Wimbo Na. 138
Jina Lako Ni Yehova
Makala Iliyochapishwa
Mungu liye hai—
Wa kweli na Muumba
Yehova jina lako—
Halibadiliki.
Tunajivunia
Kuitwa jina lako.
Na duniani kote,
Sifa twatangaza.
(KORASI)
Yehova, Yehova,
Wewe ndiye Mungu.
Mbinguni na duniani
Hakuna mwingine.
Ni wewe tu Mweza-Yote,
Wote watambue.
Yehova, Yehova,
Hatuna Mungu mwingine.
Watufanya tuwe,
Kile unachotaka.
Yehova jina lako—
Nasi twakutii.
Mashahidi wako
Umetuita hivyo.
Heshima kubwa sana—
Kuwa watu wako.
(KORASI)
Yehova, Yehova,
Wewe ndiye Mungu.
Mbinguni na duniani
Hakuna mwingine.
Ni wewe tu Mweza-Yote,
Wote watambue.
Yehova, Yehova,
Hatuna Mungu mwingine.
(Ona pia 2 Nya. 6:14; Zab. 72:19; Isa. 42:8.)