-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Mashahidi Wawili Wauawa
19. Kulingana na simulizi la Ufunuo, kunatukia nini wakati mashahidi wawili wanapomaliza kushuhudu kwao?
19 Tauni hii ilikuwa kali sana hivi kwamba baada ya mashahidi wawili kuwa wametoa unabii kwa miezi 42 katika nguo za magunia, Jumuiya ya Wakristo ilitumia uvutano wayo wa kilimwengu kusababisha ‘wauawe.’ Yohana anaandika: “Na wakati wao wamekwisha kumaliza kushuhudu kwao, hayawani-mwitu ambaye hupanda kutoka katika abiso atafanya vita na wao na kushinda wao na kuua wao. Na maiti zao zitakuwa katika njia pana ya jiji kubwa ambalo kwa maana ya kiroho huitwa Sodoma na Misri, ambako pia Bwana yao alitundikwa kwenye nguzo. Na wale wa vikundi vya watu na makabila na ndimi na mataifa watatazama maiti zao kwa siku tatu na nusu, na wao hawaruhusu maiti zao zilazwe katika kaburi. Na wale wanaokaa juu ya dunia hushangilia juu yao na kujifurahisha wenyewe, na wao watapelekeana zawadi, kwa sababu manabii wawili hawa walitesa wale wanaokaa juu ya dunia.”—Ufunuo 11:7-10, NW.
20. Ni nini “hayawani-mwitu ambaye hupanda kutoka katika abiso”?
20 Hili ndilo la kwanza la marejezo 37 katika Ufunuo kwa hayawani-mwitu. Wakati uwadiapo tutachunguza huyu na hayawani wengine kwa ukamili. Kwa sasa yatosha kusema kwamba “hayawani-mwitu ambaye hupanda kutoka katika abiso” ni ubuni wa Shetani, mfumo wa mambo wa kisiasa ulio hai.b—Linga Ufunuo 13:1; Danieli 7:2, 3, 17.
21. (a) Wale maadui wa kidini wa mashahidi wawili walitumiaje kwa faida yao hali ya vita? (b) Uhakika wa kwamba zile maiti za mashahidi wawili ziliachwa bila kuzikwa ulionyesha nini? (c) Kipindi cha wakati cha siku tatu na nusu chapasa kionweje? (Ona kielezi cha chini.)
21 Kutoka 1914 kufika 1918 mataifa yalikuwa yakishughulika na vita ya kwanza ya ulimwengu. Hisi za utukuzaji wa taifa zilipanda juu, na katika masika ya 1918, maadui wa kidini wa mashahidi wawili walijifaidi na hali hiyo. Walitumia kwa hila chombo cha Serikali cha kisheria hivi kwamba wahudumu wenye madaraka miongoni mwa Wanafunzi wa Biblia walitiwa gerezani kwa mashtaka bandia ya kufitini serikali. Wafanya kazi wenzi waaminifu waliduwaa. Utendaji wa Ufalme karibu ulikoma. Ilikuwa kana kwamba ile kazi ya kuhubiri ilikuwa imekufa. Katika nyakati za Biblia ulikuwa utovu wa heshima mbaya sana kutolazwa katika kaburi la ukumbusho. (Zaburi 79:1-3; 1 Wafalme 13:21, 22) Kwa hiyo, suto kubwa lingeshikamana na kuacha mashahidi wawili bila kuzikwa. Katika hewa yenye joto ya Palestina, maiti ikiwa peupe katika barabara wazi ingeanza kuvunda kikweli baada ya siku tatu na nusu halisi.c (Linga Yohana 11:39.) Elezo hili lenye mambo mengi katika unabii huonyesha aibu ambayo hao mashahidi wawili walilazimika kuvumilia. Hao ambao wametajwa hapo juu ambao walitiwa gerezani hata walikatazwa dhamana wakati kesi zao zilipokuwa kwenye rufani. Walifichuliwa peupe muda mrefu kutosha kuwa uvundo kwa wakazi wa “jiji kubwa.” Lakini hili “jiji kubwa” lilikuwa nini?
22. (a) Ni nini jiji kubwa? (b) Vichapo vya umma vilijiungaje na viongozi wa kidini katika kushangilia juu ya kunyamazishwa kwa mashahidi wawili? (Ona kisanduku.)
22 Yohana anatupa sisi madokezo fulani. Yeye anasema kwamba Yesu alitundikwa kwenye nguzo huko. Hivyo mara moja sisi tunafikiria Yerusalemu. Lakini yeye anasema pia kwamba hilo jiji kubwa linaitwa Sodoma na Misri. Basi, Yerusalemu halisi liliitwa Sodoma wakati mmoja kwa sababu ya mazoea yalo machafu. (Isaya 1:8-10; linga Ezekieli 16:49, 53-58.) Na Misri, ile serikali ya ulimwengu kubwa ya kwanza, nyakati nyingine huonekana ikiwa picha ya huu mfumo wa mambo wa ulimwengu. (Isaya 19:1, 19; Yoeli 3:19) Kwa sababu hiyo, jiji hili kubwa ni picha ya “Yerusalemu” lililochafuliwa ambalo hudai kuabudu Mungu lakini ambalo limekuwa chafu na lenye dhambi, kama Sodoma, na sehemu ya huu mfumo wa wambo wa ulimwengu wa kishetani, kama Misri. Ni picha ya Jumuiya ya Wakristo, ambayo ni kisawe cha Yerusalemu lisilo jaminifu, tengenezo ambalo washiriki walo walikuwa na sababu kubwa sana ya kushangilia wakati waliponyamazisha ile kazi sumbufu ya mashahidi wawili ya kuhubiri.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
c Angalia kwamba katika kuchunguza yanayopata maono ya watu wa Mungu wakati huu, inaonekana kwamba ingawa miezi 42 huwakilisha miaka mitatu na nusu halisi, siku tatu na nusu haziwakilishi kipindi halisi chenye saa 84. Inaelekea kwamba, kipindi mahususi cha siku tatu na nusu kimetajwa mara mbili (katika mstari wa 9 na 11) kukazia kwamba kingekuwa kipindi kifupi tu kikilinganishwa na miaka mitatu na nusu ya utendaji inayokitangulia.
-