Wimbo Na. 52
Linda Moyo Wako
Makala Iliyochapishwa
1. Linda sana moyo wako;
Uepuke dhambi.
Mungu husoma mioyo,
Tulivyo moyoni.
Moyo hupotosha wengi;
Ni mudanganyifu.
Tuulinde moyo wetu;
Tembea na Mungu.
2. Tayarisha moyo wako;
Sali kwa bidii.
Yanayokuhangaisha,
Mujulishe Mungu.
Twapaswa kutii mambo,
Atufundishayo.
Ushikamane na Yeye,
Fanya apendayo.
3. Linda sana moyo wako;
Tafakari mema.
Neno lipenye moyoni,
Likuimarishe.
Yehova anawapenda
Washikamanifu.
Mwabudu kwa moyo wote;
Awe rafikiyo.
(Ona pia Zab. 34:1; Flp. 4:8; 1 Pet. 3:4.)