Wimbo Na. 97
Songeni Mbele, Enyi Wahudumu wa Ufalme!
1. Songeni mbele, tangazeni,
Wote na wasikie.
Na tusaidie wapole,
Wote wajiunge na sisi.
Utumishi wetu kwa Mungu,
Kwa kweli ni pendeleo.
Basi twende tukatangaze,
Jina tukufu la Mungu.
(KORASI)
Songa mbele,
Tangaza Ufalme kwa ujasiri.
Songa mbele,
Simama upande wake Yehova.
2. Wa’budu wa kweli songeni,
Tuzo tazamieni.
Mwigeni Yesu Bwana wetu,
Ufalme tangazeni.
Wote wapate kusikia,
Ujumbe huo muhimu.
Twamutegemea Yehova,
Hatuogopi chochote!
(KORASI)
Songa mbele,
Tangaza Ufalme kwa ujasiri.
Songa mbele,
Simama upande wake Yehova.
3. Tunasonga mbele pamoja,
Mabaki na kondoo.
Wazee, vijana, na wake,
Sambamba na ukweli.
Tuna huduma takatifu,
Hatufanyi kidesturi.
Mungu wetu tumupendeze,
Kwa mwenendo wetu safi.
(KORASI)
Songa mbele,
Tangaza Ufalme kwa ujasiri.
Songa mbele,
Simama upande wake Yehova.
(Ona pia Zab. 23:4; Mdo 4:29, 31; 1 Pet. 2:21.)