawala kwa haki na uadilifu. Chini ya utawala wake wa kimbingu, aina ya binadamu haitahatarisha mazingira.​—Isaya 9:6, 7; 11:9; Danieli 2:44.

Ushauri Mbaya

Je! ni vibaya mtoto kutotii wazazi wake? Si kwa lazima, anadai Leon Kuczynski, profesa wa saikolojia ya ukuzi kwenye Chuo Kikuu cha Guelph katika Ontario, Kanada. Kwa uhakika, The Toronto Star inaripoti kwamba baada ya kuchunguza akina mama 70 na watoto wao, Kuczynski anaitikadi kwamba “mbinu ambazo mtoto hutumia ili kutotii wazazi wake ni za maana katika ukuzi wake wa kijamii.” Kulingana na makala hiyo, watoto wasipofanya wanaloambiwa, wazazi wasikate tamaa. Kwa sababu gani? Kuczynski anasema kwamba huo ni mwenendo wa kikawaida. Profesa huyo anahisi kwamba pia “kukataa kwa mtoto kutii wazazi wake kunaweza kuwa ishara ya kujitegemea na kukomaa.”

Kutotii kwa watoto wazazi wao si ishara ya kukomaa. Bali, Mfalme Sulemani mwenye hekima aliandika hivi: “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto.” (Mithali 22:15) Ingawa huenda watu fulani hata wakakata shauri kwamba kutotii kwa mtoto hutokeza matokeo mazuri, Neno la Mungu halikubali. Karne kadhaa zilizopita mtume Paulo aliandika hivi: “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.” (Wakolosai 3:20) Wazazi wenye hekima watategemea Yehova Mungu awe mamlaka yao ya kuzoeza watoto.​—Mithali 19:18; 29:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki